VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Alisema hivi:https://www.youtube.com/watch?v=4CFDwaH3EPM Halafu, akasema hivi:https://www.youtube.com/watch?v=gU29hxl-e9Y. Unajua kwanini? Ngoja niwaambie. Joseph Msukuma, Mwenyekiti wa CCM Geita na mgombea wa Ubunge hukohuko Geita ni mfanyabiashara.
Baada ya Joseph Msukuma kujiweka mbele kama mtetezi wa Lowassa na hata kuendelea kumsupport Lowassa hata alipobaki CCM, CCM ikautumia mkono wa chuma. Ikambana kwenye biashara zake. Kupitia TRA.Msukuma hakulipa kodi kwa miaka takribani saba. Aliachwa kwakuwa ni wa CCM. Alipoleta za kuleta akabanwa. Mabilioni ya kodi yakamshinda kulipa na kuamua kujisalimisha.
Msukuma si wa kuaminika kama alivyo Sophia Simba na Emmanuel Nchimbi. Sophia Simba 'alisusiwa' msiba wa nduguye na kuogopa. Akajisalimisha. Nchimbi naye akaogopa kupoteza alivyovichuma akiwa CCM. Akafyata mkia. Ni hao pamoja na Adam Kimbisa ndiyo waliojitokeza hadharani kupinga maamuzi ya Kamati Kuu ya CCM. Hawaaminiki. Lakini, hawa wamekuwa wanachama wa CCM kwa woga tu. Mioyoni mwao wameshahama.
Hiyo ndiyo CCM yetu ilikofika. Kuwa na wanachama wa kuwalazimisha!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Baada ya Joseph Msukuma kujiweka mbele kama mtetezi wa Lowassa na hata kuendelea kumsupport Lowassa hata alipobaki CCM, CCM ikautumia mkono wa chuma. Ikambana kwenye biashara zake. Kupitia TRA.Msukuma hakulipa kodi kwa miaka takribani saba. Aliachwa kwakuwa ni wa CCM. Alipoleta za kuleta akabanwa. Mabilioni ya kodi yakamshinda kulipa na kuamua kujisalimisha.
Msukuma si wa kuaminika kama alivyo Sophia Simba na Emmanuel Nchimbi. Sophia Simba 'alisusiwa' msiba wa nduguye na kuogopa. Akajisalimisha. Nchimbi naye akaogopa kupoteza alivyovichuma akiwa CCM. Akafyata mkia. Ni hao pamoja na Adam Kimbisa ndiyo waliojitokeza hadharani kupinga maamuzi ya Kamati Kuu ya CCM. Hawaaminiki. Lakini, hawa wamekuwa wanachama wa CCM kwa woga tu. Mioyoni mwao wameshahama.
Hiyo ndiyo CCM yetu ilikofika. Kuwa na wanachama wa kuwalazimisha!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam