KIGOGO WA CELTEL anaswa na TAKUKURU

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Kigogo CELTEL anaswa na TAKUKURU


Na Mwandishi Wetu

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imemkamata Ofisa Usalama wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Celtel (T) Limited, Bw. Mohamed Gulamali, kwa kushawishi na kupokea rushwa ya sh. milioni tatu.

Taarifa iliyotolewa jana na Ofisi ya Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni, ilisema tukio hilo lilitokea Julai 8 mwaka huu saa 10 jioni katika maeneo ya ofisi za Celtel, Kijitonyama, Kinondoni, Dar es Salaam.

Ilisema Juni 30 mwaka huu, taasisi hiyo ilipokea taarifa ya kushawishi hongo kutoka kwa mlalamikaji ambaye jina lake linahifadhiwa, ikidai kuwa mtuhumiwa alitaka mtoa taarifa amwongeze mkataba wa kulinda minara ambao ulikwisha muda wake siku hiyo.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, iwapo mkataba huo ungepitishwa basi ingebidi alipwe kila mwezi sh. milioni 4.5, ili malipo yao yawe yanaharakishwa kila mwezi.

Taarifa ilisema baada ya kupata taarifa hiyo, uchunguzi wa awali ulianza kwa nia ya kuthibitisha tuhuma hiyo na Julai 2 mwaka huu, mazungumzo yalifanyika baina ya mtoa taarifa na mtuhumiwa, Bw. Gulamali.

"Bw. Gulamali alisisitiza nia yake, kuwa bila kutimizwa kwa malipo hayo, mkataba hautasainiwa kwani kampuni zingine zinawania kazi hiyo. Aidha iwapo hongo itapokewa, atakuwa anaharakisha malipo yao kila mwezi," ilisema taarifa.

Iliongeza kuwa siku ya tukio, saa 8.30 mchana, mtoa taarifa alipokea ujumbe ukimtaka apeleke fedha, vinginevyo hatua za awali za mkataba hazitapitishwa na hivyo mkataba huo kufutwa.

"Mtoa taarifa alifika ofisini na uchunguzi uliamua kuweka mtego, ambapo mtuhumiwa alikamatwa saa 10 jioni akipokea hongo ya sh. milioni tatu katika ofisi za Celtel, Kijitonyama.

"Utambuzi wa fedha ulifanyika na mashahidi walioshuhudia walizitambua noti na baadaye mtuhumiwa aliletwa ofisini kwa mahojiano ili kukamilisha uchunguzi," ilisema taarifa na kuongeza kuwa baada ya uchunguzi, hatua zingine za kisheria zitafuata.
 
Kigogo CELTEL anaswa na TAKUKURU


Na Mwandishi Wetu

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imemkamata Ofisa Usalama wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Celtel (T) Limited, Bw. Mohamed Gulamali, kwa kushawishi na kupokea rushwa ya sh. milioni tatu.

Taarifa iliyotolewa jana na Ofisi ya Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni, ilisema tukio hilo lilitokea Julai 8 mwaka huu saa 10 jioni katika maeneo ya ofisi za Celtel, Kijitonyama, Kinondoni, Dar es Salaam.

Ilisema Juni 30 mwaka huu, taasisi hiyo ilipokea taarifa ya kushawishi hongo kutoka kwa mlalamikaji ambaye jina lake linahifadhiwa, ikidai kuwa mtuhumiwa alitaka mtoa taarifa amwongeze mkataba wa kulinda minara ambao ulikwisha muda wake siku hiyo.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, iwapo mkataba huo ungepitishwa basi ingebidi alipwe kila mwezi sh. milioni 4.5, ili malipo yao yawe yanaharakishwa kila mwezi.

Taarifa ilisema baada ya kupata taarifa hiyo, uchunguzi wa awali ulianza kwa nia ya kuthibitisha tuhuma hiyo na Julai 2 mwaka huu, mazungumzo yalifanyika baina ya mtoa taarifa na mtuhumiwa, Bw. Gulamali.

"Bw. Gulamali alisisitiza nia yake, kuwa bila kutimizwa kwa malipo hayo, mkataba hautasainiwa kwani kampuni zingine zinawania kazi hiyo. Aidha iwapo hongo itapokewa, atakuwa anaharakisha malipo yao kila mwezi," ilisema taarifa.

Iliongeza kuwa siku ya tukio, saa 8.30 mchana, mtoa taarifa alipokea ujumbe ukimtaka apeleke fedha, vinginevyo hatua za awali za mkataba hazitapitishwa na hivyo mkataba huo kufutwa.

"Mtoa taarifa alifika ofisini na uchunguzi uliamua kuweka mtego, ambapo mtuhumiwa alikamatwa saa 10 jioni akipokea hongo ya sh. milioni tatu katika ofisi za Celtel, Kijitonyama.

"Utambuzi wa fedha ulifanyika na mashahidi walioshuhudia walizitambua noti na baadaye mtuhumiwa aliletwa ofisini kwa mahojiano ili kukamilisha uchunguzi," ilisema taarifa na kuongeza kuwa baada ya uchunguzi, hatua zingine za kisheria zitafuata.


Hii ni preliminary.Tusubiri kuona kama kesi itafika popote
 
Hawa takukuru mbona hawajakamata watu wa richmond na Dowans waliokuwa wakikinga pesa kwa kutumia makampuni ya mfukoni?

Au kuna takukuru ni kwa ajiri ya rushwa ndogo za traffic, waiba miwa, nk?

anyway kazi nzuri.
 
Tunataka na hizo nyingine za mikataba minono ya mafisadi wa nchi hii. Rushwa ni rushwa na hiyo TAKUKURU kazi yao ni kukamata na sio kutangaza. Mimi hainiingii akilini kwanza hao jamaa hawafanyi kazi yao sawasawa na ndio maana wakikamata kidogo tu wanatangaza kwenye vyombo vya habari. Anyway wamejitahidi kidogo lakini safari bado ni ndefu kwa hawa jamaa wa TAKUKURU.
 
AKUKURU wanachukua uzoefu jamani, walianza na rushwa ya Tsh elfu moja, ikaja elfu 3, 5, 10, 30, 50, laki na sasa milioni 3. Wanagain momentum kuendea kwenye rushwa za vijisenti!!!
 
ashakwisa kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Nzige wanatafunana wenyewe kwa wenyewe takukuru wanakula rushwa huku wanakamata wala rushwa. hivi huyu hosea anaondoka lini tunataka mtu anayeweza kusgughulikia mafisadi.
 
........ whoooooooopsss ! Bado vijidagaa vyaendelea kukamatwa !! SAMAKI wakubwa wao lini maana wanajulikana ?????????
 
hao TAKUKURU ni wanafiki wakubwa.
kwenye viishu vidogo vidogo ndo wanajitia wana meno ya kung'ata na kutafuna...mbona kwenye ishu ya richmond walisema kuwa hakuna harufu yoyote ya rushwa mpaka kamanda dr halison ford ooops sorry dr halison george mwakyembe na timu ya mashujaa walipofumua shuzi na kuwaweka wezi hadharani?
 
wamezoea vya kunyonga hawa mbona wasichinje basi? Kama wana ubavu wawakamate wahalifu ambao nchi nzima inawajua ila wao wamewafumbia macho
 
Back
Top Bottom