KIGOMA: Mwanamke anusurika kifo baada ya mume wake kumkata kwa kisu shingoni

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,252
wivu.jpg

Mwanamke mkazi wa Kijiji cha Mahembe, Wilaya ya Kigoma,Bibi SIYAJUI ALMAS, amenusurika kifo baada ya mume wake aitwaye, MAGURU SHABANI, kumkata kwa kisu shingoni kwania ya kumuua kutokana na wivu wa mapenzi.

Akieleza hali ilivyokuwa, majeruhi SIYAJUI ALMAS ambaye amelazwa katika Kituo cha Afya Bitale Wilayani Kigoma, amesema mumewe amechukua uamuzi huo baada ya kutokea kutoelewana baina yao kutokana na shutuma za usaliti wa mapenzi.

Amesema mumuwe alikimbia baada ya kuhisi kuwa amekufa na kwamba kutokana na kupiga kelele majirani na wifi yake walifika kumsaidia.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Bitale, Bwana NORBERT NSHEMETSE amesema majeruhi ambaye amepokelewa akiwa amepoteza damu nyingi anaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu.

Polisi inaendelea kumsaka mume wa majeruhi ambaye ametoroka baada ya tukio.

Chanzo: ITV


My take: Michepuko siyo dili, tutakuja kutoana roho bure!
 
Si angeacha naye tu. Ya nini kutaka kumuua, wanawake wote hawa!
 
Aiseee wanaume ni nn kimewapata mbona haya mambo yanashamiri sana jmn
 
Huu sasa ujinga unazidi..... Wanaume embu grow up some balls...

K zote hizi mtaani..utoe mtu uhai!!??
 
Back
Top Bottom