Chief Kabikula
JF-Expert Member
- Jan 1, 2019
- 7,567
- 9,026
Leo askari wa magereza wameua msichana Neema Dominic , mkazi wa Tuamoyo aliyemaliza kidato cha nne mwaka juzi.
Kifo hicho kimetokana na Askari Magereza kumfyatulia risasi mfungwa aliyekuwa ameachiwa na Mahakama wakitaka kumkamata tena ndipo risasi walizomfyatulia zikampata Neema na kumuua papo hapo, nyingine zikimjeruhi mama yake mzazi.
_____
Maoni Yangu:
Hivi haya mauaji ya askari kwa RAIA mpaka lini?
========
Dar es Salaam. Neema Dominick mkazi wa Kigamboni Mtaa wa Tuamoyo jijini Dar es Salaam amefariki dunia baada ya kupigwa risasi katika eneo la paja na askari Magereza.
Baada ya risasi iliyomuua Neema kutokea upande wa pili pia ilimjeruhi mama yake mzazi, Rehema Ibrahimu katika eneo la paja.
Mauti hayo yalimpata Neema jana akiwa nyumbani kwao karibu na Mahakama ya Kigamboni wakati askari wa Magereza alipokuwa akijaribu kumzuia mtuhumiwa asitoroke mahakamani.
Akizungumzia tukio hilo, kaka wa marehemu, Juma Mwinjaku alisema kabla ya tukio hilo mtuhumiwa huyo alitoroka kwa mara ya kwanza askari wakafanikiwa kumdhibiti kabla ya kutoroka tena na kuamua kutumia risasi kumzuia.
“Mara zote alipotoroka alikuwa akitumia upande ambao nyumba yetu ipo jambo ambalo lilifanya hata walipotumia risasi kuwa rahisi kutufikia.”
“Lakini kwa nini watumie risasi kumzuia mtuhumiwa ilhali wanajua eneo lile liko karibu na makazi ya watu pamoja na shule? Kwa nini hawaangalii madhara yanayoweza kutokea kwa watu,” alihoji.
“Binti huyo alimaliza kidato cha nne mwaka juzi kuna wakati alikuwa akitaka kwenda jeshini akakosa nafasi hivyo alikuwa yupo nyumbani tu akisubiri utaratibu mwingine,” alisema
Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa aliyekuwa akizuiwa kwa risasi alikuwa tayari ameachiliwa na Mahakama.
Chanzo: Mwananchi
Kifo hicho kimetokana na Askari Magereza kumfyatulia risasi mfungwa aliyekuwa ameachiwa na Mahakama wakitaka kumkamata tena ndipo risasi walizomfyatulia zikampata Neema na kumuua papo hapo, nyingine zikimjeruhi mama yake mzazi.
_____
Maoni Yangu:
Hivi haya mauaji ya askari kwa RAIA mpaka lini?
========
Dar es Salaam. Neema Dominick mkazi wa Kigamboni Mtaa wa Tuamoyo jijini Dar es Salaam amefariki dunia baada ya kupigwa risasi katika eneo la paja na askari Magereza.
Baada ya risasi iliyomuua Neema kutokea upande wa pili pia ilimjeruhi mama yake mzazi, Rehema Ibrahimu katika eneo la paja.
Mauti hayo yalimpata Neema jana akiwa nyumbani kwao karibu na Mahakama ya Kigamboni wakati askari wa Magereza alipokuwa akijaribu kumzuia mtuhumiwa asitoroke mahakamani.
Akizungumzia tukio hilo, kaka wa marehemu, Juma Mwinjaku alisema kabla ya tukio hilo mtuhumiwa huyo alitoroka kwa mara ya kwanza askari wakafanikiwa kumdhibiti kabla ya kutoroka tena na kuamua kutumia risasi kumzuia.
“Mara zote alipotoroka alikuwa akitumia upande ambao nyumba yetu ipo jambo ambalo lilifanya hata walipotumia risasi kuwa rahisi kutufikia.”
“Lakini kwa nini watumie risasi kumzuia mtuhumiwa ilhali wanajua eneo lile liko karibu na makazi ya watu pamoja na shule? Kwa nini hawaangalii madhara yanayoweza kutokea kwa watu,” alihoji.
“Binti huyo alimaliza kidato cha nne mwaka juzi kuna wakati alikuwa akitaka kwenda jeshini akakosa nafasi hivyo alikuwa yupo nyumbani tu akisubiri utaratibu mwingine,” alisema
Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa aliyekuwa akizuiwa kwa risasi alikuwa tayari ameachiliwa na Mahakama.
Chanzo: Mwananchi