Kigoma Yatengwa! Usafiri balaa ..

Ibrah

JF-Expert Member
Mar 22, 2007
2,729
528
Hali ya usafiri wa Treni ambao ndiyo usafiri pekee wa uhakika kwenda mikoa mingine ni mbaya mno na inazidi kuwa mbaya siku hadi siku. Wasafiri wanasafiri bila taa kitu ambacho ni hatari kwa usalama na afya (maana kwenda haja usiku ni noma)

Kwa sasa usafiri wa Daraja la 3 ambao ndiyo unamudiwa na watu wengi ni adha tupu tiketi zinauzwa 8 tu na zimeisha! Ukibahatika kupata tiketi basi namba za siti zimegonganishwa kwa watu wengine wawili (na mtajuana wenyewe)na ni juu yenu kupangiana zamu ya kukaa! Ikiwa unataka kusafiri siku unayotaka inakupasa kulipa shilingi 45,000/- ili uweze pata tiketi ya kwenda Dar es Salaam nauli ambayo walipa wasafiri wa Kanda ya Ziwa kutoka Dar kupitia nchi jirani (Kenya na Uganda).
 
Ibrah, ni kuwapa pole ndugu zetu wa Kigoma... Unajua quality ya life after mwekezaji inategemea pia huyo mwekezaji nyumbani anaishije!!?? Kumbuka kwenye picha za treni/garimoshi India jamaa wanasafiri wakiwa wamekaa mpaka juu ya garimoshi lenyewe, kufika wanafika lakini ni adha tu ndio kidogo inakuwa tatizo!!

Mwekezaji mpya TRL (ndio jina jipya hilo after TRC) ametoka India....... So, we are to learn travelling Indian Style

Personally sitegemei mabadiliko makubwa kwenye hilo shirika letu......
 
Ibrah, ni kuwapa pole ndugu zetu wa Kigoma... Unajua quality ya life after mwekezaji inategemea pia huyo mwekezaji nyumbani anaishije!!?? Kumbuka kwenye picha za treni/garimoshi India jamaa wanasafiri wakiwa wamekaa mpaka juu ya garimoshi lenyewe, kufika wanafika lakini ni adha tu ndio kidogo inakuwa tatizo!!

Mwekezaji mpya TRL (ndio jina jipya hilo after TRC) ametoka India....... So, we are to learn travelling Indian Style

Personally sitegemei mabadiliko makubwa kwenye hilo shirika letu......

Asante sana Morani; hawa Wahindi wa TRL ndiyo wanaoendesha zile treni ambazo watu wanakaa hadi juu ya behewa. Duniani kote hakuna mahali penye usafiri duni wa Treni kama kule India.

Nakumbuka kuona picha ya namna hiyo kwenye magazeti yetu kama kuna mtu anazo atubandikie hapa.

Wakati Rais anafunga miaka 2 ya utawala kuna mwandishi alimwuliza kuhusu usafiri wa Reli , TRL an uwekezaji Muungwana akadai kuwa wakati wa TRC treni ilichukua hadi siku 8 kwenda Kigoma! Nilimshangaaa, maana haijawahi kutokea katika TRC Wasafiri kukaa siku 5 njiani ati kwa kuwa mabehewa ya mizigo yametokea never, Rais aliwadanganya WaTz! Kitu ambacho TRC walikuwa wakifanya ni kubadilisha Wasafiri kuhamia treni nyingine (kubadlishana) na ilikuwa sahihi kabis. Sijui Muungwana alipandaga Treni ya TRC lini!
 
Ibrah unataka kunitoa machoni.
Pamoja na serikali kuwa wabaguzi wakubwa sana na kuutenga mkoa wa kigoma makusudi lakini kinachochangia matatizo hayo kikubwa ni ukosefu wa wabunge makini.

Kigoma haijapata kuwa na MBUNGE Makini anayewatetea hata siku moja. Hukumbuki miezi kama miwili iliyopita tu iliwalazimu FFU kuingia kuwatoa wasalifiri waliokuwa wamekaliana vichwani.
Kwa kifupi ule sio usafiri.

