Kidato Cha NNE Kesho Wataanza Mitihani Ya Mwisho ya Taifa.....Katibu Mkuu NECTA awaasa kutojihusisha na udanganyifu

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,395
Watahiniwa 385,938 wanatarajiwa kutafanya mtihani wa Taifa wa kidato cha nne nchini.

Akizungumza leo Jumapili, Oktoba 29,2017 Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde amesema kati ya watahiniwa hao, 323,513 ni wa shule na 62,425 ni wa kujitegemea.

Dk Msonde amesema mtihani huo utaanza kesho Oktoba 30,2017 hadi Novemba 17,2017.

Dk Msonde amesema maandalizi ya mitihani yameshakamilika."Hivi ninavyozungumza mitihani imeshafika kwenye vituo.”

Amezitaka kamati za mitihani za mikoa na halmashauri kuhakikisha utaratibu wa uendeshaji wa mitihani unafuatwa.

Katibu mtendaji huyo amewataka wanafunzi kuacha vitendo vya udanganyifu wakati wa kufanya mitihani kwa kuwa wanaweza kufaulu bila kufanya hivyo.

"Mliyojifunza yanatosha fanyeni mitihani kwa kufuata utaratibu uliowekwa," amesema.

Dk Msonde amesema baraza hilo halitasita kuwafutia mitihani wote watakaojihusisha na udanganyifu.

- Mpekuzi
 
Hata Katika Ndoa Unaweza Kucheat ili Ndowa Yako Idumu!
By the Way! Kuna Group lolote la Watsapp Kwa Ajili ya Wanafunzi Wanaofanya Mtihani Kidato cha Nne?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom