Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,813
- 4,547
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma amesema boti inayobeba abira katika Ziwa Tanganyika ya MV Nzeimana inayofanya safari zake kati ya Sibweso na Ikola mkoani Katavi imezama
Amesema inasemekana majira ya leo saa kumi na moja na nusu ilianza safari kutoka Sibweso ila ilipofika eneo linaitwa Rasini ilipigwa na dhoruba kali na kupinduka
Kamanda huyo, Martin Ottieno ambaye ameeleza kuwa naelekea eneo la tukio, amesema kuwa inasemekana boti hiyo ilikuwa na watu wapatao 60
Amesema miili ya watu tisa waliofariki imeshaopolewa kwenye maji na kati yao Wanawake ni 7 na Wanaume ni 2 na watu 51 wameokolewa wakiwa hai. Amesema akifikia atatoa taarifa kamili
Amesema inasemekana majira ya leo saa kumi na moja na nusu ilianza safari kutoka Sibweso ila ilipofika eneo linaitwa Rasini ilipigwa na dhoruba kali na kupinduka
Kamanda huyo, Martin Ottieno ambaye ameeleza kuwa naelekea eneo la tukio, amesema kuwa inasemekana boti hiyo ilikuwa na watu wapatao 60
Amesema miili ya watu tisa waliofariki imeshaopolewa kwenye maji na kati yao Wanawake ni 7 na Wanaume ni 2 na watu 51 wameokolewa wakiwa hai. Amesema akifikia atatoa taarifa kamili