Kifua kikuu cha ng’ombe (bovine tuberclosis)-tb

achengula

JF-Expert Member
Jul 30, 2009
369
62
Ugonjwa wa kifua kikuu cha ng’ombe ni ugonjwa hatari sana wenye madhara makubwa kiafya kwa ng’ombe, mwanadamu na hata katika biashara ya kimataifa. Ni ugonjwa unaosababishwa vimelea vya bakteria wanaojulikana kwa jina la kitaalamu kama Mycobacterium bovis. Kimsingi ni ugonjwa wa mfumo wa upuuaji unaochukua muda mrefu (kuanzia wiki chache hadi maisha yote) kujijenga ndani ya mwili tangu maambukizi hadi kuanza kujitokeza dalili za ugonjwa na kuanza kuambukiza wanyama wengine. TB yaweza kuwapata wanyama wengi lakini mara nyingi ni ng’ombe na nyati. Mwanadamu hupata ugonjwa wa kifua kikuu kutoka kwa ng’ombe au mazao yake, lakini pia mwanadamu anauwezo wa kumuambukiza ng’ombe. Maambukizi yameonekana pia kwa kondoo, mbuzi, farasi, nguruwe, paa, mbwa na paka. Kwa maelezo zaidi (dalili, utambuzi, tiba na uzuiaji) juu ya ugonjwa huu soma hapa SEKTA YA MIFUGO TANZANIA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom