Kifo hakina huruma

Mima white cute

JF-Expert Member
Nov 24, 2017
740
1,305
Ukweli usiopingika kuhusu binadamu .Binadamu tunapitia vupindi Vingi kwenye maisha yetu lakini kuna vipindi huwa ni vigumu hata kuelezeka kipindi cha kufiwa huwa kinauma sana hasa unapofiwa na MTU wako wa karibu .

Nipo kwenye msiba wa jirani yangu hapa.Vilio navyoviona hapa wafiwa wanalia kwa uchungu huwa vinanipotezea kabisa amani ya moyo wangu.Nachukia kifo ila siwezi kushindana na mungu

Sipendi kuhudhuria misiba hasa ila sina jinsi.Na nimetokea kuchukia kwenda misibani sababu najikuta kama Mimi ndio nimefiwa msiba unanikumbusha mbali sana.Msiba unanikumbusha ukiwa nilio nao nilivyopote zawazazi wangu kwa mfululizo yahn mababa wote kwenye familia baba wakubwa wadogo na baba mzazi na matokeo yake tumebaki mayatima familia ya watoto watupu na wanawake inaumiza sana...ukiwa mbaya sana jamanii.

Nahuzuni sana siku ya leo .Lakini nimejifunza kitu kwenye maisha. Ni lazima tufe ili tupishe vizazi vijavyo.

Ahsante mungu kwa kila jambo.
R .I.p dady

qully nafsi dharikat mauti
 
Lazima tuachiane kijiti

jitahidi tu uache jina,

si unamuona hitler mpaka leo tunamuongelea wakati hata fuvu lake lishaoza..way to go
 
Mungu amlaze pema!!!!

Kila nafsi itaionja mauti, tuishi kwa amani na watu wote!!! Ukilala ukiamka salama ni kumshukuru Mungu
 
Hatuna namna yoyote ni lazima tufe tu, tukitaka maisha mengine baada ya kifo basi tuishi maisha yampendezayo Mungu.
Yah ni kweli kabisa..lakini unaweza kupatwa a mitihani ukakufuru mungu na kuhusu Wenda umeonewa.ukawaza kwa nini hakuchukua japo akawabakishia hata wakuwaongoza wa kumkimbilia.

Ukawaza kwa nini ww tu.na kwa nini awachukue wote basi Tena kwa pamoja kwa nini asichukue mmoja na kwengine akachukua mmoja.lakini unapewa mitihani ww MTU mmoja tu.ila hii yote kudhihirisha uwepo wake.kikubwa tuzidishe ibada zetu kwake

Ila kazi ya mungu haina makosa .na namshukuru mungu kwa kila jambo.
 
Hatuna namna yoyote ni lazima tufe tu, tukitaka maisha mengine baada ya kifo basi tuishi maisha yampendezayo Mungu.
Yah ni kweli kabisa..lakini unaweza kupatwa a mitihani ukakufuru mungu na kuhusu Wenda umeonewa.ukawaza kwa nini hakuchukua japo akawabakishia hata wakuwaongoza wa kumkimbilia.

Ukawaza kwa nini ww tu.na kwa nini awachukue wote basi Tena kwa pamoja kwa nini asichukue mmoja na kwengine akachukua mmoja.lakini unapewa mitihani ww MTU mmoja tu.ila hii yote kudhihirisha uwepo wake.kikubwa tuzidishe ibada zetu kwake

Ila kazi ya mungu haina makosa .na namshukuru mungu kwa kila jambo.
 
Mungu amlaze pema!!!!

Kila nafsi itaionja mauti, tuishi kwa amani na watu wote!!! Ukilala ukiamka salama ni kumshukuru Mungu
Kabisa yahni na siku hizi vifo kila siku zamani hakukuwa hivi mnaweza kukaaa mpaka mnasahau Mara ya mwisho mmezika link lakini sasa duhhhh
 
Back
Top Bottom