GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,054
- 107,538
Ni kweli hakuna ambaye alikuwa hajui kwamba huyu Mama Mndeme alikuwa na bonge la ' Bifu ' na aliyekuwa ' Bosi ' wake na ambaye ni Mkuu wa Mkoa aliyeondolewa Bwana Jordan Rugimbana hali ambayo kiukweli kwa 95% ndiyo imepelekea Yeye kuondoshwa hapo hasa baada ya kuonekana kusingekuwa na ' tija ' katika huo Mkoa ambao pia ndiyo Mji Mkuu wa Tanzania wa Dodoma.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida kabisa kuna ' Mtangazaji ' mmoja wa tv moja ' pendwa ' hapa Tanzania leo siku nzima alipofungua tu Kipindi alianza kuonyesha dhahiri kwamba anafufahia huku akiwa anamcheka Kinafiki na Kidharau Bwana Rugimbana kwamba kaondolewa Ukuu wa Mkoa halafu hapo hapo akawa anatumia muda mwingi ' Kumpamba ' Mama Mndeme ambaye jana alipandishwa kutoka Ukuu wa Wilaya na kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ' cheo ' ambacho alikuwa nacho ' Bosi ' wake ambaye walikuwa na ' Bifu ' kali sana.
Cha kusikitisha zaidi nadhani huyu Mtangazaji alikuwa ama hajui au amesahau kwamba hata Watazamaji wao wengi pia ni Watendaji wa karibu na Mheshimiwa Rais lakini na hata Rais mwenyewe huwa anawatizama kila asubuhi hivyo ' ubwabwaji ' wake wa leo huku kila mara akijigamba kwamba huyo Mama ni Mtu wake wa Karibu sana na kwamba hata Yeye amefurahi kusikia kwamba amepandishwa na kuwa Mkuu wa Mkoa.
Wakati huyu Mtangazaji akiendelea ' Kubwabwaja ' zake kama ilivyo kawaida yake mara akatokea tena ' Mchekeshaji ' mmoja maarufu mno kwa sasa hapa nchini ambaye siku chache tu zilizopita ' Israeli Mtoa Roho ' alimkosakosa kumpeleka Mbinguni ambaye na yeye pia akaanza kumwagia ' misifa ' kibao huyo Mama hadi kuongea mambo mengine ya ' Kibinafsi ' nae hali ambayo kwa Watendaji wa ' System ' wanaoijua vyema Kazi yao walianza kushtuka kisha wakatathmini upya ' uteuzi ' wa huyo Mama Mndeme na kugundua ya kwamba kwa hali iliyokuwepo si vyema akawa Mkuu wa Mkoa huo wa Dodoma japo ni Mtendaji mzuri ila ahamishwe Mkoa mwingine na ndipo wakaenda kwa Bwana Mkubwa / Taita wa Magogoni Feri na kumshauri amuhamishe Mkoa na kweli akapelekwa Ruvuma na yule wa Ruvuma Mzee Mahenge akaletwa Dodoma.
Kilichotokea leo nadhani kinapashwa kuwa ni Funzo kwa Watu wote kwamba hata kama Wewe unajuana au una ukaribu na ' Mkubwa ' fulani Serikalini ila si vyema sana ukaja kutuonyesha Sisi Watu wengine huo ukaribu wenu kwani kuna uwezekano huku kuonyesha Kwenu ukaribu ndiyo ukawa chanzo cha hata Wao kuanza kufuatiliwa ' nyendo ' zao na hatimaye mkajikuta mnawaharibia ' Vibarua ' vyao na wanarudi zao ' Uraiani ' kusota tena.
Na pia nitoe ' Wito ' hasa kwa Wanawake wa Kitanzania kwamba jifunzeni kuwa na Kifua, staha pamoja na uvumilivu pindi jambo fulani jema linapokutokea. Inasemekana mara baada tu ya kutangazwa jana kuwa ameteuliwa kuwa Mkuu wa huo Mkoa wa Dodoma huyu Mama muda mwingi aliutumia kufurahi huku akishirikiana na ' Mashosti ' zake kupiga ' Vijembe ' vya mbaya wake / adui yake Mkuu wa Mkoa aliyeondolewa Bwana Rugimbana bila kusahau na kutuma meseji kadhaaa za Kimafumbo na Kimajungu huku akisahau kwamba tokea jana alikuwa akifuatiliwa na wenye ' Kazi ' yao.
Haya Mama kila la kheri sasa huko Ruvuma ambako umepangiwa na Wewe Mtangazaji jaribu sana kupunguza ' Kiherehere ' chako cha kujifanya unajuana na ' Wakubwa ' wote wa nchi hii japo najua na hili nalisema waziwazi kwamba kuwa kuna Mwana Mama mmoja ambaye amekuteua kuwa ' Balozi ' wake katika Taasisi yake huko Mkoani Mbeya umemtumia aweze kukufanyia ' upatu ' kwa ' Bwana Mkubwa ' ili uteuliwe kuwa Mkuu wa Wilaya na niseme tu rasmi usiku huu kwamba huko ' Kujipendekeza ' Kwako kwa huyo Mama ambaye pia ni Naibu wa ' Mhimili ' mmoja wenye nguvu hapa nchini umezaa ' matunda ' kwani muda wowote kuanzia sasa pakitangazwa Wakuu wapya wa Wilaya basi na Wewe pia utakuwepo na hatimaye kuweza kuwaacha hapo katika hiyo tv huyo ' Emolo ' wenu na huyo Mwanadada wa Kikenya asiyeweza kutamka vizuri neno ' Kutengeneza ' na husema ' Kutengeza '.
