Kigwangalla ajitetea kuwa yeye sio fisadi na hakula pesa za Umma. Yupo tayari kula kiapo kwa Quran hadharani

Kamanda Asiyechoka

JF-Expert Member
Sep 13, 2020
3,166
4,581
Amefunguka
👇
====
FqmWZXpWYAAXrjO

Alichokisema Hamis Kigwangalla katika majadiliano ClubHouse

Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini, Dkt. Hamis Kigwangalla amezungumza kwenye majadiliano ya Clubhouse na kuelezea msimamo wake kuhusu suala la kuapa kwa kutumia Quran na kashfa za rushwa zinazomkabili.
Akizungumza kwenye majadiliano hayo, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba yeye ni Muislamu na anaweza kuapa hadharani kwa kutumia Quran kuthibitisha kwamba hakuchukua fedha za Urithi Festival na wala hakutumia ndege za TANAPA kwa maslahi yake binafsi.

Kuhusu suala la vibali kwa raia wa Tanzania kuingia na kutoka wanavyotaka na haki nyingine kama kumiliki ardhi, Dkt. Kigwangalla alisema kuwa hata kama kuna wasiwasi wa masuala ya usalama, ni vyema vibali hivyo vikutolewe ili kukuza uchumi. Alisema kwamba mambo mengi yanakwama nchini siyo kwa sababu watu hawajasoma, bali ni kutokana na ukosefu wa exposure.

Akizungumzia kashfa ya rushwa inayomkabili, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba rushwa ni kitu kibaya sana na kiongozi yeyote anayehongwa huwezi kusimamia haki na kutoa maamuzi sahihi. Aliongeza kuwa yeye sio mtu wa kuchukua rushwa na kama kuna wanasiasa watatu nchini ambao hawachukui rushwa, hawezi kuachwa nyuma.

Kuhusu suala la uwajibishwaji, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba uliopo ni mdogo sana na sio wa kiwango kinachotisha watumishi waliopo kwenye ofisi ili wasifanye ubadhirifu. Alisisitiza kwamba kuna haja ya kudai uwajibikaji zaidi.

Akitoa ufafanuzi kuhusu madai kwamba alitumia ndege za TANAPA kwenda kutalii na wanawake, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba ni uongo tu na kwamba mara zote alikuwa analipa gharama zote kwa fedha zake mwenyewe.

Mwisho, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba yeye sio mtu wa mambo ya kichini chini na anasema mambo hadharani ambayo siyo sawa. Alisema kwamba watu wanaofanya mambo chini chini na kuandika barua kwenda kwa wakubwa wanaonekana kuwa viongozi wazuri, lakini yeye na wengine kama yeye ambao wanasema mambo hadharani ndio wanaonekana kuwa viongozi wabaya.

Jamii Forums
 
Yeye si alisema hakuna hamisi fala? Kwamba watu wanashindwa ku think outside the box.

Naomba na huo ubunge wake uishe sasa ili tuone jinsi gani anaweza kufikiria nje ya box. Maana wanakuwaga na mbwembwe sana wakiwa kwenye ma Vx V8 meusi
 
Mbunge wa Nzega Kigwangala amesema ukiambiwa utaje watu watatu wa juu wasiochukua Rushwa nchi hii huwezi kuacha kumtaja na yeye.

Dr. Kigwangala amesema yeye anaswali na ana hofu ya Mungu na yuko tayari kuapa kwa Quran kwamba hajawahi kutumia Ndege za Tanapa kwenda kula bata na wanawake wazuri.

Chanzo: Jambo TV

Nchi ngumu sana hii!

===
Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini, Dkt. Hamis Kigwangalla amezungumza kwenye majadiliano ya Clubhouse na kuelezea msimamo wake kuhusu suala la kuapa kwa kutumia Quran na kashfa za rushwa zinazomkabili.
Akizungumza kwenye majadiliano hayo, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba yeye ni Muislamu na anaweza kuapa hadharani kwa kutumia Quran kuthibitisha kwamba hakuchukua fedha za Urithi Festival na wala hakutumia ndege za TANAPA kwa maslahi yake binafsi.

Kuhusu suala la vibali kwa raia wa Tanzania kuingia na kutoka wanavyotaka na haki nyingine kama kumiliki ardhi, Dkt. Kigwangalla alisema kuwa hata kama kuna wasiwasi wa masuala ya usalama, ni vyema vibali hivyo vikutolewe ili kukuza uchumi. Alisema kwamba mambo mengi yanakwama nchini siyo kwa sababu watu hawajasoma, bali ni kutokana na ukosefu wa exposure.

Akizungumzia kashfa ya rushwa inayomkabili, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba rushwa ni kitu kibaya sana na kiongozi yeyote anayehongwa huwezi kusimamia haki na kutoa maamuzi sahihi. Aliongeza kuwa yeye sio mtu wa kuchukua rushwa na kama kuna wanasiasa watatu nchini ambao hawachukui rushwa, hawezi kuachwa nyuma.

Kuhusu suala la uwajibishwaji, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba uliopo ni mdogo sana na sio wa kiwango kinachotisha watumishi waliopo kwenye ofisi ili wasifanye ubadhirifu. Alisisitiza kwamba kuna haja ya kudai uwajibikaji zaidi.

Akitoa ufafanuzi kuhusu madai kwamba alitumia ndege za TANAPA kwenda kutalii na wanawake, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba ni uongo tu na kwamba mara zote alikuwa analipa gharama zote kwa fedha zake mwenyewe.

Mwisho, Dkt. Kigwangalla alisema kwamba yeye sio mtu wa mambo ya kichini chini na anasema mambo hadharani ambayo siyo sawa. Alisema kwamba watu wanaofanya mambo chini chini na kuandika barua kwenda kwa wakubwa wanaonekana kuwa viongozi wazuri, lakini yeye na wengine kama yeye ambao wanasema mambo hadharani ndio wanaonekana kuwa viongozi wabaya.
 
Rushwa huwa ina pande mbili, upande wa utoaji na uchukuaji.

Hivyo Kigwa huenda yupo sahihi kwa kuuongelea upande wa uchukuaji.

Maana ambalo nina uhakika nalo ni mtoaji mzuri sana wa Rushwa
 
Hamisi bwana, Hamisi mimi najua ni tajiri kwenye kilimo huko... Tena wakati huu ni vyema akachukua nafasi ya Mo Dewji pale Simba kwenye uwekezaji.
 
Back
Top Bottom