Jumanne Mkota
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 2,917
- 1,660
Taasisi ya Kupambana na kuthibiti Rushwa Nchini TAKUKURU imemkamata aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Ndugu Mamboleo Tery na Aliyekuwa Afisa Elimu wilaya ya Mwanga Mama Phoibe Lyatuu kwa tuhuma za kuisababishia serikali hasara ya Tsh 20,000,000/=.
Mafisadi wote wawili hao walipata dhamana na kukwepa kwenda Kiruru baada ya kila mmoja kudhaminiwa kwa hati ya nyumba yenye thamani ya Tsh 45,000,000.
Baada ya kupata dhamana Mwenyekiti huyo alitamba kuwa hawezi kuwa mbuzi wa kafara kwani Prof. Maghembe ndie kinara wa wanaoimaliza Wilaya ya Mwanga kwa Ufisadi. Alifanya hayo alituhumiwa nayo ili kuhakikisha Mbunge anapata ubunge. Amewaomba PCCB wamkamate pia Mh. Mbunge kwani ndie mhusika mkuu.
My Take
Hao waliokamatwa nadhani ni vidagaa tu kwani kuna mlolongo mrefu na fedha zilizoibwa Mwanga sio hizo tu. Mwanga haina tofauti kabisa na H/Mashauri ya Kishapu.
Mafisadi wote wawili hao walipata dhamana na kukwepa kwenda Kiruru baada ya kila mmoja kudhaminiwa kwa hati ya nyumba yenye thamani ya Tsh 45,000,000.
Baada ya kupata dhamana Mwenyekiti huyo alitamba kuwa hawezi kuwa mbuzi wa kafara kwani Prof. Maghembe ndie kinara wa wanaoimaliza Wilaya ya Mwanga kwa Ufisadi. Alifanya hayo alituhumiwa nayo ili kuhakikisha Mbunge anapata ubunge. Amewaomba PCCB wamkamate pia Mh. Mbunge kwani ndie mhusika mkuu.
My Take
Hao waliokamatwa nadhani ni vidagaa tu kwani kuna mlolongo mrefu na fedha zilizoibwa Mwanga sio hizo tu. Mwanga haina tofauti kabisa na H/Mashauri ya Kishapu.