Kigugumizi (Stuttering): Chanzo na Tiba kwa watu wazima na watoto

mamamia ametoa mchango mzuri sana na kiresula ufuate huo ushauri utakusaidia sana

mimi binafsi nilikuwa na kigugumizi kikali sana hadi miaka 8. kila nilipokuwa nashindwa kabisa kutamka neno na wenzangu kunicheka nilikuwa nalia sana, nilikuwa najisiakia vibaya na mara nyingi nilikuwa najisikia aibu kuongea mbele ya wenzangu. kwa uzoefu wangu:

1. baadhi ya maneno ni magumu kutamka zaidi ya mengine

2. ukijiandaa kutamka neno huwa kinaongezeka kuliko kutamka bila kujiandaa

3. kutamka pamoja na kuimba (kama alivyofafanua mamamia) kunarahisisha kutamka na kunaweza kufunika kabisa kisionekane

4. mtu akiudhiwa na kukasirika hata kwa kiasi kidogo tu ama akiwa na wasiwasi huongezeka

bahati mbaya sikusoma nursery school na sikuwahi kufundishwa na mwalimu anayejua saikolojia ya watoto wakati wa utoto wangu. namshukuru Mungu nilifanikiwa kufanya mazoezi mawili makubwa na nikakimaliza kabisa hadi leo sina hata kidogo, ooh, glory to God!

mazoezi hayo ni

1. kutamka neno lililokuwa linanitatiza kwa kulirefusha (kulivuta) badala ya kulikata. mfano kutamka neno "mkutano" nilikuwa natamka ‘mkuuuuuutaaaaaano" badala ya "mku mku mku ku ku ta ta ta no" kwa hiyo nilikuwa kama naimba wimbo fulani hivi

2. kuweka kiambishi "a" au "ya" kabla ya neno lenye kutatiza kutamka (na wakati mwingine kukivuta kama nilivyofafanua katika (1) hapo juu kama neno litaendelea kuwa gumu kutamka). mfano neno "mkutano" nilikuwa natamka ‘amkutano" au "yamkutano" au wakati mwingine navuta hivyo viambishi na kutamka ‘aaaamkutano" au "yaaaamkutano"

kwa hiyo mpendwa unaweza kumhsawishi na kumfanyia mazoezi mwanao ajaribu mbinu hii huenda ikamsaidia kama ilivyonisaidia mimi. ila natoa tahadhari kuwa:

1. watu tumetofautiana. kwangu mimi viambishi hivi vya "a" na "ya" vilinirahisishia kutamka neno lolote ambalo lilikuwa linanisumbua. kwa hivyo inawezekana mimi mbinu hii ilinisaidia lakini mwingine isimsaidie.

2. umri wa mtoto waweza kumuwia vigumu kutumia mbinu hii, ila wewe mwenyewe na jamaa zako wengine walio watu wazima mnaweza kujaribu hii mbinu na mnaweza kuondokana na tatiza hili hata huku ukubwani

3. muwe watundu na wadadisi kwa kujaribu viambishi vingine mbalimbali kwani viambishi vilivyonisaidia mimi vinawezaa visiwasaidie nyinyi lakini kukawa na viambishi vingine vyenye msaada kwenu kutegemeana na ndimi zenu. kwa hiyo jaribuni viambishi mbalimbali

kwa haya machache nawaombea faraja na baraka za Mungu
mbarikiwe sana na msife moyo wala kufadhaika,
Mungu anawapenda sana, anawapenda upeo!!
 
mwenye kigugumizi
1. SI MWONGO
2. NI MWAMINIFU
3. ALWAYS DIRECT TO THE POINT... he doesnt hit around the bush
 
Habari wanaJF,

Kuna mdogo wangu ana tatizo la kigugumizi cha kuongea kiasi kwamba hawezi kuzungumza bila kujipigapiga au kuruka!!Ningependa kujua chanzo cha tatizo hili na pia tiba yake kama ipo!!

Naomba kuwasilisha!!
 
the way is there any body knows where to get this kind of couse in Tanzania of CD programs of same kind?
 
Asante mkuu kwa mwanga huu!!nataman hiyo cure centre yao ingekuwa tz ili nimpeleke course ya hizo wiki 2 apone!!hivi unaweza kuwasiliana nao na wakakueleza tiba yake?
 
Habari wana jf,
Kuna mdogo wangu ana tatizo la kigugumizi cha kuongea kiasi kwamba hawezi kuzungumza bila kujipigapiga au kuruka!!Ningependa kujua chanzo cha tatizo hili na pia tiba yake kama ipo!!
Naomba kuwasilisha!!

