Kigoda cha mwalimu Nyerere kazi yake nini?

lendila

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
5,806
4,370
Kigoda cha Mwalimu Nyerere ni taasisi inayojitangaza kwa watanzania kuwa imekuwa na kazi ya kuenzi fikra za mwalimu Nyerere.

Je, ni kweli kigoda cha mwalimu Nyerere kinamuenzi kwa vitendo? Au kigoda cha mwalimu Nyerere ni wapigaji kama wapigaji wengine?

Kigoga cha Mwalimu Nyerere kimejipambanua wazi wazi mchana kweupe kuwa kinaenzi fikra za mwalimu nyerere. Swali linakuja je, kigoda hakioni jinsi makongamano yenye migongano na mawazo tofati yanayosuguana yamepigwa marufuku nchini?

Moja ya fikra za mwalimu nyerere ni kuwa na nchi yenye mfumo wa vyama vyingi vya siasa. Je, kigoda cha Mwalimu Nyerere kinachukua hatua gani kwa kuona mfumo wa vyama vyingi vya siasa uko hatarini kuliwa na dola mchana kweupe?

Je, kigoda cha mwalimu Nyerere hakina haja ya katiba bora? Kigoda cha mwalimu Nyerere hakijasoma ripoti ya Jaji Kisanga, Jaji Nyalali, Jaji Warioba na kadhalika?

Kigoda cha mwalimu Nyerere kinamuenzi mwalimu kwa lipi? Kwa fikra? Je, hawasikii watanzania wenye mawazo tofauti wanavyokula matusi mazito kutoka kwa Mkapa?

Naomba kigoda cha mwalimu Nyerere wajitafakari upya na wadumishe kweli fikra za mwalimu Nyerere kwa vitendo ikiwepo fikra ya mwalimu Nyerere ya kuleta mfumo wa vyama vyingi vya kisiasa.

Fikra ya mwalimu ya watu kuwa huru bila kubughudhiwa, kubaguliwa kwa vyama vyao, rangi zao dini zao, makabila yao na kadhalika.

Uhuru wa kutoa na kupokea maoni.

Haya ni maendeleo makubwa kwa mwanadamu kuliko hata majengo barabara,ndege na kadhalika,maendeleo ni watu, maendeleo sio vitu mwalimu Nyerere aliyasema haya mwaka 1972, maendeleo ni pamoja na uhuru wa watu kujieleza, kupingana, kukusanyika na kadhalika.
=======

Kigoda cha Mwalimu Nyerere ni nini? SOMA => Kigoda cha Nyerere na ‘utakatifu’ wake
 
Kigoda cha mwalimu nyerere ni taasisi inayojitangaza kwa watanzania kuwa imekuwa na kazi ya kuenzi fikra za mwalimu nyerere je, ni kweli kigoda cha mwalimu nyerere kinamuenzi mwalimu nyerere kwa vitendo?au kigoda cha mwalimu nyerer ni wapigaji kama wapigaji wengine?
Kigoga cha mwalimu nyerere kimejipambanua wazi wazi mchana kweupe kuwa kinaenzi fikra za mwalimu nyerere,swali linakuja je, kigoda cha mwalimu nyerere hakioni jinsi makongamano yenye migongano na mawazo tofati yanayosuguana yamepigwa marufuku nchini?
Moja ya fikra za mwalimu nyerere ni kuwa na nchi yenye mfumo wa vyama vyingi vya siasa,je kigoda cha mwalimu nyerere kinachukua hatua gani kwa kuona mfumo wa vyama vyingi vya siasa uko hatarini kuliwa na dola mchana kweupe?
Je, kigoda cha mwalimu nyerere hakina haja ya katiba bora?kigoda cha mwalimu nyerere hakijasoma ripoti ya jaji kisanga,jaji nyalali,jaji warioba na kadhalika,kigoda cha mwalimu nyerere kinamuenzi mwalimu nyerere kwa lipi?Kwa fikra ?je hawasikii watanzania wenye mawazo tofauti wanavyokula matusi mazito kutoka kwa mkapa?
Naomba kigoda cha mwalimu nyerere wajitafakari upya,na wadumishe kweli fikra za mwalimu nyerere kwa vitendo ikiwepo fikra ya mwalimu nyerere ya kuleta mfumo wa vyama vyingi vya kisiasa
Fikra ya mwalimu ya watu kuwa huru bila kubuguziwa,kubaguliwa kwa vyama vyao,rangi zao dini zao,makabila yao na kadhalika
Uhuru wa kutoa na kupokea maoni,
Haya ni maendeleo makubwa kwa mwanadamu kuliko hata majengo barabara,ndege na kadhalika,maendeleo ni watu,maendeleo sio vitu mwalimu nyerere aliyasema haya mwaka 1972, maendeleo ni pamoja na uhuru wa watu kujieleza,kupingana,kukusanyika,na kadhalika

Sent from my Fero L100 using JamiiForums mobile app

kukaliwa na wanasiasa
 
KIDOGA CHA MWALIMU NYERERE NI KIKUNDI CHA WANAFIKI NA WACHUMIA TUMBO PLUS WAZANDIKI

Sent from my SM-J120H using JamiiForums mobile app
 
Ngoja wanakigoda waje.
Pia watuelezee na matokeo chanya kwenye jamii ya kigoda tangu kimekuwepo.
Binafsi nyerere naona aliweka legacy ya kudumu muda wote hata Bila kigoda
 
Kwa kweli lazima kigoda cha mwl.nyerere kitekeleze kwa vitendo fikra sahihi za mwalimu nyerer,ikiwa ni pamoja na kupigania viongozi kuheshimu katiba ya nchi

Sent from my Fero L100 using JamiiForums mobile app
 
Swali kigoda cha mwl kinaunga mkono kauli ya mzee mwinyi kuwa mh rais magufuli atawale milele mpaka afe?

Sent from my Fero L100 using JamiiForums mobile app
 
Mm kigoda nachokielewa ni hiki

OvA
 

Attachments

  • 250px-Tabouret_pour_traire.JPG
    250px-Tabouret_pour_traire.JPG
    7.2 KB · Views: 46
Umeshahudhuria vigoda vingapi? Na je ktk hivyo vigoda ulivyohudhuria vinavyojadiliwa vina umuhimu au hakuna umuhimu ? Vinatelezeka au havitelezeki? Anayetakiwa kutekeleza ni Nyagoda ? Udsm? jamii au serikali?
 
Hapa tunafikirisha fikra na hatudumishi fikra- Issa Shivji akiongea ktk kigoda cha Tano.
 
wao kazi yao ni kuandaa makongamano ambayo mengi yake theme ni" azimio la arusha" tu au mambo yanayofanana nayo!!

lakini hawazungumzi kilimo cha kufa na kupona
Hawazungumzii Demokrasia ya vyama vingi
Hawazungumzii umuhimu wa kuheshimu katiba

Yaani wanabaki kumzungumzia mwalimu kama mtu, na si kupigia kelele "kisomi" values zake!
 
Kile Kigoda kimejaa wahenga!

Sent from my HTC Desire 820G PLUS dual sim using JamiiForums mobile app
 
wao kazi yao ni kuandaa makongamano ambayo mengi yake theme ni" azimio la arusha" tu au mambo yanayofanana nayo!!

lakini hawazungumzi kilimo cha kufa na kupona
Hawazungumzii Demokrasia ya vyama vingi
Hawazungumzii umuhimu wa kuheshimu katiba

Yaani wanabaki kumzungumzia mwalimu kama mtu, na si kupigia kelele "kisomi" values zake!
Wenye kigoda cha mwalimu ukiwauliza mambo yanayohusu katiba hawataki kabisa

Sent from my Fero L100 using JamiiForums mobile app
 
Bado wako kimya?

Post sent using JamiiForums mobile app
 
nimegundua wachangiaji wengi sambamba na mtoa mada hajui chochote kuhusu kigoda cha mwalimu nyerere
 
Back
Top Bottom