Kigoma: Majambazi matano yameuwa yakijibizana na polisi.

Siwamini polisi wa Tanzania.
Siwapendi polisi wa Tanzania
Nikisikia mtu amfyatua mjegeje na polisi wamechapika nafurahi sana.
P.I.P HAMZA asante kwa kidogo ulichofanya.
Vipi, kambi yenu ya Msumbiji naona haikaliki wauajii wakubwa nyie, mnaua hata watu wetu mpakani
 
Si tulishakubaliana police CCM wanalinda viroboto, wahuni na matapeli?

Basi waungulie jahanamu polisi wote waliotokomea na kina Ben, Lijenje, Azory, Malema na wenzao kusikojulikana.

Wasibakizwe pia waliopanga, kudhamiria, na kutekeleza shambulio la Lissu.

Yawafike makubwa waliowauwa wafanya biashara wa madini wa Ifakara.

Wasibakizwe waliosokomeza watu kwenye viroba.

Eeh mola wetu usimnusuru na adhabu yako awaye yote kwa dhuluma zao dhidi ya waja wako kwa sababu tu wao ni polisi.
Ukiniwekea ushahidi kuwa polisi wanahusika 100% kwenye matukio pamoja na kupotea baadhi ya watu uliowataja,, nakuahidi tunafungua kesi wiki ijayo Mkuu na tunashinda nasubiri ushahidi haki ipatikane
 
Ukiniwekea ushahidi kuwa polisi wanahusika 100% kwenye matukio pamoja na kupotea baadhi ya watu uliowataja,, nakuahidi tunafungua kesi wiki ijayo Mkuu na tunashinda nasubiri ushahidi haki ipatikane

Watu hawa wametoweka. Pana tunaowalipa ili kuhakikisha usalama wa watu na mali zao. Yanakuingia akilini haya?

1. Moses Lijenje kwa mara ya mwisho alichukuliwa na kina kingai:

(a) Mohammed Ling'wenya alitaarifiwa hivyo na Goodluck wakiwa pamoja na Mahita.
(b) Komando Mhina anathibitisha kutumika kwa askari wengi kwenye ukamatwaji wao. Lijenje asingeweza kutoweka.

2. CCTV za tukio la Lissu ziko mikononi mwa polisi:

IMG_20211210_091620_397.jpg


3. Wafanya biashara wa madini wa Ifakara waliuwawa mikononi mwa polisi.

4. Luteni Urio na Komando Malema, walionekana mara ya mwisho wakiwa mikononi mwa polisi.

5. Azory alichukuliwa na watu waliokuwa wamevalia uniform za kipolisi.

6. Ben simu yake iliendelea kuwapo hewani pamoja na kutoweka kwake bila polisi kuchukua hatua zozote.

Kwani, kuhakikisha kupatikana kwa haki kwa watu hawa ni jambo la hisani?
 
Watu hawa wametoweka. Pana tunaowalipa ili kuhakikisha usalama wa watu na mali zao. Yanakuingia akilini haya?

1. Moses Lijenje kwa mara ya mwisho alichukuliwa na kina kingai:

(a) Mohammed Ling'wenya alitaarifiwa hivyo na Goodluck wakiwa pamoja na Mahita.
(b) Komando Mhina anathibitisha kutumika kwa askari wengi kwenye ukamatwaji wao. Lijenje asingeweza kutoweka.

2. CCTV za tukio la Lissu ziko mikononi mwa polisi:

View attachment 2052646

3. Wafanya biashara wa madini wa Ifakara waliuwawa mikononi mwa polisi.

4. Luteni Urio na Komando Malema, walionekana mara ya mwisho wakiwa mikononi mwa polisi.

5. Azory alichukuliwa na watu waliokuwa wamevalia uniform za kipolisi.

6. Ben simu yake iliendelea kuwapo hewani pamoja na kutoweka kwake bila polisi kuchukua hatua zozote.

Kwani, kuhakikisha kupatikana kwa haki kwa watu hawa ni jambo la hisani?
Nani kasema hisani,,,
Weka ushahidi unaweka maneno mengi yasiyothibitika Mkuu upo serious umesema Apo kuna cctv zilichukua tukio la lissu ziweke hapa na tuone kama polisi nd walimtia risasi mh lissu
 
Nani kasema hisani,,,
Weka ushahidi unaweka maneno mengi yasiyothibitika Mkuu upo serious umesema Apo kuna cctv zilichukua tukio la lissu ziweke hapa na tuone kama polisi nd walimtia risasi mh lissu

Kwamba:

1. Wanaothibitisha Lijenje kuchukuliwa na polisi wapo.
2. Wanaothibitisha kuwa na CCTV za tukio la Lissu wapo.
3. Wanaothibitisha wafanya biashara wa Ifakara kufia mikononi mwa polisi wapo.
4. Wanaothibitisha kuwaona makomando Urio na Malema mara ya mwisho mikononi mwa polisi wapo.
5. Wanaothibitisha Azory kuonekana mara ya mwisho mikononi mwa polisi wapo.
6. Walioshuhudia ndivyo sivyo za polisi zenye kutia shaka kwenye kutoweka kwa Ben wapo.

Bado unataka nini kama kuhakikisha usalama wa watanzania hawa si jambo la hisani?

Acheni usanii.

Nani asiyejua kuwa polisi mnabambika kesi na hata kuwadhulumu watu maisha yao?

Nani ambaye hajaonja shubiri za dhuluma zenu?

Usisahau hata Mama Samia ni mhanga wenu pia.
 
Magaidi yanapojiita polisi.

Wapumzike kwa amani wahanga wote:

1. Wapumzike kwa amani wafanya biashara wa madini wa Ifakara.
2. Wapumzike kwa amani waliopotelea mikononi mwa polisi
3. Apumzike kwa amani Hamza Mrefu.
4. Wapumzike kwa amani wote walioporwa roho zao kwenye dhuluma lukuki za namna hii.
mkuu umewasahau na polisi wenyewe pia wapo waliodedi wkfanya hayo mmbo
 
Siku watakapofika majambazi majumbani kwenu mtajua tu umuhimu wa polisi na ubaya wa majambazi,,
Asee jambazi ni mtu mbaya sana usipomuua ni lazma akuue wewe tuliopitia hizo zahma tunaelewa mapambano na ubaya wa hao watu,,
#Go on our heroes
#Go on police ua hao majambazi ni watu wabaya sana ukiingia kwenye 18 zao.
dah polisi mwenyewe.Hongera afande kwa kutulinda
 
dawa ya majambazi ni moto tu hapana kuwachelewesha.
safi sana Jeshi la Poisi Kigoma.
 
Halafu unakuta hakuna polisi hata mmoja aliyepunyuliwa na risasi

Mbona HAMZA mmoja tu aliwatoa jasho tena akiwa Hajilindi wao wamevaa bullet proofs na wamejificha??

Hapo ukute washapora mali na kuwaua na wala sio majambazi
 
Vp mlitaka polisi wawaachie hao majambazi

Hivi nyie kigoma mnaijua kiundani huko kuna uhalifu wa hatari ngoja siku ikukute ndiyo utakuja kujua

Ova
 
Kuna watu wakickia majambazi wameuawa wanakereka,,,,wakifanya uhalifu na kuuwa askari na raia wanamsakama na kumlaumu mama. Hii nchi cjui nani aliwaloga. Acha wauawe
Kwa mambo yalipofikia sasa ni muhimu ujiridhishe kama kweli waliouawa ni wahalifu. Usishangae wakijitokeza ndugu wakidai ndugu zao wameporwa mali na kuuawa na polisi.
 
Back
Top Bottom