Harafu angali wabunge wa kigoma siku ile ya ZITO walivyoshambuliana bungeni. Selukamba&Msambya dhidi ya ZITO.

Utafikiri ndicho kilicjhowapeleka bungeni.

Ni aibu sana ndugu zanguni,

Naomba Jambo forum itusaidie kutuokoa watu wa KIGOMA twafa.
 
Pale Mwanza kuna jamaa zangu kibao toka Kigoma, mara nyingi wamekuwa wakilalamikia suala usafiri. Ni vema suala hili sasa likatupiwa japo jicho la huruma...
 
Nafikiri Serikali inasubiri yatokee maafa ili Rais akaweke Mnara wa kumbukumbu katika eneo la Tukio. Kwa nini tunakuwa wazito kujifunza kutoka na uzembe wa yaliyopita. Watu wakifariki ndipo utamwona rais na watendaji wake wanauongelea usafari huu na kuwapa kifuta machozi wafiwa cha shs 50,000/-.

Mwekezaji gani huyu huduma inamshinda hadi anafika mahali huduma inakuwa duni zaidi ya ile aliyoikuta. Pia inasemekana Serikali imempa mtaji mtaji, it means ameenda kuinvest kwingine na kutuacha na matatizo yetu ya usafir ukizidi kuwa mbovu zaidi.

Siwezi kuwalaumu wawekezaji, they are here to make business, and not kuwafurahisha wabongo msafiri kwa starehe kama mko kwenye ndege ya chini. Viongozi wetu waliosaini mkataba na hawa jamaa ya kutoa huduma bora na kuboresha miundo mbinu ndio wa kulaumiwa. Hawatufai
!
 
Hali ya usafiri wa Treni ambao ndiyo usafiri pekee wa uhakika kwenda mikoa mingine ni mbaya mno na inazidi kuwa mbaya siku hadi siku. Wasafiri wanasafiri bila taa kitu ambacho ni hatari kwa usalama na afya (maana kwenda haja usiku ni noma)

Kwa sasa usafiri wa Daraja la 3 ambao ndiyo unamudiwa na watu wengi ni adha tupu tiketi zinauzwa 8 tu na zimeisha! Ukibahatika kupata tiketi basi namba za siti zimegonganishwa kwa watu wengine wawili (na mtajuana wenyewe)na ni juu yenu kupangiana zamu ya kukaa! Ikiwa unataka kusafiri siku unayotaka inakupasa kulipa shilingi 45,000/- ili uweze pata tiketi ya kwenda Dar es Salaam nauli ambayo walipa wasafiri wa Kanda ya Ziwa kutoka Dar kupitia nchi jirani (Kenya na Uganda).
Ibrah ni kweli usafir wa treni una matatitizo makubwa na si kwa Kigoma tu bali kwa wale wote wanaoitegemea reli ya kati hasa kule kusikopitiwa na barabara kuu. Yule mwekezaji wa kihindi tusitegemee miujiza kwani hatuoni lolote la kuvutia kule ambako amekuwa akiendesha reli kwa muda mrefu.

Hoja yako ya "jamhuri" pamoja na kutengwa kiusafiri haileti matumaini bali inaondoa kabisa matumaini. Isijekuwa kuna hoja za kujitenga? tunafahamu kuwa wenyeji wa mkoa huu wanashabihiana lugha na nchi jirani; na vilevile wakazi wengi wa pale Ujiji walipewa uraia na hayati Mwalimu mara tu baada ya uhuru.

Baadhi yetu tulifanyia kazi Kigoma kwa miaka kadhaa, tulitegemea zaidi usafiri wa barabara kupitia Kasulu-Kibondo-Nyakanazi, na huko tunajiunga na barabara kuu inayotokea mikoa ya kanda ya ziwa.
 
1. Viongozi toka Kigoma pia wamewaangusha wana Kigoma- kusema kweli sijawahi ona msukumo wa kweli toka kwa viongozi wanaotoka Kigoma! Angalia mfano wa 1.4 Bil toka kwa wana kagera!

2. Sasa utamlaumu nani??? wakti viongozi wamekimbia Kigoma na kujenga Mz na Dar?

3. Jawabu kudumu ni kujenga daraja Malagarasi- na barabara lami na kuwa na usafiri wa uhakika wa barabara- haya ndo mambo ya kutetea kwa nguvu na Wanakigoma kuondoa shilingi ktk budgeti! Ahadi tu za serikali kila siku over daraja na barabara- sasa 46 years! Hamna kitu!

Sasa kama Kigoma wanachagua wabunge wanaotetea mambo ya Kitaifa kama Bugwazi na Zitto kwa nini wanashindwa kutetea infrustructure ya Kigoma?
 
Ibrah unataka kunitoa machoni.
Pamoja na serikali kuwa wabaguzi wakubwa sana na kuutenga mkoa wa kigoma makusudi lakini kinachochangia matatizo hayo kikubwa ni ukosefu wa wabunge makini.

Kigoma haijapata kuwa na MBUNGE Makini anayewatetea hata siku moja. Hukumbuki miezi kama miwili iliyopita tu iliwalazimu FFU kuingia kuwatoa wasalifiri waliokuwa wamekaliana vichwani.
Kwa kifupi ule sio usafiri.

Harafu angali wabunge wa kigoma siku ile ya ZITO walivyoshambuliana bungeni. Selukamba&Msambya dhidi ya ZITO.

Utafikiri ndicho kilicjhowapeleka bungeni.

Ni aibu sana ndugu zanguni,

Naomba Jambo forum itusaidie kutuokoa watu wa KIGOMA twafa.


Sasa hii bwana inabidi iwe next agenda ya Zitto, tena aibebee mbeleko haraka sana. Hali hii inatisha, yaani nikisoma maandishi yenu ni kama nawaona hao wapiga kura wa CCM wakiwa pale stesheni Dar kuelekea Kigoma-ni balaa kubwa.
 
huu ni uhuni na kwenda kinyume na katiba ya jamhuri ya muungano kuutangaza mkoa wa kigoma kuwa jamhuri.

kabla ya yote alieleta mada hii na kuipa jina hilo amekusudia fitna na shari na sio kuwasilisha matatizo ya wanakigoma au kutafuta suluhisho la kweli.

mtu huyu ashindwe na alegee
 
Kama mkiona namna gani vipi mnaweza kujiunga na Jamhuri ya Burundi isiwe taabu ishakuwa nongwa sasa mbona watu wa Mtwara miaka nenda miaka rudi wanasota na barabara mbaya tena Mtwara hata ukitupisha jiwe kutoka Dar kwa mkono linafika au jogoo akiwika Dar Mtwara anasikika...

Anyway msikwazike na maneno haya si ndio majibu tunayowapa Wazanzibari wakilalamika?
 
Ibrah unataka kunitoa machoni.
Pamoja na serikali kuwa wabaguzi wakubwa sana na kuutenga mkoa wa kigoma makusudi lakini kinachochangia matatizo hayo kikubwa ni ukosefu wa wabunge makini.

Kigoma haijapata kuwa na MBUNGE Makini anayewatetea hata siku moja. Hukumbuki miezi kama miwili iliyopita tu iliwalazimu FFU kuingia kuwatoa wasalifiri waliokuwa wamekaliana vichwani.
Kwa kifupi ule sio usafiri.

Harafu angali wabunge wa kigoma siku ile ya ZITO walivyoshambuliana bungeni. Selukamba&Msambya dhidi ya ZITO.

Utafikiri ndicho kilicjhowapeleka bungeni.

Ni aibu sana ndugu zanguni,

Naomba Jambo forum itusaidie kutuokoa watu wa KIGOMA twafa.

