magistergtz
JF-Expert Member
- Dec 17, 2011
- 282
- 56
Kuna wengi walodai kuwa jk na serikali yake ni legelege. Zipo pia takwimu za kisayansi kuonesha kiwango cha uongozi duni wa jk; mfano ni zile za mfumuko wa bei unaoambatana na kupanda kwa gharama za maisha; kushuka kwa kiwango cha elimu, kushuka kwa morali ya wafanyakazi, kuongezeka kwa utegemezi wa nchi, ufisadi na wizi wa mali za umma, na mengine mengi. Haya yote yako wazi kwa kila mwenye akili nzuri, na mtu huitaji nguvu nyingi kumfanya mtanzania ayaone. Hivo. nakubaliana na takwimu zote hizo ambazo zimewafanya baadhi ya wadau waione serikali ya jk janga la kitaifa.
Hata hivo, mnyonge mnyongeni, haki yake mpe. Kubali kataa Jk amefanya kazi nzuri ya kuwaepusha watanzania na ccm. Hii kazi ameifanikisha kwa asilimia kubwa na anaendelea vizuri kuikamilisha. Tumpongeze kwa hili maana walau liko wazi kwamba 2015 ccm itazikwa lasmi, na jk mwenyewe agongelea msumari wa mwisho ktk jeneza lake.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki. Jk
Hata hivo, mnyonge mnyongeni, haki yake mpe. Kubali kataa Jk amefanya kazi nzuri ya kuwaepusha watanzania na ccm. Hii kazi ameifanikisha kwa asilimia kubwa na anaendelea vizuri kuikamilisha. Tumpongeze kwa hili maana walau liko wazi kwamba 2015 ccm itazikwa lasmi, na jk mwenyewe agongelea msumari wa mwisho ktk jeneza lake.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki. Jk