Orketeemi
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 4,313
- 10,017
SIKIA
Bissmillah naanza, kwa jina lake manani,
Kwa maneno nakufunza, na wala sina utani,
Umeshageuka funza,kutukuza ushetani.
Ewe kiumbe sikia, yalo mazuri chukua.
Unaliza waungwana, kwa kuupenda ubwana,
Wasababisha tosana, badala ya kuungana,
Kila Mara kutishana, raha kwako kuuana,
Ewe kiumbe sikia, yalo mazuri chukua.
Wafanya hofu tawala, mwenye akili ni wewe,
Umbwa wadogo wawala, kwa kutaka sujudiwe,
Vyote shaghalabaghala, twahitaji tuachiwe,
Ewe kiumbe sikia, yalo mazuri chukua.
Umeshachokwa na wote, tatuingiza vitani,
Ukisemwa na yeyote, namuweka matatani,
Fikra zako zi kiwete, mithili ya punguani,
Ewe kiumbe sikia, yalo mazuri chukua.
Bissmillah naanza, kwa jina lake manani,
Kwa maneno nakufunza, na wala sina utani,
Umeshageuka funza,kutukuza ushetani.
Ewe kiumbe sikia, yalo mazuri chukua.
Unaliza waungwana, kwa kuupenda ubwana,
Wasababisha tosana, badala ya kuungana,
Kila Mara kutishana, raha kwako kuuana,
Ewe kiumbe sikia, yalo mazuri chukua.
Wafanya hofu tawala, mwenye akili ni wewe,
Umbwa wadogo wawala, kwa kutaka sujudiwe,
Vyote shaghalabaghala, twahitaji tuachiwe,
Ewe kiumbe sikia, yalo mazuri chukua.
Umeshachokwa na wote, tatuingiza vitani,
Ukisemwa na yeyote, namuweka matatani,
Fikra zako zi kiwete, mithili ya punguani,
Ewe kiumbe sikia, yalo mazuri chukua.