Kigwangalla apinga Spika kuleta madaktari wa India Apollo, apingwa na wenzake!

Huyu lusinde nashindwa kumwelewa kama amekamilika kibinadamu, maana kauli zake hazina muwala kabisa
 
Kigwangala ana point nzuri tu, lakini tatizo anapigania maslahi ya madaktari na wananchi kwa ujumla from a very wrong angle!
 
Najua madaktari wa India watakuja na vipimo tu bila dawa, hivyo baada ya vipimo tutashuhudia wabunge wakimiminika india kwa ajili ya kitakachoitwa matibabu..maana viongozi wetu wengi wagonjwa angalia tu kikombe cha babu Loliondo walivyomiminika kwa wingi.!
 
Makinda kumbe mawazo yake ni sawa kabisa na Lusinde?kweli ukitaka kujua busara za mtu aliekaa kimya mpe madaraka kidogo na nafasi ya kuongea!!utashangaa......Bunge limekosa mwelekeo katika historia na nchi hii,wanajadili upuuzi mtupu!mambo ya msingi wanayakimbiaa wanalinda chama!damn shit
 
Ni mawazo mazuri ya Kigwangula. mimi nahisi tungeenda mbali zaidi, nako ni kuweka utaratibu maalum wa hawa
wabunge kwenda India kutibiwa!! sasa hivi wamekuja na fashion hata kucheki malaria au BP wanaenda India
(hivi wanatumia hela gani hawa jamaa)??

Hivi mtu kama huyu anaweza kuikalia serikali kooni ili huduma za afya ziboreshwe ilhali yeye anaenda India kila uchao!
Hakuna haja ya kwenda popote, ikibidi kufa afe hapa2 tujue tatizo ni nini katika tiba zetu! vinginevyo aende huko kama
private patient, hela ya mlipa kodi isitumike!
 
Leo kwenye kikao cha 'briefing' cha wabunge, mbunge wa nzega Mh Dkt. Hamis Kigwangalla amejikuta ktk wakati mgumu alipoamua kuweka wazi msimamo wake kuwa hakubaliani na mpango wa spika wa bunge Mh Anne Makinda kuwaalika madaktari bingwa kutoka hospitali za Apollo kule India kuja kuwacheki afya wabunge. Kigwangalla alisema: 'serikali ya Tanzania chini ya Rais Kikwete imefanya jitihada kubwa sana kusomesha wataalam mabingwa hususani kwenye fani za moyo, viungo, meno, mafigo na hawajashindwa kubaini na kutibu magonjwa ya wabunge wa Tanzania mpaka tuite wahindi kuja kubaini liffestyle problems za wabunge wetu, itakuwa ni kuwadharau wataalam wetu, kutumia vibaya pesa za walipa kodi na zaidi ni kujiona sisi ni muhimu na special zaidi kuliko waliotuchagua...mimi napinga mpango huu na ninakushauri Mh Spika usituletee aibu ya kuwa wasaliti kwa wananchi ambao tunapaswa kuwatetea wapate huduma bora za afya...'
Wabunge wengi walionekana wakiguna kuonesha kuwa wanampinga.

Mh Lusinde Livingstone alimpinga akisema 'tusione aibu kutafuta tiba za afya zetu...pengine wengine wanatoa michango ya hovyo hapa kwa sababu wana homa vichwani mwao'

Mh George Mkuchika naye akasema: 'kwa mara ya kwanza frequency zangu zimeoana na za Kigwangalla...hebu limalizeni hili dada yangu Anne, litoe kwenye mpango wako, litatuaibisha...'

Ahsanteni,
Zul.

Mhh!!!!!!!
Only in TZ.
 
Namuunga mkono kwa 100% colleague wangu Dr Kigwangalla...hii ni kudhalilisha taaluma, kujiona wao bora na wana thamani zaidi, na matumizi mabovu ya kodi zetu. Sasa mpaka screening ya NCDs uchukue wataalamu toka Apollo!? Maspecialist vijana wenye skills wanagraduate kila mwaka toka vyuo vikuu vyetu wanashindwa kufanya screening ya NCDs! Dharau...
NCDs ni non-communicable diseases (magonjwa yasiyo ya kuambukiza), daktari Riwa kuna watu hapa uliwaacha njiani.

Kwa hili Kigwa has finally come to his senses.
 
