Kigangwalla na wabunge wa wadesign yako someni kauli ya Deo (MB)- No Maslahi ya chama

bemg

JF-Expert Member
Apr 25, 2010
2,799
642
FILIKUNJOMBE ANENA


FILIKUNJOMBE ANENA
Mbunge wa Ludewa (CCM) akizungumza katika mahojiano maalum ya NIPASHE Jumapili jijini Dar es Salaam juzi, Filikunjombe alisema tuhuma zinazowakabili mawaziri husika ni moja ya maeneo yanayoiathiri jamii pana ya Tanzania hivyo hakuna sababu ya kuweka mbele maslahi ya kisiasa.
Alisema kama hoja ya kuwataka mawaziri kujiuzulu ingesimamiwa kidete na wabunge wa upinzani, isingekuwa na nguvu kama ilivyotokea kwa upande wa CCM.
“Hoja hii ingesimamiwa na akina Zitto Kabwe isingekuwa na nguvu kwa maana watu wangesema ni kawaida ya upinzani, lakini wabunge wa CCM tuliposimama na kuzungumza, imeleta matokeo makubwa,” alisema.

Filikunjombe alisema hali ya ustawi wa jamii imedumaa huku baadhi ya viongozi wa serikali wakiwemo mawaziri wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wakijilimbizia mali kinyume cha sheria.
“Tunapokuwa majimboni kama kule kwangu Ludewa, wananchi wanahoji kuhusu ukosefu wa huduma bora za afya, elimu, miundombinu na maji safi na salama,” alisema.
Aliongeza,“ kwa hali ilivyo sasa na hulka hii ya mawaziri wasiokuwa waaminifu kuhujumu rasilimali za nchi, si rahisi kuyafikia maisha bora kwa kila Mtanzania.”



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI





 
Filikunjombe ni mkweli na jasili, tatizo sio maslahi ya chama bali ni nizamu ya uoga waliyonayo wabunge wengi kwa vyama vyao na kujua kwamba wako responsible to both vyama na wananchi hivyo ku balance majukumu yao.
 
FILIKUNJOMBE ANENA


FILIKUNJOMBE ANENA
Mbunge wa Ludewa (CCM) akizungumza katika mahojiano maalum ya NIPASHE Jumapili jijini Dar es Salaam juzi, Filikunjombe alisema tuhuma zinazowakabili mawaziri husika ni moja ya maeneo yanayoiathiri jamii pana ya Tanzania hivyo hakuna sababu ya kuweka mbele maslahi ya kisiasa.
Alisema kama hoja ya kuwataka mawaziri kujiuzulu ingesimamiwa kidete na wabunge wa upinzani, isingekuwa na nguvu kama ilivyotokea kwa upande wa CCM.
"Hoja hii ingesimamiwa na akina Zitto Kabwe isingekuwa na nguvu kwa maana watu wangesema ni kawaida ya upinzani, lakini wabunge wa CCM tuliposimama na kuzungumza, imeleta matokeo makubwa," alisema.

Filikunjombe alisema hali ya ustawi wa jamii imedumaa huku baadhi ya viongozi wa serikali wakiwemo mawaziri wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wakijilimbizia mali kinyume cha sheria.
"Tunapokuwa majimboni kama kule kwangu Ludewa, wananchi wanahoji kuhusu ukosefu wa huduma bora za afya, elimu, miundombinu na maji safi na salama," alisema.
Aliongeza," kwa hali ilivyo sasa na hulka hii ya mawaziri wasiokuwa waaminifu kuhujumu rasilimali za nchi, si rahisi kuyafikia maisha bora kwa kila Mtanzania."



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI





Kigwangallah ni mchumia tumbo, ni mtu wa "hand to mouth politics".
 
Back
Top Bottom