Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Akizungumza katika mkutano wa Kijiji uliofanyika katika kijiji cha Juhudi Kata ya Kasanda Mwenyekiti wa wanawake hao, Tatu Kiuliko alisema Wanaume wengi katika vijiji hivyo vilivyopo karibu na kambi ya wakimbizi wengi wao wamekuwa wakitelekeza familia zao na kwenda kambini kuoa wakimbizi jambo ambalo limekuwa Kero kwa Wamama hao na kumuomba Mkuu wa Wilaya hiyo kuwasaidia kuwarejesha.
Alisema baadhi ya wanawake wameachwa na watoto zaidi ya nane na nyumba zimeezuliwa na mvua ya upepo ilionyesha mwishoni mwa wiki hii, wanashindwa wafanye nini waweze kuwalea watoto wao, mpaka sasa ambapo ni msimu wa Kilimo wanaume hao wapo kambini wanaishi na wakimbizi wakikwepa majukumu yao.