Hivi sheria ya Tanzania inasema kuwa lazima Mbunge wa sehemu fulani apige kelele Bungeni ndio barabara ijengwe? Umuhimu wa mkoa wa Kigoma (mkoa wa mpakani) haujulikani kwa serikali mpaka mbunge wa Kigoma aseme? miaka yote hii toka uhuru hakuna mtu serikalini anajua hili?

Hii ni aibu kwa serikali kuu?
 
1. Viongozi toka Kigoma pia wamewaangusha wana Kigoma- kusema kweli sijawahi ona msukumo wa kweli toka kwa viongozi wanaotoka Kigoma! Angalia mfano wa 1.4 Bil toka kwa wana kagera!

2. Sasa utamlaumu nani??? wakti viongozi wamekimbia Kigoma na kujenga Mz na Dar?

3. Jawabu kudumu ni kujenga daraja Malagarasi- na barabara lami na kuwa na usafiri wa uhakika wa barabara- haya ndo mambo ya kutetea kwa nguvu na Wanakigoma kuondoa shilingi ktk budgeti! Ahadi tu za serikali kila siku over daraja na barabara- sasa 46 years! Hamna kitu!

Sasa kama Kigoma wanachagua wabunge wanaotetea mambo ya Kitaifa kama Bugwazi na Zitto kwa nini wanashindwa kutetea infrustructure ya Kigoma?

Mkuu Mzalendo,

Ni jukumu la serikali kujenga miundombinu kutokana na pesa ya kodi inayotozwa kwa wananchi. Sidhani kama ni vyema wananchi kuchangishana kujenga barabara wakati huo huo wakilipa kodi!

Kinaumiza kusikia kuwa wizi wa benki kuu ni zaidi ya billioni mia moja (kwa figure za Kikwete) na zaidi ya tilioni moja (kwa report ya Slaa) na wachache wanafaidika huku miundombinu ya nchi ikidumaa!

Aibu kabisa kwa serikali kuu (to be specific serikali ya ccm) na viongozi wake!
 
Asante sana Morani; hawa Wahindi wa TRL ndiyo wanaoendesha zile treni ambazo watu wanakaa hadi juu ya behewa. Duniani kote hakuna mahali penye usafiri duni wa Treni kama kule India.

Nakumbuka kuona picha ya namna hiyo kwenye magazeti yetu kama kuna mtu anazo atubandikie hapa.
Mkuu,
Tanzania ina matatizo mengi, na karibia kila sehemu inamatatizo yake,kuna mikoa kama Rukwa ambao wako kimya.

Usafiri wa treni wa india huwezi kulinganisha na nchi zetu za kajambanani, india iko advanced katika usafiri wa terni, na wana grades za treni pia., na wananjia nyingi, siyo kama sisi, treni moja kwa wakati mmoja! Si sahihi kwa ulivyosema kuhusu India.

Wakati Rais anafunga miaka 2 ya utawala kuna mwandishi alimwuliza kuhusu usafiri wa Reli , TRL an uwekezaji Muungwana akadai kuwa wakati wa TRC treni ilichukua hadi siku 8 kwenda Kigoma! Nilimshangaaa, maana haijawahi kutokea katika TRC Wasafiri kukaa siku 5 njiani ati kwa kuwa mabehewa ya mizigo yametokea never, Rais aliwadanganya WaTz! !

Mimi natoka sehemu ambayo miaka nenda miaka rudi, TRC alikuwa partner wangu mkuu katika mambo ya usafiri, tangia enzi zile tunalala chini ya uvungu wa viti! Wakati ule watu walikuwa wanakaliana vichwani na miguuni, ilikuwa inajaza kama vile mabasi ya kwenda mwanza kupitia njia ya kati yanavyojaza! Na ilikuwa inawezekana kukaaa siku kadhaa porini, mvua ikinyesha 'godegode, kidete', treni ya mizigo ikianguka n.k taratibu TRC ikaongeza 'customer care' kwa kuwa inawaleta abiria wake kwa mabasi pindi hali inapokuwa tete.

TRL imeanza kazi, ni budi wadau tupige kelele pale ambako tunaona wanataka kuturudisha miaka ile tulivyokuwa tunasafiri kama mizigo! ni budi tupige kelele kuona haki za wasafir zinalindwa ikiwemo compensation pindi treni inapochelewa kufika kama ilivyokusudiwa!

Kitu ambacho TRC walikuwa wakifanya ni kubadilisha Wasafiri kuhamia treni nyingine (kubadlishana) na ilikuwa sahihi kabis. Sijui Muungwana alipandaga Treni ya TRC lini

Ilikuwa pia inategemea na chanzo cha tatizo! Kama kipindi cha masika, hali ya treni moja kukwama 'Morogoro', nyingine 'Godegode; na nyingine 'Dodoma', ilikuwa jambo la kawaida, hapo huwezi kubadilishana! ni lazima moja ya gode gode iondoke kwanza ifike morogoro, na ya morogoro ifike dodoma ndipo ya dodoma iondoke! piga mahesabu hapo ni siku ngapi njiani! na kufika mapema kwa treni iliyokwama godegode ni majaaliwa ya hali ya mvua ikoje, na ikilzamika kuondoka bila kuangalia miundombinu ikoje, ndio matatizo kama ile ajali ya KIDETE ilivyotokea.
 
Mikoa hii (Kigoma, Tanga, Mtwara, Lindi na Rukwa) inadharauliwa kama siyo vile siyo sehemu ya Tanzania, pamoja na kuwa nyuma sana kimaendeleo lakini mgawo wa bajeti ya maendeleo unaotolewa katika mikoa hii ni mdogo sana ukilinganisha na mikoa mingi ambayo hali yao ina ahueni. Labda waombe kujitenga na kuwa sehemu ya nchi jirani ndio vilio vya mikoa hii vitasikilizwa, vinginevyo itabaki kuwa nyuma kimaendeleo milele.
 
Mikoa hii ( Tanga) inadharauliwa .

Tanga hawana tatizo la barabara wala hawajatengwa- umefika Tanga mjini barabara zote leo zina lami- je utalinganisha na Kigoma? Kama Tanga wako nyuma ni sababu zaidi za watu wa huko-- angalia hadi leo hii hawana Chuo Kikuu hata kimoja yetu miundombinu iko ok na wanakusanya pesa nyingi TRA!

Be fair Bubu kwa Tanga!
 
Naijua Tanga vizuri sana. Tanga ya miaka 60 na 70 siyo Tanga ya leo imerudi nyuma sana kimaendeleo maana wakuu wameamua kuitelekeza.
 
Naamini, Tunaweza kuomba mambo mengi mazuri yafanywe na wanasiasa wakatoa kila ahadi; lakini kama rasilimali zetu hazitumiki vema tutaishia kuongeza madeni ya nje kwa TZ. Kwanza usafi ufanywe ndani ya Kaya yetu, kama vile walau tumeona na bado hatujaridhika tu na ufagiaji alioujaribu(ingawa mdigo), then tubaki na wachache (hata mawaziri) wanaosimamia maslahi ya wananchi(sio matumbo yao kama ilivyodhihirika pale DOM kwa WNM/and CCM MP's) dhidi ya Kabwe; hilo likiisha, rasilimali zikazalisha kadri inavyopaswa kuwa; tukaweka malengo endelevu (yakiwa na Katiba isiyo mawaa) then sasa Dai huo mkoa unaoutaja au eneo unalolitaja; bila hivyo; tutapiga hatua kurudi nyuma tu.
 
hii hali ni mbaya sana na haikubaliki, bandari ya kigoma inaingiza pesa nyingi sana serikalini kutokana na kuwa mpakani, sasa iweje watu wasitengenezewe miundombinu bora, je ni ubaguzi au, na je kwa nini wananchi wa Kigoma waendeelee kuichagua ccm wakati inawapa mateso haya?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom