Baraka21
JF-Expert Member
- Mar 15, 2021
- 1,265
- 3,177
Kumekuwa na hii tabia hasa kwenye makanisa ya kilokole kumuita Mchungaji wako kuwa ni baba yako wa kiroho.
Huyu ni mtu ambaye hutakiwi kufanya jambo lolote bila kumshirikisha. Ukitaka kuoa au kuolewa lazima ukamuulize kwanza, umepata kiwanja lazima umuulize kuwa ununue au usinunue, unataka kuanza ujenzi lazima umwambie, mkeo hataki kutoa unyumba lazima umshirikishe.
Mwisho lazima ajue kipato chako chote na mapato na matumizi ikiwemo michango ya kanisani.
Kuna watu TB Joshua alikuwa ndio baba yao wa kiroho yaani tumaini lao lote lilikuwa kwa TB JOSHUA. Kila mwaka ilikuwa lazima waende SCOAN mara moja au mara mbili kwa baba yao. Leo hii baba yao wa kiroho amekufa hawana tena direction/muelekeo wa maisha ya kiroho. Wao walimuamini mwanadamu sio Mungu.
Wapendwa naomba tuweke tumaini letu kwa Mungu sio wanadamu. Mungu hafi, halali wala hasinzii.
AMELAANIWA YULE AMTEGEMEAYE MWANADAMU.
Huyu ni mtu ambaye hutakiwi kufanya jambo lolote bila kumshirikisha. Ukitaka kuoa au kuolewa lazima ukamuulize kwanza, umepata kiwanja lazima umuulize kuwa ununue au usinunue, unataka kuanza ujenzi lazima umwambie, mkeo hataki kutoa unyumba lazima umshirikishe.
Mwisho lazima ajue kipato chako chote na mapato na matumizi ikiwemo michango ya kanisani.
Kuna watu TB Joshua alikuwa ndio baba yao wa kiroho yaani tumaini lao lote lilikuwa kwa TB JOSHUA. Kila mwaka ilikuwa lazima waende SCOAN mara moja au mara mbili kwa baba yao. Leo hii baba yao wa kiroho amekufa hawana tena direction/muelekeo wa maisha ya kiroho. Wao walimuamini mwanadamu sio Mungu.
Wapendwa naomba tuweke tumaini letu kwa Mungu sio wanadamu. Mungu hafi, halali wala hasinzii.
AMELAANIWA YULE AMTEGEMEAYE MWANADAMU.