Kigoma: Aliyekuwa Mbunge wa Mhambwe(NCCR Mageuzi), Mkosamali ajivua uanachama. Asema chama kimemezwa na CHADEMA

Status
Not open for further replies.

Trump2

JF-Expert Member
May 28, 2017
1,553
2,608
ANGALIZO: Habari hii imekanushwa - News Alert: - Felix Mkosamali: Sina mpango wa kuhama chama cha NCCR Mageuzi

mkosamali.jpg
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Muhambwe Mkoani Kigoma kupitia chama Cha NCCR-Mageuzi Felix Francis Mkosamali ametangaza kujivua uanachama wa chama hicho kwa kile alichoeleza kuwa chama hicho kimemezwa na Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) hivyo kupoteza dira.

Pia Mkosamali ameongeza kuwa vyama vya upinzani vimepoteza dira baada ya kukumbatia waliokuwa mafisadi wanaohamia kwenye vyama hivyo kutoka CCM.

Sababu nyingine aliyoitoa ndugu Mkosamali ni kuwa anamuunga mkono Rais Magufuli kwenye vita dhidi ya ufisadi na kupigania na kulinda rasilimali za taifa.

Aidha Mkosamali amesema siku kadhaa zijazo atatangaza atakachojiunga nacho.
 
Yule mleta ana matatizo ya akili ameandika mbunge kumbe alikuwa mbunge akashindwa kutetea nafasi yake mbwembwe za nini? huyu atakuwa ameshahongwa pesa anahamia CCM mbona muda wote alikuwa huko NCCR hakujiondoa njaa haiwajahi kuwaacha salama wenye njaa.
 
Sasa chama chake ameshindwa kukiokoa kisimezwe halafu bado anajiita ni mwanasiasa!?

Tena, bado anasema vyama vimepoteza uelekeo wa kisiasa.

Tangia November 2015 iweje leo 2017 ndiyo aje kuona juhudi za Rais!? Wakati speed ya Rais haijawahi kubadilika tangia aingie madarakani!?

Anaenda wapi sasa, au CCM ambako yeye mwenyewe anakili kuwa waliotoka huko na kujiunga upinzani ni mafisadi na ndiyo wanaua upinzani !?

Maana ,kwa kifupi yeye binafsi hana vision kabisa ya kuponya chama chake hata huko aendako si ataua tu chama atakachojiunga na mwisho kikifa nacho atamlaumu nani!?

Kweli Tanzania tuna wana sesere kwenye siasa badala ya wanasiasa.
 
[HASHTAG]#DARMPYABLOGUPDATES[/HASHTAG]

Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma kupitia chama Cha NCCR Mageuzi Felix Fransic Mkosamali ametangaza kujivua uwanachama wa chama hicho kwa kile alichoeleza kuwa chama hicho kimemezwa na Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) hivyo kupoteza dira,pia Mkosamali ameongeza kuwa vyama vya upinzani vimepoteza dira baada ya kukumbatia waliokuwa mafisadi wanaohamia kwenye vyama hivyo kutoka CCM .Sababu nyingine aliyoitoa ndugu Mkosamali ni kuwa anamuunga mkono Rais Magufuli kwenye vita dhidi ya ufisadi na kupigania na kulinda rasilimali za taifa.Aidha Mkosamali amesema siku kadhaa zijazo atatangaza atakachojiunga nacho


Kigoma ni karibu sana na Burundi..nilishangaa amechelewa sana.
 
Ukawa unapukitika... Waendelee na hoja dhaifu kuwa wananunuliwa... Kuna hela gn ya kuchezea kiasi hicho tena serikali ya kubana matumizi.. Kuwakumbatia mafisadi kama mamvi na mr zero inahitaji moyo wa chuma

Zitto amemtaka CAG akague 300b zilipolekwa kwenye ujenzi wa uwanja wa Chato. Tulia tu utajua pesa za kununua wapinzani zinatoka kwenye fungu gani.
 
... Kuna hela gn ya kuchezea kiasi hicho tena serikali ya kubana matumizi.. Kuwakumbatia mafisadi kama mamvi na mr zero inahitaji moyo wa chuma
Kama ccm wanatumia polisi na tume kushinda chaguzi kama inavyodaiwa, kwanini waharibu pesa yao kununua watu?!
 
Zitto amemtaka CAG akague 300b zilipolekwa kwenye ujenzi wa uwanja wa Chato. Tulia tu utajua pesa za kununua wapinzani zinatoka kwenye fungu gani.
Zitto Mwenyewe kwa taarifa zilizopo ameshafika bei
 
Wanasiasa Uchwara ni watu wa ajabu sana.
Wewe Mkosamali wewe ni Mtu wa kusaliti wapiga kura wako.
Kwa sababu za kipuuzi kama hizi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom