Kifo cha Gaddafi ni fedheha kwa bara la Afrika na kejeli kwa kizazi chetu

Civilian Coin

JF-Expert Member
Dec 2, 2012
2,305
4,332
Kutoka Fb nawe shiriki hii post,

KIFO CHA GADAFI NI FEDHEHA KWA BARA LA AFRIKA NA KEJERI KWA KIZAZI CHETU, UNITED NATION JITAZAMENI MLIPOJIKWAA

Mimi si mshabiki wa watenda dhambi bali ni mshabiki wa watu wanaojali maslahi ya taifa lao, kama Gadafi alifanya mema kwa maslahi ya Taifa lake, sioni kosa lake, na kama kosa lake ni kugoma kuwapa rutuba mataifa ya nje basi sio kosa na kama kosa ni kukaaa madarakani kwa muda mrefu basi ilitakiwa ashinikizwe kuitisha uchaguzi na kumpindua kupitia matokeo ya uchaguzi.

Lakini sio mtu mweupe aliyetufedhehesha wana wa Afrika bali ni mtu mwenzetu mweusi mwenzetu aliyepewa dhamana na mamlaka katika nchi ya watu weupe na akatupindua Libya, je, Mweupe ana akili sana ameona yeye akimwaga damu atalaaniwa na akaona ni bora amtume mweusi mwenzao akamwage damu au? Mimi sijui na jaribu kutafakari kama tunaweza kusaidiana. Kama Gadafi alikuwa na ugomvi binafsi na familia flani basi wangemalizana wao kwa chuki zao, kuliko kuasiri taifa zima la Libya na wanachi wake. Leo Libya wanamkumbuka Gadafi, yale mema aliyoyafanya sasa hayapo tena, je, huenda walimpindua ilikuweka vibaraka wao? Lakini Gadafi kwangu mimi Yupo hai mbele za Mungu maana ni mmoja ya watu wema katika bara la afrika.

Nchi za magharibi hazina uwezo wa rasilimali bali zinategemea Afrika ndio iwasaidie na kusababisha kuitwa Nchi zinazoendelea kutokana na kupata rasilimali Afrika. Je, kwanini wasituheshimu na wanatufanyia unyama badala ya kutafta mbinu mbadala ya kuepuka kumwaga damu za watu wasio na hatia hasa wananchi. Tusichukiane kisa tumeshindwa kufikia muafaka wa makubaliano ya kimaslahi. Tujifunze kuwa na hekima ya kutatua matatizo, U.N inanafasi kubwa sana ya kubadilisha mfumo mzima wa Kiutawala Dunia nzima lakini yote haya tunatakiwa kupata Katibu Mkuu wa U. N mwenye Hekima na Busara zaidi ya akili zake ili kujenga Dunia nzima katika mfumo safi. Mimi ni Mtanzania niliyeguswa na Kifo cha Rais gadafi lakini sina meno ya kujitokeza hadharani na kusema ukweli wa namna gani tusuluhishe migogoro binafsi na namna gani tulipe kisasi bila kuathiri wengine.

Naitwa DEOGRATIUS KISANDU

Kijakazi Cha roho Mtakatifu.

7 Dec 2016.
 
Upumbavu ni mzigo!

Gaddafi kafa kwa ujinga na tamaa zake. Mtu tajiri wa mali na anasa, akiilisha kabila yake mema huku akiwaacha wengine hoi kule Benghazi leo hii atangazwe mtakatifu nje ya ardhi yake na kibaraka mweusi.

Kwani hizi habari za kwamba Walibya wanamlilia Gaddafi mnazisikia kwa Walibya wote au watu wa familia yake? Mmesahau kuwa ni Gaddafi huyu huyu alifadhili uharamia?
 
Ulisubiri afe ndo upost pumba zako, aliwindwa siku ngapi mbona ulidhan film

Duh...una sababu gani ya kujibu kwa namna hiyo???!!! Huwezi kutumia lugha ya ustaarabu kumjibu mwenzio???
 
Duh...una sababu gani ya kujibu kwa namna hiyo???!!! Huwezi kutumia lugha ya ustaarabu kumjibu mwenzio???

Bara inamatatizo mengi alafu yeye analeta upumbavu, na wewe ipo siku utasema Mseveni hakutendewa haki siku haya ya Ghadafi yakimkuta....ni vizuri kuwatetea watu smart siyo wanaoingia madarakani kwa nia nzuri alafu wanageuka kua nyoka tena.
Kheri ya sikuku njema
 
Bara inamatatizo mengi alafu yeye analeta upumbavu, na wewe ipo siku utasema Mseveni hakutendewa haki siku haya ya Ghadafi yakimkuta....ni vizuri kuwatetea watu smart siyo wanaoingia madarakani kwa nia nzuri alafu wanageuka kua nyoka tena.
Kheri ya sikuku njema


Duh....siwezi kuendelea tena baada ya kuona kuna 'alafu', 'Mseveni', 'kua'.....
 
Upumbavu ni mzigo!

Gaddafi kafa kwa ujinga na tamaa zake. Mtu tajiri wa mali na anasa, akiilisha kabila yake mema huku akiwaacha wengine hoi kule Benghazi leo hii atangazwe mtakatifu nje ya ardhi yake na kibaraka mweusi.

Kwani hizi habari za kwamba Walibya wanamlilia Gaddafi mnazisikia kwa Walibya wote au watu wa familia yake? Mmesahau kuwa ni Gaddafi huyu huyu alifadhili uharamia?
Aliyesema jf kuna shetan hukukosea,leo nimeamini.
 
Duh...una sababu gani ya kujibu kwa namna hiyo???!!! Huwezi kutumia lugha ya ustaarabu kumjibu mwenzio???
kama unamwabudu ni wew kwanza hayatuhusu ya gadaff, mmefumdishwa kueneza chuki pasipo haki na halali, wakat anasakwa mlikua mkitazama porn au ili afe mpate la kapost, mnakera jichunguzen, watz tunamkumbuka Nyerere, Gaddafi na Libya wenzake ka walibya mkaishi kule tu
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom