komedi
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 204
- 17
Angalia magazeti yetu fulani yalivyokuwa yakiandika vichwa vya habari na linganisha na stori yenyewe.
Mheshimiwa JK Amejiuzulu
Katika hali isiyokuwa ya kawaida( inaendelea ukurasa wa 4).... bwana Jumanne Kazimoto ambaye alikuwa ni mwenyekiti wa kijiji cha manumba mawili wilaya ya Nsuba amejiuzulu rasmi jana mara baada ya kutuhumiwa kuiba sungura wawili wa bi Kimoto wa kijiji cha jirani.....
Dr. Slaa kuhamia CCM leo
Habari nzito tulizozipata punde tu kutoka kwa mwandishi wetu maalum aliyeshiriki katika kikao cha dharura cha kamati kuu ya chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA zinasema kwamba( Inaendelea ukurasa wa 7)......baada ya kuongoza maandamano ya Arusha Dr. Slaa anatarajiwa kuhamia CCM kirumba City yaani mji wa Mwanza baadaye leo kupokea maandamano mengine makubwa........
Lowasa kugombea Urais 2015
Imethibitika rasmi kuwa katika uchaguzi ujao wa( inaendelea ukurasa wa 2)... chama cha mpira wa mkufu wilaya ya Monduli mwaka 2015 bwana mmoja anayejulikana kwa jina la Josephath Sakatai Ngarenanyuki au kwa jina la utani ' Lowasa' atagombea urais wa chama hicho kwa kuwa atakuwa amefikisha miaka inayotakiwa kikatiba kuweza kugombea kwa..........
Yathibitika Waziri wa Serikali ya Kikwete Kabaka
Baada ya mabishano ya chini kwa chini na minong'ono ya hapa na pale sasa imethibitika bila ubishi kuwa mheshimiwa waziri wa kazi na ajira( Inaendelea Ukurasa wa 4)...... aliyechaguliwa katika Baraza jipya la mawaziri ni Bi Gaudensia Kabaka.
Jamani waandishi wa magazeti fulani mnatupasua mioyo wenzenu? Kha! mweh!
Yaani mnataka muuze leo tu? Kesho hapana?
Najua wanajamvi mna mengi upande huu.
Mheshimiwa JK Amejiuzulu
Katika hali isiyokuwa ya kawaida( inaendelea ukurasa wa 4).... bwana Jumanne Kazimoto ambaye alikuwa ni mwenyekiti wa kijiji cha manumba mawili wilaya ya Nsuba amejiuzulu rasmi jana mara baada ya kutuhumiwa kuiba sungura wawili wa bi Kimoto wa kijiji cha jirani.....
Dr. Slaa kuhamia CCM leo
Habari nzito tulizozipata punde tu kutoka kwa mwandishi wetu maalum aliyeshiriki katika kikao cha dharura cha kamati kuu ya chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA zinasema kwamba( Inaendelea ukurasa wa 7)......baada ya kuongoza maandamano ya Arusha Dr. Slaa anatarajiwa kuhamia CCM kirumba City yaani mji wa Mwanza baadaye leo kupokea maandamano mengine makubwa........
Lowasa kugombea Urais 2015
Imethibitika rasmi kuwa katika uchaguzi ujao wa( inaendelea ukurasa wa 2)... chama cha mpira wa mkufu wilaya ya Monduli mwaka 2015 bwana mmoja anayejulikana kwa jina la Josephath Sakatai Ngarenanyuki au kwa jina la utani ' Lowasa' atagombea urais wa chama hicho kwa kuwa atakuwa amefikisha miaka inayotakiwa kikatiba kuweza kugombea kwa..........
Yathibitika Waziri wa Serikali ya Kikwete Kabaka
Baada ya mabishano ya chini kwa chini na minong'ono ya hapa na pale sasa imethibitika bila ubishi kuwa mheshimiwa waziri wa kazi na ajira( Inaendelea Ukurasa wa 4)...... aliyechaguliwa katika Baraza jipya la mawaziri ni Bi Gaudensia Kabaka.
Jamani waandishi wa magazeti fulani mnatupasua mioyo wenzenu? Kha! mweh!
Yaani mnataka muuze leo tu? Kesho hapana?
Najua wanajamvi mna mengi upande huu.