Ukisikia viongozi wako out of touch ndio hii!!!
Nilichoona hapa ni kwamba speaker hajaelezea ukweli wote. Kinachoonekana kutaka kufanywa na Speaker ni kuwaleta madaktari ambao watatoa recommendations za wabunge kuwa wanaenda India kwa regular check up kama preventive programs. Speaker ameona hakuna mwanya wa kupata recommendations kwa kupitia mdaktari wa nchini kwa sababu basically hakuna daktari wa Tanzania anachoshindwa kufanya ambacho anaweza kufanya daktari wa India. Naona sasa wabunge hawaridhiki na kutiba India wanataka mpaka prevention check ups wawe wanalipiwa kwenda India!!!
Inasikitisha...
 
Daah amakweli kila kikao cha bunge kina kioja chake. Makinda hii kali ya mwaka. Tanzania madaktari kibao, hao sunche wanini huku kwetu. Mwee au wanaogopa kujilikana status zao kiafya? Waende mirembe wakafanyiwe EEG kwanza. Mengine sisemi.
 
Nadhani wabunge wengi wanaogopa madaktari wa hapa bongo kutokana na kitu ambacho serikali imemfanyia dr ulimboka. Wanajua kuwa madaktari bado wana kinyongo nao hasa waliokuwa mstari wa mbele kuwapondea waliokuwa kwenye mgomo
 
Leo kwenye kikao cha 'briefing' cha wabunge, mbunge wa nzega Mh Dkt. Hamis Kigwangalla amejikuta ktk wakati mgumu alipoamua kuweka wazi msimamo wake kuwa hakubaliani na mpango wa spika wa bunge Mh Anne Makinda kuwaalika madaktari bingwa kutoka hospitali za Apollo kule India kuja kuwacheki afya wabunge. Kigwangalla alisema: 'serikali ya Tanzania chini ya Rais Kikwete imefanya jitihada kubwa sana kusomesha wataalam mabingwa hususani kwenye fani za moyo, viungo, meno, mafigo na hawajashindwa kubaini na kutibu magonjwa ya wabunge wa Tanzania mpaka tuite wahindi kuja kubaini liffestyle problems za wabunge wetu, itakuwa ni kuwadharau wataalam wetu, kutumia vibaya pesa za walipa kodi na zaidi ni kujiona sisi ni muhimu na special zaidi kuliko waliotuchagua...mimi napinga mpango huu na ninakushauri Mh Spika usituletee aibu ya kuwa wasaliti kwa wananchi ambao tunapaswa kuwatetea wapate huduma bora za afya...'
Wabunge wengi walionekana wakiguna kuonesha kuwa wanampinga.

Mh Lusinde Livingstone alimpinga akisema 'tusione aibu kutafuta tiba za afya zetu...pengine wengine wanatoa michango ya hovyo hapa kwa sababu wana homa vichwani mwao'

Mh George Mkuchika naye akasema: 'kwa mara ya kwanza frequency zangu zimeoana na za Kigwangalla...hebu limalizeni hili dada yangu Anne, litoe kwenye mpango wako, litatuaibisha...'

Ahsanteni,
Zul.
NImekumbuka ule wimbo wa Tanzania,Tanzania nakupenda kwa moyo wote nchi yangu Tanzania.........mtanisaidia kumalizia
 
Huu ni Ufisadi, Kuna haja ya walalahoi kuwatimua hawa wapuuzi huko Dodoma, na kulifunga bunge mpaka tutakapoapata wabunge wenye akili timamu
 
Hivi wanajua kuwa kuna mamilioni ya watanzania wanakufa vijijini kwa sababu hakuna dawa za kutibu malaria? hawahitaji check up, wanajulikana kuwa wanaumwa malaria, lakini hawana dawa na wanakufa.
Wabunge wanashindwa kuishi vizuri qwenyewe na kujipatia life style diseases wanataka kuagiza madaktari kutoka India kuja kuchunguza afya zao! Kwa nini hao madaktari wasipelekwe vijijini kutibu wazalishaji?
 
Mh Lusinde Livingstone alimpinga akisema 'tusione aibu kutafuta tiba za afya zetu...pengine wengine wanatoa michango ya hovyo hapa kwa sababu wana homa vichwani mwao'

Kweli Lusinde ana mtindio wa ubongo! apelekwe mirembe ASAP.

Damu za ngómbe zimemdhuru tangu siku nyingi alipokuwa machinjioni mitaa ya Mombasa kuelekea Gongolamboto.
 
Hofu ya wabunge ni juu ya maradhi yao kujulikana kwa madaktari wakitanzania....
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom