Kifo cha ghafla cha Mfugale sawa na Prof. Chachage: Kuna viashiria vyote vya kupewa sumu. Serikali ichunguze

Ni fumbo kwa kuwa tu kinakuja bila taarifa, ila baada ya hapo ni lazima sababu ijulikane.
Mkuu nimekwambia siyo lazima sababu ijulikane kwa asilimia mia, binadamu siyo Mungu anayejua kila jambo na yale yaliyo sirini.....
 
Miradi mikubwa kama Daraja la Busisi na Bwawa la umeme la nyerere lazima ife ili wapiga dili za vivuko na kampuni za uzalishaji umeme kama IPTL mpya zizalishwe!!!Watu kama mfugale ni mwarobaini wa kuzuia dili hizo sishangai akimfuata mwenda zake na miradi izikwe rasmi!!!NAJARIBU KU CONNECT DOTS TU WAKUU!!!
 
Umesikiliza maelezo ya waziri wake? Najua ugonjwa wake uliokuwa unamsumbua muda.
Ila kilichotokea muda mfupi kabla ya yeye kufariki kitaalam hakina uhusiano wowote na kupanda au kushuka kwa lile tatizo lake.
Ulitaka wakwambie Corona imemuuwa au?.
 
SAWA.
Mengi uliyoandika ni sahihi. Lakini ushuhuda wako hauna msingi wowote katika kuondoa uwezekano wa COVID-19 kuhusika.

Na hayo uliyoeleza, siyo kwamba ndio sehemu kamilifu ya matatizo yanayoambatana na COVID-19; kwa sababu bado kuna mengi yasiyofahamika juu ya ugonjwa wenyewe; na ukichukulia kwamba siyo wagonjwa wote ni lazima waonyeshe dalili hizo na kwa nyakati hizo ulizotaja wewe.

Ulijua kwamba Mfugale kabla hajafariki hakuwa na baadhi ya dalili hizo, hata kama alikuwa halalamiki juu yake? Siyo watu wote huonyesha dalili hizo ulizotaja kwa ukubwa wa kuwatia hofu na kuanza kutafuta msaada, hasa ukichukulia tabia za watu wengi kujihisi kuwa miili yao ni imara. Wanasubiri hadi hali iwe ngumu zaidi kabla ya kutafuta msaada.

Kinachozungumziwa hapa ni kutojua ni nini hasa kinaweza kuwa kimesababisha au kimechangia kifo cha Mfugale. Ni kazi ndogo sana sasa kupima na kujua kama marehemu alikuwa na COVID-19 au hapana.

Hii ni hatua moja ya kujaribu kutambua sababu za kifo cha ghafla.
Sikuandika maoni yangu ila nimekupa taarifa zilizoandikwa na madakatari waliofanya utafiti wa kina kuhusu ugonjwa huu. Ninakubaliana nao kwa sababu hali ilivyokuwa hapa kwetu watu walikufa zaidi ya 6,000 (siyo mji mkubwa sana) lakini walikuwa hawaugui na kufa ghafla tu. Ilifikia kugeuza viwanja vya michezo ya ndani kuwa hospitali za dharura kwa vile mahospitali yalikuwa yamejaa.
 
Mkuu, kwenye matukio ya hao watu, ilithibitika wazi kwamba walipewa sumu?

Ushahidi upo, au niyale yale ya semwayo mitaani?

Sina sababu za kutilia mashaka utaalam wako kama ulivyojieleza hapo juu, lakini swali langu liko wazi kabisa. Naomba ulijibu bila ya wasi wowote.

Kuna kitu hata mimi bado kinanishangaza mimi.

Inakuwaje ndugu wa marehemu wawe wanalalamika tu, huku wakikubali kwenda kumzika ndugu yao kabla ya kujiridhisha kwamba hakufanyiwa mchezo mchafu?

Ninashindwa kabisa kulielewa hili. Sasa wakishazika, wataendelea tena kulalamika?

Kwa kawaida ningetegemea, hata bila ya ndugu kuhimiza:

1. Hospitali wawe wameufanyia postmortem mwili ili kujua chanzo cha mauti yake, matatizo ya moyo, upumuaji ,n.k.; lakini sijui kama haya yalifanyika (itakuwa ni ajabu kama haikufanyika postmortem); na kwa kifo cha ghafla kama hiki, na uwezekano wa uwepo wa mchezo mchafu, ndugu nao wangekaribishwa, au wangeombwa/wangeomba awepo mwakilishi wao katika uchunguzi huo.

2. Sasa hivi, uwepo wa COVID-19, itashangaza sana, kama hapakuwepo vipimo vya COVID-19, ili kujiridhisha kwamba haikuwa sehemu ya matatizo yaliyomsababishia kifo.

3.Sampuli za damu, masalia ya chakula tumboni mwa marehemu, ndugu wangehakikisha sampuli hizo zinachukuliwa na kufanyiwa uchunguzi, chini ya uangalizi wao

Sasa sijui kama yote haya yamefanyika. Kama yamefanyika, basi kama ni sumu kapewa, kuna uwezekano ikajulikana ni sumu gani, halafu huo utakuwa ni mwanzo wa kumtafuta aliyefanya kazi hiyo.

Maelezo yaliyotolewa na wizara kufuatia kifo cha Mfugale yanaacha maswali mengi juu ya kifo chake.
Kifo kinapotokea ghafla Post moterm ni jambo la muhimu ili tatizo lililosababisha mauti kwa mhanga liweze kupatiwa ufumbuzi ili isitokee kwa mwingine. "The deads like the living but the living run away from the dead". Matokeo ya post moterm yameleta ufumbuzi kwenye mambo mengi ikiwemo magonjwa na jinsi ya kuyakabili, upangaji wa mauaji na jinsi ya kudhibiti, kuwaondoa watu katika hatia kutokana na kuhusishwa na vifo vya wengine. hii habari ya kuwa mpaka ndugu watake haijakaa sawa kabisa.
 
Sikuandika maoni yangu ila nimekupa taarifa zilizoandikwa na madakatari waliofanya utafiti wa kina kuhusu ugonjwa huu. Ninakubaliana nao kwa sababu hali ilivyokuwa hapa kwetu watu walikufa zaidi ya 6,000 (siyo mji mkubwa sana) lakini walikuwa hawaugui na kufa ghafla tu. Ilifikia kugeuza viwanja vya michezo ya ndani kuwa hospitali za dharura kwa vile mahospitali yalikuwa yamejaa.
Huelewi kilichoandikwa basi.

Hao madaktari wamesema kwene ripoti yao kwamba hakuna dalili nyingine zozote, na kwamba walichoandika ndicho kichukuliwe kama hitimisho juu ya ugonjwa huo?

COVID-19, bado ina'evolve', hakuna anayejua dalili zote na madhara yote inayosababisha kwa watu wote wanaopata ugonjwa huo.

Kwa hiyo, wewe hapo unakazania maoni ambayo hujui yanazungumzia kitu gani, na unayakomalia kweli kweli kama unavyoonyesha hapa.
Lakini hiyo si ajabu, kwa sababu unajulikana kukomalia mambo ambayo hata hayana msingi wowote, kama ule uwanja wa ndege wa Chato.
 
Au Utopolo wamemtoa kafara Kwa ushindi wa leo?
IMG-20210703-WA0011.jpg
 
Mkuu, kwenye matukio ya hao watu, ilithibitika wazi kwamba walipewa sumu?

Ushahidi upo, au niyale yale ya semwayo mitaani?

Sina sababu za kutilia mashaka utaalam wako kama ulivyojieleza hapo juu, lakini swali langu liko wazi kabisa. Naomba ulijibu bila ya wasi wowote.

Kuna kitu hata mimi bado kinanishangaza mimi.

Inakuwaje ndugu wa marehemu wawe wanalalamika tu, huku wakikubali kwenda kumzika ndugu yao kabla ya kujiridhisha kwamba hakufanyiwa mchezo mchafu?

Ninashindwa kabisa kulielewa hili. Sasa wakishazika, wataendelea tena kulalamika?

Kwa kawaida ningetegemea, hata bila ya ndugu kuhimiza:

1. Hospitali wawe wameufanyia postmortem mwili ili kujua chanzo cha mauti yake, matatizo ya moyo, upumuaji ,n.k.; lakini sijui kama haya yalifanyika (itakuwa ni ajabu kama haikufanyika postmortem); na kwa kifo cha ghafla kama hiki, na uwezekano wa uwepo wa mchezo mchafu, ndugu nao wangekaribishwa, au wangeombwa/wangeomba awepo mwakilishi wao katika uchunguzi huo.

2. Sasa hivi, uwepo wa COVID-19, itashangaza sana, kama hapakuwepo vipimo vya COVID-19, ili kujiridhisha kwamba haikuwa sehemu ya matatizo yaliyomsababishia kifo.

3.Sampuli za damu, masalia ya chakula tumboni mwa marehemu, ndugu wangehakikisha sampuli hizo zinachukuliwa na kufanyiwa uchunguzi, chini ya uangalizi wao

Sasa sijui kama yote haya yamefanyika. Kama yamefanyika, basi kama ni sumu kapewa, kuna uwezekano ikajulikana ni sumu gani, halafu huo utakuwa ni mwanzo wa kumtafuta aliyefanya kazi hiyo.

Maelezo yaliyotolewa na wizara kufuatia kifo cha Mfugale yanaacha maswali mengi juu ya kifo chake.
Ndio. Mtu analalamika kuwa naumwa wanamwambia kapumzike ofisini badala ya kumkimbiza hospitali. Inatia shaka hata familia wanaposema hata hospitali hawajasema sababu ya kifo. This is very unprofessional kama sio yamepangwa. Waondoe haya mashaka yaliyoonyeshwa na familia ya marehemu.
 
Habari wana JF.

Leo nimefuatilia live wakati Eng. Mfugale anaagwa Dar. Kwa maelezo machache ya familia, idara na wizara ni wazi kabisa Eng. Mfugale alipewa sumu.

Wito wangu kwa Serikali ifanye uchunguzi wa kina kwa kutumia vyombo na njia zote. Kwa sababu bado hajazikwa nafasi ya uchunguzi wa kina bado ipo.

Kifo cha Eng. Mfugale kimefanana kabisa na kifo cha Prof. Chachage pale Kibaha kwenye kikao.

Nina sababu nyingi za kwanini nasema hivyo, nachelea ziandika hapa kwa sababu inaweza ishia toa hints zangu (taaluma na kazi yangu). Nimefunzwa vyema maeneo hayayalehayale (sitaki toa codes).

Pia nilifuatilia vyema issues za Prof. Chachage, Dr. Mwakyembe, Dr. Omary A. Juma kwa kutaja wachache.

NB: Pia nipo JF kitambo sana; wauaji au serikali wanaweza kuja na hoja mufilisi ya ugeni wa akaunti yangu. Hii ipo kimkakati na hii ndiyo chapisho langu la kwanza.

Best Regards;
Uviko 19 in 2021.
HUYO KAFA KWA "MALIPO MARA 2" KWA WAKANDARASI. Acha akasalimiane na mwendazake! wezi wakubwa!
 
Binadamu bana, haya sasa tumechunguza kapewa sumu, DEJAVU haya atarudi kuwa hai??

Kifo hakikosi sababu! Mfugale kafariki POLE kwa familia apumzike kwa amani.
Kina Azory, Ben walipotea nao pia POLE kwa familia.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Najaribu kufikiri tu , kama marehemu alikuwa anajiuliza swali hili baada ya kifo cha hayati , Nini hatma ya kazi yangu?
Basi hicho kikao kilikuwa na muingiliano wa jibu wa hilo swali.

NB :
Ubaya wa inshu za kuondoa roho ni kuwa, wanaoratibu lazima waondolewe kwa njia hiyo....ndio maana kuna mmoja tayari kapewa siku zisizozidi 1835 za mwisho mwisho...
 
Habari wana JF.

Leo nimefuatilia live wakati Eng. Mfugale anaagwa Dar. Kwa maelezo machache ya familia, idara na wizara ni wazi kabisa Eng. Mfugale alipewa sumu.

Wito wangu kwa Serikali ifanye uchunguzi wa kina kwa kutumia vyombo na njia zote. Kwa sababu bado hajazikwa nafasi ya uchunguzi wa kina bado ipo.

Kifo cha Eng. Mfugale kimefanana kabisa na kifo cha Prof. Chachage pale Kibaha kwenye kikao.

Nina sababu nyingi za kwanini nasema hivyo, nachelea ziandika hapa kwa sababu inaweza ishia toa hints zangu (taaluma na kazi yangu). Nimefunzwa vyema maeneo hayayalehayale (sitaki toa codes).

Pia nilifuatilia vyema issues za Prof. Chachage, Dr. Mwakyembe, Dr. Omary A. Juma kwa kutaja wachache.

NB: Pia nipo JF kitambo sana; wauaji au serikali wanaweza kuja na hoja mufilisi ya ugeni wa akaunti yangu. Hii ipo kimkakati na hii ndiyo chapisho langu la kwanza.

Best Regards;
Uviko 19 in 2021.
Tuacheni uzushi, Afrika vifo vyote ni vya kulishwa sumu, kuuawa na kurogwa! Hakuna kifo cha kawaida! Tuacheni ramli chonganishi, hii siyo sawa kabisa!
 
Back
Top Bottom