Nawasilisha.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida kabisa kuna ' Mtangazaji ' mmoja wa tv moja ' pendwa ' hapa Tanzania leo siku nzima alipofungua tu Kipindi alianza kuonyesha dhahiri kwamba anafufahia huku akiwa anamcheka Kinafiki na Kidharau Bwana Rugimbana kwamba kaondolewa Ukuu wa Mkoa halafu hapo hapo akawa anatumia muda mwingi ' Kumpamba ' Mama Mndeme ambaye jana alipandishwa kutoka Ukuu wa Wilaya na kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ' cheo ' ambacho alikuwa nacho ' Bosi ' wake ambaye walikuwa na ' Bifu ' kali sana.
Cha kusikitisha zaidi nadhani huyu Mtangazaji alikuwa ama hajui au amesahau kwamba hata Watazamaji wao wengi pia ni Watendaji wa karibu na Mheshimiwa Rais lakini na hata Rais mwenyewe huwa anawatizama kila asubuhi hivyo ' ubwabwaji ' wake wa leo huku kila mara akijigamba kwamba huyo Mama ni Mtu wake wa Karibu sana na kwamba hata Yeye amefurahi kusikia kwamba amepandishwa na kuwa Mkuu wa Mkoa.
Wakati huyu Mtangazaji akiendelea ' Kubwabwaja ' zake kama ilivyo kawaida yake mara akatokea tena ' Mchekeshaji ' mmoja maarufu mno kwa sasa hapa nchini ambaye siku chache tu zilizopita ' Israeli Mtoa Roho ' alimkosakosa kumpeleka Mbinguni ambaye na yeye pia akaanza kumwagia ' misifa ' kibao huyo Mama hadi kuongea mambo mengine ya ' Kibinafsi ' nae hali ambayo kwa Watendaji wa ' System ' wanaoijua vyema Kazi yao walianza kushtuka kisha wakatathmini upya ' uteuzi ' wa huyo Mama Mndeme na kugundua ya kwamba kwa hali iliyokuwepo si vyema akawa Mkuu wa Mkoa huo wa Dodoma japo ni Mtendaji mzuri ila ahamishwe Mkoa mwingine na ndipo wakaenda kwa Bwana Mkubwa / Taita wa Magogoni Feri na kumshauri amuhamishe Mkoa na kweli akapelekwa Ruvuma na yule wa Ruvuma Mzee Mahenge akaletwa Dodoma.
Kilichotokea leo nadhani kinapashwa kuwa ni Funzo kwa Watu wote kwamba hata kama Wewe unajuana au una ukaribu na ' Mkubwa ' fulani Serikalini ila si vyema sana ukaja kutuonyesha Sisi Watu wengine huo ukaribu wenu kwani kuna uwezekano huku kuonyesha Kwenu ukaribu ndiyo ukawa chanzo cha hata Wao kuanza kufuatiliwa ' nyendo ' zao na hatimaye mkajikuta mnawaharibia ' Vibarua ' vyao na wanarudi zao ' Uraiani ' kusota tena.
Na pia nitoe ' Wito ' hasa kwa Wanawake wa Kitanzania kwamba jifunzeni kuwa na Kifua, staha pamoja na uvumilivu pindi jambo fulani jema linapokutokea. Inasemekana mara baada tu ya kutangazwa jana kuwa ameteuliwa kuwa Mkuu wa huo Mkoa wa Dodoma huyu Mama muda mwingi aliutumia kufurahi huku akishirikiana na ' Mashosti ' zake kupiga ' Vijembe ' vya mbaya wake / adui yake Mkuu wa Mkoa aliyeondolewa Bwana Rugimbana bila kusahau na kutuma meseji kadhaaa za Kimafumbo na Kimajungu huku akisahau kwamba tokea jana alikuwa akifuatiliwa na wenye ' Kazi ' yao.
Haya Mama kila la kheri sasa huko Ruvuma ambako umepangiwa na Wewe Mtangazaji jaribu sana kupunguza ' Kiherehere ' chako cha kujifanya unajuana na ' Wakubwa ' wote wa nchi hii japo najua na hili nalisema waziwazi kwamba kuwa kuna Mwana Mama mmoja ambaye amekuteua kuwa ' Balozi ' wake katika Taasisi yake huko Mkoani Mbeya umemtumia aweze kukufanyia ' upatu ' kwa ' Bwana Mkubwa ' ili uteuliwe kuwa Mkuu wa Wilaya na niseme tu rasmi usiku huu kwamba huko ' Kujipendekeza ' Kwako kwa huyo Mama ambaye pia ni Naibu wa ' Mhimili ' mmoja wenye nguvu hapa nchini umezaa ' matunda ' kwani muda wowote kuanzia sasa pakitangazwa Wakuu wapya wa Wilaya basi na Wewe pia utakuwepo na hatimaye kuweza kuwaacha hapo katika hiyo tv huyo ' Emolo ' wenu na huyo Mwanadada wa Kikenya asiyeweza kutamka vizuri neno ' Kutengeneza ' na husema ' Kutengeza '.
Nawasilisha.