Kifo cha Mandela kiwe ni kichocheo cha mapigano mapya...

Sep 10, 2013
335
471
Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha mzee wetu Mandela kama watu wengine wengi wapenda haki duniani watakavyokuwa wameguswa,ni kweli kuwa kwa umri wake yapasa kumshukuru Mungu lakini kitendo cha yeye kuwa mzima ilitupa faraja kubwa sana.

Naomba siku tatu za maombolezo zilizotolewa na serikali yetu ziwe za matafakuri makubwa juu ya misingi ya utu aliyoipigania Mandela,mzee huyu alipinga ubaguzi kwa kila njia aliyoweza,leo nchini kwetu ubaguzi ndiyo fasion kwa watawala,mfano siku hizi kuna mahakama za wenye nazo na wasio nazo,kibaka tajiri kosa lake hubatizwa jina jingine na hutamkwa kama "mambo binafsi"sheria
zimepindishwa na kununuliwa na matajiri,najiuliza hivi serikali ya CCM inaujasiri wa kumuenzi Mandela na wakati wanaua hadharani,wanabambikia kesi watu,wanateka,wanafungia vyombo vya habari,wanang'oa kucha na meno ya wanaharakati,naamini Mandela asingependa CCM ya leo iguse jeneza lakewala kushiriki msiba wake kwa namna yoyote ile.

Kwa wanaharakati huu ni mwanzo mpya wa kupigania uhuru wa kweli.Mapambano yanaendelea,leo nitamwongelea kidogo kwenye mkutano wa leo hapa Jimbo la Kisesa.
 
inahitaji weredi na integrity ya hali ya juu sana atokee mtu kama mandela,mfano SA kuna madini mengi sana na Tembo wengi sana kwa jinsi walivyomuamini Mandela angeweza kujinyakulia na kuwa tajiri mkubwa sana barani Afrka na duniani lakini wapi.........hakua na tamaa
 
Mandela hakuwa mbaguzi alikubali Mahakama ya Kadhi kuwepo Afrika ya Kusini.
 
inahitaji weredi na integrity ya hali ya juu sana atokee mtu kama mandela,mfano SA kuna madini mengi sana na Tembo wengi sana kwa jinsi walivyomuamini Mandela angeweza kujinyakulia na kuwa tajiri mkubwa sana barani Afrka na duniani lakini wapi.........hakua na tamaa
Ukiongelea tembo unanipa machungu kwa jinsi akina KINANA wanavyowamaliza kwa ujangili.
View attachment 125177
 
As I walked out the door toward the gate that would lead to my freedom, I knew if I didn't leave my bitterness and hatred behind, I'd still be in prison," Mandela said after he was freed in in 1990.
 
Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha mzee wetu Mandela kama watu wengine wengi
wapenda haki duniani watakavyokuwa wameguswa,ni kweli kuwa kwa umri wake
yapasa kumshukuru Mungu lakini kitendo cha yeye kuwa mzima ilitupa
faraja kubwa sana. Naomba siku tatu za maombolezo zilizotolewa na
serikali yetu ziwe za matafakuri makubwa juu ya misingi ya utu
aliyoipigania Mandela,mzee huyu alipinga ubaguzi kwa kila njia
aliyoweza,leo nchini kwetu ubaguzi ndiyo fasion kwa watawala,mfano siku
hizi kuna mahakama za wenye nazo na wasio nazo,kibaka tajiri kosa lake
hubatizwa jina jingine na hutamkwa kama "mambo binafsi"sheria
zimepindishwa na kununuliwa na matajiri,najiuliza hivi serikali ya ccm
inaujasiri wa kumuenzi Mandela na wakati wanaua hadharani,wanabambikia
kesi watu,wanateka,wanafungia vyombo vya habari,wanang'oa kucha na meno
ya wanaharakati,naamini Mandela asingependa ccm ya leo iguse jeneza lake
wala kushiriki msiba wake kwa namna yoyote ile.Kwa wanaharakati huu ni
mwanzo mpya wa kupigania uhuru wa kweli.

Ccm wamegeuka makaburu, wanaua na kungo'a kucha na meno kwa plaizii!, kubambikiwa kesi ni jambo la kawaida.. Tunaweza sema heri makaburu kuliko ccm ya kipindi hiki.
 
As I walked out the door
toward the gate that would lead to my freedom, I knew if I didn't leave
my bitterness and hatred behind, I'd still be in prison," Mandela said
after he was freed in in 1990.

Quote of a life time
 
Mandela hakuwa mbaguzi alikubali Mahakama ya Kadhi kuwepo Afrika ya Kusini.

mbona wakristo hawana mahakama na hawalalamiki, masuala ya kidini yashughulikiwe na dini zenyewe na kwa gharama zao. ninyi kama mnataka mahakama ya kadhi anzisheni na endesheni kwa gharama zenu. mbona mnafunga ndoa na wakristo halafu mnataka kutumia sheria za kiislamu, kweli itawezekana? tena wengine mnaoa hawana hata dini, je hapo sheria ya kiislamu itafanyaje kazi? mkiendelea hivo wakristo nao watakuja kudai mahakama ya kikristo, matokeo yake hakuna mgogoro utakaotatuliwa maana sheria za kikristo naona ni ngumu kuliko zenu, kwa mfano wao hawaamini katika talaka na kutalikiana nyie mnaamini talaka na kutalikiana, sasa ukiwa umeoa mkristo hilo litakuwaje?

tatueni migogoro yenu kupitia bakwata na jumuiya mlizounda, msitafute kuanzisha vitu ambavyo vitaongeza gharama bila sababu.

kuzungumzia udini na mahakama za kidini haina totafuti na kauli ya Mwl. Nyerere alisema watu wanaozungumzia udini na ukabila wamefilisika sera, hawana ubunifu tena
 
mbona wakristo hawana mahakama na hawalalamiki, masuala ya kidini yashughulikiwe na dini zenyewe na kwa gharama zao. ninyi kama mnataka mahakama ya kadhi anzisheni na endesheni kwa gharama zenu. mbona mnafunga ndoa na wakristo halafu mnataka kutumia sheria za kiislamu, kweli itawezekana? tena wengine mnaoa hawana hata dini, je hapo sheria ya kiislamu itafanyaje kazi? mkiendelea hivo wakristo nao watakuja kudai mahakama ya kikristo, matokeo yake hakuna mgogoro utakaotatuliwa maana sheria za kikristo naona ni ngumu kuliko zenu, kwa mfano wao hawaamini katika talaka na kutalikiana nyie mnaamini talaka na kutalikiana, sasa ukiwa umeoa mkristo hilo litakuwaje?

tatueni migogoro yenu kupitia bakwata na jumuiya mlizounda, msitafute kuanzisha vitu ambavyo vitaongeza gharama bila sababu.

kuzungumzia udini na mahakama za kidini haina totafuti na kauli ya Mwl. Nyerere alisema watu wanaozungumzia udini na ukabila wamefilisika sera, hawana ubunifu tena
Nijalalamika nimemsifia Mandela hakuwa mbaguzi wa dini.
 
Usituharibie mjadala wa hapa, jukwaa lenu la dini lipo, katifuaneni huko kuhusu hizo mahakama, sisi tunamuongelea " The great son of Africa" ambaye Obama kasema, "He no longer belongs to us. He belongs to the ages," "I am one of the countless millions who drew inspiration from Nelson Mandela's life," he continued. "And like so many around the globe, I cannot fully imagine my own life without the example that Nelson Mandela set."
Mandela hakuwa mbaguzi alikubali Mahakama ya Kadhi kuwepo Afrika ya Kusini.
 
Usituharibie mjadala wa hapa, jukwaa lenu la dini lipo, katifuaneni huko kuhusu hizo mahakama, sisi tunamuongelea " The great son of Africa" ambaye Obama kasema, "He no longer belongs to us. He belongs to the ages," "I am one of the countless millions who drew inspiration from Nelson Mandela's life," he continued. "And like so many around the globe, I cannot fully imagine my own life without the example that Nelson Mandela set."
Ukitaka kumuongelea Mandela lazima ugusie kupinga ubaguzi wa aina zote. Usibague aina ya ubaguzi utakuwa na wewe ni mbaguzi.
 
Sasa mbona wewe umebagua aina ya ubaguzi? Basi nawe ni mbaguzi umetaja aina ya ubaguzi!! Hata ukijibaraguza tunajua ugonjwa unaokusumbua. Si ungesema alipinga ubaguzi wa aina yoyote mbona ungeeleweka tu
Ukitaka kumuongelea Mandela lazima ugusie kupinga ubaguzi wa aina zote. Usibague aina ya ubaguzi utakuwa na wewe ni mbaguzi.
 
Back
Top Bottom