Kifo cha CCM ni mafanikio makubwa JK alowapa watanzania

magistergtz

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
282
56
Kuna wengi walodai kuwa jk na serikali yake ni legelege. Zipo pia takwimu za kisayansi kuonesha kiwango cha uongozi duni wa jk; mfano ni zile za mfumuko wa bei unaoambatana na kupanda kwa gharama za maisha; kushuka kwa kiwango cha elimu, kushuka kwa morali ya wafanyakazi, kuongezeka kwa utegemezi wa nchi, ufisadi na wizi wa mali za umma, na mengine mengi. Haya yote yako wazi kwa kila mwenye akili nzuri, na mtu huitaji nguvu nyingi kumfanya mtanzania ayaone. Hivo. nakubaliana na takwimu zote hizo ambazo zimewafanya baadhi ya wadau waione serikali ya jk janga la kitaifa.

Hata hivo, mnyonge mnyongeni, haki yake mpe. Kubali kataa Jk amefanya kazi nzuri ya kuwaepusha watanzania na ccm. Hii kazi ameifanikisha kwa asilimia kubwa na anaendelea vizuri kuikamilisha. Tumpongeze kwa hili maana walau liko wazi kwamba 2015 ccm itazikwa lasmi, na jk mwenyewe agongelea msumari wa mwisho ktk jeneza lake.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki. Jk
 
Kumlilia mtu kwamba kafa kabla hajafa ni uthibitisho kwamba ataishi muda mrefu.

Hadi kaburi lichimbwe na kufukia ndipo machozi ya kumlilia marehemu hufutwa.

CCM bado wameshika dola utasema kirahisi tu kwamba kimekufa!!!!!!!!!!!
 
Kumlilia mtu kwamba kafa kabla hajafa ni uthibitisho kwamba ataishi muda mrefu.

Hadi kaburi lichimbwe na kufukia ndipo machozi ya kumlilia marehemu hufutwa.

CCM bado wameshika dola utasema kirahisi tu kwamba kimekufa!!!!!!!!!!![
yaaan hayo yote unayoyaona na kuyasikia ktk taifa hili huwez hata kutumia akili kdgo tu na kutambua tunapoelekea??? japo kuwa wanadola ila habari kamili na hali halis wanaishilia!! je unahitaj uthibitisho gan???
 
Kuna wengi walodai kuwa jk na serikali yake ni legelege. Zipo pia takwimu za kisayansi kuonesha kiwango cha uongozi duni wa jk; mfano ni zile za mfumuko wa bei unaoambatana na kupanda kwa gharama za maisha; kushuka kwa kiwango cha elimu, kushuka kwa morali ya wafanyakazi, kuongezeka kwa utegemezi wa nchi, ufisadi na wizi wa mali za umma, na mengine mengi. Haya yote yako wazi kwa kila mwenye akili nzuri, na mtu huitaji nguvu nyingi kumfanya mtanzania ayaone. Hivo. nakubaliana na takwimu zote hizo ambazo zimewafanya baadhi ya wadau waione serikali ya jk janga la kitaifa.

Hata hivo, mnyonge mnyongeni, haki yake mpe. Kubali kataa Jk amefanya kazi nzuri ya kuwaepusha watanzania na ccm. Hii kazi ameifanikisha kwa asilimia kubwa na anaendelea vizuri kuikamilisha. Tumpongeze kwa hili maana walau liko wazi kwamba 2015 ccm itazikwa lasmi, na jk mwenyewe agongelea msumari wa mwisho ktk jeneza lake.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki. Jk

Majister hili bonge la article nimelipesti na kulihifadhi mahali. Weldone jf umeifanya week end yangu kuwa nzuri saana
 
Majister hili bonge la article nimelipesti na kulihifadhi mahali. Weldone jf umeifanya week end yangu kuwa nzuri saana

huyu jk anavichembe chembe vya upinzani na ameingia kwa gia kuwa yeye ni m ccm lakini ukiangalia kwa undani utagundua kuwa anaisambaratisha ccm kiujanja ujanja, hivi mnamkumbuka MICHAEL GOLBACHEV WA RUSSIA BY THAT TIME? ALIFANYA HIVI HIVI KAMA JK NA MWISHO DOLA KUBWA ILISAMBARATIKA.
 
Huu wimbo wa kifo cha CCM ni moja kati ya mbinu za kukiimarisha chama hicho. Kuna usemi adui muombee njaa ila akijua unamuombea njaa anatumia kila njia kujiimarisha kwenye suala la chakula.

Sidhani kama CCM inakufa na nisingependa CCM ife kwani role ya CCM ni ileile ambayo leo hii ni role ya CDM. Mimi binafsi siiombei CCM kifo ila ninaiombea ipoteze dola na hilo ndilo lengo hasa la kuwa na vyama vingi. Kuufanya uongozi wa nchi kuwa ni dhamana ya wananchi na si mali ya chama fulani.

Ninaamini CCM bora na imara yenye watu wenye nzuri na nchi ni jambo jema kwa Tanzania. Ila kuipata CCM ya aina hiyo ni sharti CCM itolewe madaraka kwa muda na kupukutisha kupe wote walijipachika katika chama hicho kwa lengo la kuinyonya nchi. I wish Tanzania tungekuwa na vyama vikuu viwili yaani CCM na kingine kama CDM vikiwa na ushawishi unaowiana katika jamii na kuwa na viti vya wabunge vinavyokaribiana ili kuleta national concesus kwenye mambo muhimu badala ya party monopoly.

Nafikiri tusiiombee kifo CCM tuiombee ikubali kushindwa katika chaguzi na kukubali Tanzania kuwa na fair and free elections, kwanza kukiwa na fair and free elections itakuwa pia ni heathy issue kwa uhai wa CCM kwani mtindo wa kutoa rushwa ndani ya chama kugombea uteuzi haitakuwa guarantee ya kuingia Ikulu, na hivyo itasababisha watu waache kuchukua risks za kuhonga wajumbe wakati uongozi unatoka kwa wananchi.
 
Kuna wengi walodai kuwa jk na serikali yake ni legelege. Zipo pia takwimu za kisayansi kuonesha kiwango cha uongozi duni wa jk; mfano ni zile za mfumuko wa bei unaoambatana na kupanda kwa gharama za maisha; kushuka kwa kiwango cha elimu, kushuka kwa morali ya wafanyakazi, kuongezeka kwa utegemezi wa nchi, ufisadi na wizi wa mali za umma, na mengine mengi. Haya yote yako wazi kwa kila mwenye akili nzuri, na mtu huitaji nguvu nyingi kumfanya mtanzania ayaone. Hivo. nakubaliana na takwimu zote hizo ambazo zimewafanya baadhi ya wadau waione serikali ya jk janga la kitaifa.

Hata hivo, mnyonge mnyongeni, haki yake mpe. Kubali kataa Jk amefanya kazi nzuri ya kuwaepusha watanzania na ccm. Hii kazi ameifanikisha kwa asilimia kubwa na anaendelea vizuri kuikamilisha. Tumpongeze kwa hili maana walau liko wazi kwamba 2015 ccm itazikwa lasmi, na jk mwenyewe agongelea msumari wa mwisho ktk jeneza lake.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki. Jk

Naunga mkono hoja.
 
Kuna wengi walodai kuwa jk na serikali yake ni legelege. Zipo pia takwimu za kisayansi kuonesha kiwango cha uongozi duni wa jk; mfano ni zile za mfumuko wa bei unaoambatana na kupanda kwa gharama za maisha; kushuka kwa kiwango cha elimu, kushuka kwa morali ya wafanyakazi, kuongezeka kwa utegemezi wa nchi, ufisadi na wizi wa mali za umma, na mengine mengi. Haya yote yako wazi kwa kila mwenye akili nzuri, na mtu huitaji nguvu nyingi kumfanya mtanzania ayaone. Hivo. nakubaliana na takwimu zote hizo ambazo zimewafanya baadhi ya wadau waione serikali ya jk janga la kitaifa.

Hata hivo, mnyonge mnyongeni, haki yake mpe. Kubali kataa Jk amefanya kazi nzuri ya kuwaepusha watanzania na ccm. Hii kazi ameifanikisha kwa asilimia kubwa na anaendelea vizuri kuikamilisha. Tumpongeze kwa hili maana walau liko wazi kwamba 2015 ccm itazikwa lasmi, na jk mwenyewe agongelea msumari wa mwisho ktk jeneza lake.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki. Jk

Deni la Taifa limeongezeka kwa 38% kutoka mwaka wa fedha 2009/10 Trillion10.5 mpaka 2010/11 Trillion14.5.

Source: CAG report
 
CCM haifai lakini bado hakuna upinzani hovyo kabisa. tuwaombee wote waimarike ili tupate viongozi 2015.
 
Huu wimbo wa kifo cha CCM ni moja kati ya mbinu za kukiimarisha chama hicho. Kuna usemi adui muombee njaa ila akijua unamuombea njaa anatumia kila njia kujiimarisha kwenye suala la chakula.

Sidhani kama CCM inakufa na nisingependa CCM ife kwani role ya CCM ni ileile ambayo leo hii ni role ya CDM. Mimi binafsi siiombei CCM kifo ila ninaiombea ipoteze dola na hilo ndilo lengo hasa la kuwa na vyama vingi. Kuufanya uongozi wa nchi kuwa ni dhamana ya wananchi na si mali ya chama fulani.

Ninaamini CCM bora na imara yenye watu wenye nzuri na nchi ni jambo jema kwa Tanzania. Ila kuipata CCM ya aina hiyo ni sharti CCM itolewe madaraka kwa muda na kupukutisha kupe wote walijipachika katika chama hicho kwa lengo la kuinyonya nchi. I wish Tanzania tungekuwa na vyama vikuu viwili yaani CCM na kingine kama CDM vikiwa na ushawishi unaowiana katika jamii na kuwa na viti vya wabunge vinavyokaribiana ili kuleta national concesus kwenye mambo muhimu badala ya party monopoly.

Nafikiri tusiiombee kifo CCM tuiombee ikubali kushindwa katika chaguzi na kukubali Tanzania kuwa na fair and free elections, kwanza kukiwa na fair and free elections itakuwa pia ni heathy issue kwa uhai wa CCM kwani mtindo wa kutoa rushwa ndani ya chama kugombea uteuzi haitakuwa guarantee ya kuingia Ikulu, na hivyo itasababisha watu waache kuchukua risks za kuhonga wajumbe wakati uongozi unatoka kwa wananchi.

Wala hata haiko hivyo!, Wahenga walisema, Sikio la kufa halisikii dawa; Sema chochote cha kuiamsha CCM usingizini, lakini kamwe haiwezi kuamka, tayari imejitwisha jeneza lake ikielekea kaburini!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom