Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,191
- 676
Kigogo wa CCM ajiua
2008-02-25 17:08:55
Na Kiyao Hoza, Polisi Kati
Kiongozi mmoja wa Umoja wa Vijana wa CCM Jijini ameacha msiba mzito kwa wapendwa wake baada ya kujinyonga kwa shuka la kujifunikia hadi kujiua.
Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Kinondoni, Pius Sheka amesema tukio hilo limetokea jana, mishale ya saa 1:30 usiku huko Mwananyamala Kisiwani.
Kamanda Sheka amemtaja kiongozi huyo wa Vijana CCM, ambaye ni Katibu wa Kata ya Mwananyamala kuwa ni Bw. Cyprian Likonoka, 35.
Amesema Bw. Likonoka alijinyonga kwa kutumia shuka alilolitundika katika kenchi, chumbani kwa mdogo wake aliyetajwa kwa jina la Albino Likokola, 25.
Amesema chanzo cha Bw. Likonoka kujinyonga hakijafahamika na polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Akasema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mwananyamala.
Katika tukio jingine lililotokea katika barabara ya Bagamoyo eneo la Tegeta, karibu na bar iliyofahamika kwa jina la Zero, mwanaume mmoja aliyekuwa akiendesha pikipiki amekufa baada ya kujibamiza kwenye trela moja lililokuwa mbele yake.
Kaimu Kamanda Sheka amesema tukio hilo limetokea leo mishale ya saa 6:45 usiku, wakati mtu huyo, Thomas Makore, akitokea katika bar hiyo huku akiwa amelewa.
Amesema marehemu alikuwa akiendesha pikipiki yenye namba za usajili T 174 ASX, alilivaa trela lenye namba za usajili T 680 AGH iliyokuwa imeegeshwa pembezoni mwa barabara.
Amesema katika tukio hilo marehemu alijeruhiwa kichwani na kuchubuka usoni, na alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mwananyamala.
Wakati huohuo, dereva wa gari yenye namba za usajili T 385 AFP aina ya Nissan Patrol, George Masanga, 32, amefariki dunia, baada ya gari yake kuacha njia na kupinduka mara tatu.
Kaimu Kamanda Sheka amesema tukio hilo limetokea leo mishale la 8:30 usiku, katika eneo la mataa ya Magomeni.
Amesema marehemu alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Muhimbili, na maiti yake imehifadhiwa katika chumba cha maiti hospitalini hapo.
Katika tukio jingine, binti mmoja mkazi wa Ukonga Mazizini amenusurika kufa, baada ya jaribio lake la kutaka kujitoa uhai kugonga mwamba.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Masindoki Masindoki, amemtaja binti huyo kuwa ni Queen Insi, 23, aliyefanya jaribio hilo jana mishale ya saa 4:30 usiku.
Amesema binti huyo alibwia sumu ya panya kwa madai kuwa alikuwa na uvimbe tumboni ambao ulikuwa ukimsababishia maumivu makali.
Kamanda Masindoki amesema binti huyo amelazwa katika Hospitali ya Amana na hali yake inaendelea vizuri, akiwa chini ya ulinzi wa polisi.
SOURCE: Alasiri
2008-02-25 17:08:55
Na Kiyao Hoza, Polisi Kati
Kiongozi mmoja wa Umoja wa Vijana wa CCM Jijini ameacha msiba mzito kwa wapendwa wake baada ya kujinyonga kwa shuka la kujifunikia hadi kujiua.
Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Kinondoni, Pius Sheka amesema tukio hilo limetokea jana, mishale ya saa 1:30 usiku huko Mwananyamala Kisiwani.
Kamanda Sheka amemtaja kiongozi huyo wa Vijana CCM, ambaye ni Katibu wa Kata ya Mwananyamala kuwa ni Bw. Cyprian Likonoka, 35.
Amesema Bw. Likonoka alijinyonga kwa kutumia shuka alilolitundika katika kenchi, chumbani kwa mdogo wake aliyetajwa kwa jina la Albino Likokola, 25.
Amesema chanzo cha Bw. Likonoka kujinyonga hakijafahamika na polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Akasema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mwananyamala.
Katika tukio jingine lililotokea katika barabara ya Bagamoyo eneo la Tegeta, karibu na bar iliyofahamika kwa jina la Zero, mwanaume mmoja aliyekuwa akiendesha pikipiki amekufa baada ya kujibamiza kwenye trela moja lililokuwa mbele yake.
Kaimu Kamanda Sheka amesema tukio hilo limetokea leo mishale ya saa 6:45 usiku, wakati mtu huyo, Thomas Makore, akitokea katika bar hiyo huku akiwa amelewa.
Amesema marehemu alikuwa akiendesha pikipiki yenye namba za usajili T 174 ASX, alilivaa trela lenye namba za usajili T 680 AGH iliyokuwa imeegeshwa pembezoni mwa barabara.
Amesema katika tukio hilo marehemu alijeruhiwa kichwani na kuchubuka usoni, na alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mwananyamala.
Wakati huohuo, dereva wa gari yenye namba za usajili T 385 AFP aina ya Nissan Patrol, George Masanga, 32, amefariki dunia, baada ya gari yake kuacha njia na kupinduka mara tatu.
Kaimu Kamanda Sheka amesema tukio hilo limetokea leo mishale la 8:30 usiku, katika eneo la mataa ya Magomeni.
Amesema marehemu alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Muhimbili, na maiti yake imehifadhiwa katika chumba cha maiti hospitalini hapo.
Katika tukio jingine, binti mmoja mkazi wa Ukonga Mazizini amenusurika kufa, baada ya jaribio lake la kutaka kujitoa uhai kugonga mwamba.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Masindoki Masindoki, amemtaja binti huyo kuwa ni Queen Insi, 23, aliyefanya jaribio hilo jana mishale ya saa 4:30 usiku.
Amesema binti huyo alibwia sumu ya panya kwa madai kuwa alikuwa na uvimbe tumboni ambao ulikuwa ukimsababishia maumivu makali.
Kamanda Masindoki amesema binti huyo amelazwa katika Hospitali ya Amana na hali yake inaendelea vizuri, akiwa chini ya ulinzi wa polisi.
SOURCE: Alasiri