Hahahaha mpaka achome choki ndo anazungumza
 
Afanye jaribio hili, kabla ya kuzungumza avute pumzi nyingi ndani na kuihold aongee kifua kikiwa kimejaa oxigen, atoe pumzi anapokuwa amemaliza sentesi, naliwahi kuambiwa kuwa hii ni tiba.
urudi/mrudi kwa ushuhuda.
 
Habari wana jf,
Kuna mdogo wangu ana tatizo la kigugumizi cha kuongea kiasi kwamba hawezi kuzungumza bila kujipigapiga au kuruka!!Ningependa kujua chanzo cha tatizo hili na pia tiba yake kama ipo!!
Naomba kuwasilisha!!

Pole sana kwa tatzo la mdogo wako....me nlizaliwa na kigugumizi but luckily nlifanyiwa therapy na mzazi wangu ambayo imeniondolea hlo tatzo mpaka kesho.

Kwanza elewa kigugumizi kipo associated na woga au hali ya ku panic so ndo maana mtu sometimes anashndwa anashndwa kuongea, so nakushauri umwambie mdogo wako ajifunze kuongea taratibu(kupunguza speed ya kuongea)na kingine ajijengee confidence ya kutosha...i'm sure it'll work since it worked for me. May god bless and cure your sibling coz i've been through the same road and it was horrible
 
Nakushkuru sana kaka!!hakika nimepata pa kuanzia na nadhan itamsaidia sana,God bless u
 
Habari wana JF,

Nina mtoto wangu first born ana miaka minne sasa,alianza kuwa na kigugumizi toka akiwa ameanza kujifunza kuongea,akiwa na miaka mitatu niliona kama kinazidi,nikaamua kuwaona wataalam na madaktari wa magonjwa ya watoto,na majibu niliyopata ni kwamba kwa kuwa bado ni mtoto nisubiri kidogo kitaisha tu kikizidi nirudi tena kuna dawa, sasa ni mwaka wa nne na naona kama kinazidi.

Mwezi huu nikaamua kwenda kwa Dr therapist mwingine na jibu aliloniambia ni kuwa stutterers (watu wenye kigugumizi) ni watu wenye akili sana kiasi kwamba akili yako inafanya kazi haraka kuliko midomo, kwamba midomo haiwezi ni ku copy na akili.Hapo Dr ndo akanichanganya kabsa,coz kwa maelezo yake mimi nahisi ni tatizo hilo,lakini yeye anasisitiza kuwa tena stutterers wana high IQ than average.

Kuhusu dawa kanishauri nisitumie dawa yoyote zaidi ya therapy, kutokumuudhi, watoto wenzie kutokumcheka, mazingira mazuri ya kuongea au kutokumkalipia, kwani alisema kwa sasa hakuna dawa zinazotibu, na dawa maarufu iliyo za anti-convulsants, anti-depressants, antipsychotic and antihypertensive medications, and dopamine antagonists ni ziko kwenye majaribio tu.

Am kind of confused please kama kuna watu wana hii experience nitashukuru sana mchango wao ili niwe na amani na mtoto wangu, manake siku hizi kuongea ni mpaka apige mguu chini yaani mpaka namwonea huruma mtoto wangu.
 
Usiwe na wasiwasi,mimi nina kigugumizi,ubaya tukikasirika hatuwezi kuongea aisee.sijui hata kigugumizi kinasababishwa na nini?
 
Mimi mwenyewe ni muhanga wa hilo tatizo but the way nilivyokua nakua kinapugua. mwambie akiongea aongee taratibu itamsaidia. keep calm coz its normal problem.
 
Mdogo wangu anayenifuata alikuwa na kigugumizi cha kutisha hasa na hatukutumia therapy yoyote ila kadiri alivyozidi kukua ile hali iliisha kabisa wala huwezi kujua kama alikuwa mhanga wa tatizo lile hivyo naamini mwanao anavyokua atapata improvement kubwa.
 
Niliambiwa kigugumizi kinampata mtoto akiwa mchanga ajaaza kuongea alfu matone ya mvuaa yakaingia mdomoni wakati analia.
 
Kumbe tunafanana hata mimi ninae sawasawa na wewe hilo jibu la doctor wa pili kwa hali fulani naliamini kupitia kwa huyu wangu maana kutokana na umri wake na mambo na maswali ambayo huwa ananiuliza huwa nabaki nimeduwaa.
 
Hii imenigusa Nina machache ya kukwambia....

Mimi pia nilikuwa na kigugumizi balaa! YAANI ilikuwa kuongea hadi nipige ukuta au mguu chini, nilipoanza Shule kimbembe ndio kilianza nilikuwa nataniwa sana kutokana na kigugumizi changu hili lini fanya nichukuie sana Shule, darasa la kwanza muhula wa pili nilikataa kata kata kwenda Shule ikabidi nihamishiwe Shule aliyokuwa anafundisha mama yangu ingawa ilikuwa mbali kidogo huko sikutaniwa sana coz nlikuwa mtoto wa mwalimu waliogopa kunitania.

Kigugumizi kiliendelea hadi nikiwa sekondari kipindi HICHI ndo ilikuwa worse nikiwa kwenye tension nlikuwa siwezi kuongea kabisa, ka ndo mwalimu yuko na kiboko afu ananihoji nilikuwa siwezi kuongea sometime ilibidi niandike...

Nikiwa form two nilipachikwa jina la BUBU sikulipenda kabisa lakini nlikuwa sina jinsi. Ila MABADILIKO ya mwili na kukua kwa sauti kulipunguza kidogo ingawa hakikuisha kabisa.

Nikiwa kwenye 18, 19 hivi kilipungua ni kawa naongea vizuri, ingawa Sasa naongea vizuri ila kuna circumstances zinafanya kigugumizi kurudi Kama nikiwa na furaha,hasira Kali, mshtuko, lakini CHA ajabu sana nikiwa napiga story na MKE wangu popote pale hata njiani nakuwa na kigugumizi ila akiongezeka Mtu mwingine kinaishia.. mkada nimeandika story hii ndefu ili kukupa darsa kidogo kuhusu Huyo kijana.

Kigugumizi kikali ni challenge especially katika maisha ya Shule. CHA muhimu Kuwa karibu na mwanao halafu mumpe NAFASI ya kumsikiliza na kuongea huwa tunapenda kusikilizwa hata ka tunademadema, pia ka Ana ndugu zake wambie wasimtanie na wawe wanamsikiliza.

Hii itampa faraja na kumpunguzia msongo. Kwa upande wangu at teenage age kigugumizi kilifanya nijiingize kwenye makundi, ukorofi, utumiaji wa migadarati, na ulevi ili nionekane na kupunguza huo ulemavu coz hata nyumbani nilikuwa nataniwa na wote hata wazazi..

Pia angalia na muongoze mwanao katika MAAMUZI mbali mbali coz watu wenye kigugumizi wana MAAMUZI ya ghafla na kakurupuka.. Kuhusu uwezo wa akili ni kweli ila hiyo ni talent inatakiwa Kuwa nurtured.

Sio magenious kiviile ila wana kumbukumbu Nzuri sana na ni fast learners, wana mult talent ka michezo, kuimba, kuchora, kutunga vitu na etc. Usipomguide atatumia talent vibaya mf. Uongo nlikuwa na uwezo wa kutunga uwongo fasta na watu wakaamini na nikakumbuka hata for two years nilidanganya nini.

Mimi nikiwa A level mwalimu mmoja wa Biology Mr.Kimaro RIP, aliniambia na Kuhusu kigugumizi alisema ka Huyo Dr. Wako alivyo sema, nilianza kufanya informal research kuhusu watu wenye vigugumizi nimeugundua mengi.
 
Mkuu nimecheka sana kutokana na maelezo yako, Kwetu karibia ukoo mzima una kigugumizi na tunatofautiana kwa ukali wa kigugumizi, kinara wetu ni Baba mkubwa yeye ana sauti nzito na inakata kata kama gari linalotaka kuzima vile .. Kutokana na tatizo ili kwetu asilimia kuwa tumekuwa ni watu wa hasira na jazba mno na watu tusiopenda maswali ya kujirudia Lol!

Maelezo yako yanalingana na hali niliyokumbana nayo wakati nakua, ni taabu sana kwa mtoto mwenye kigugumizi kushirikiana nawenzie vizuri hasa hasa mashuleni, cha muhimu ni mzazi kumjengea mtoto kujihamini maana nimegundua kuwa ukiwa na kigugumizi hasa wa watoto kunawaondolea kujihamini na hivyo kujikuta wapeke sana au atakupelekea kufanya vibaya chuleni......

Sitasahau mwaka 2008 nikiwa katikati ya watu wengi nikapigiwa simu na jamaa yangu wakaribu sana, ile tu nilivyopokea simu na kutaka kuitikia "hallow" ghafla nikashindwa kuunganisha HA na llow nikabaki HAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA ndani ya dakika moja na nusu. watu wengi walinishangaa sana na kuniuliza nilipatwa na kitu gani kwani wengi wao hawakufahamu kama nina kigugumizi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom