Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Gazeti Very Classic kwa habari za kufichua maovu ya chini ya zulia, Risasi Jumatano, lipo kamili kuanika kila kitu, jinsi mtego ulivyoandaliwa mpaka fumanizi ambalo lilichukua nafasi kwenye Gesti ya Makanya, iliyopo Manzese Uzuri, Dar es Salaam.
Mtoa habari wetu alieleza kuwa fumanizi lilifanyika baada ya mume wa Eliza, Hamis Bashaija kuanza kunusa harufu mbaya ya usaliti ndani ya nyumba yake ambapo alisoma dalili na kupata hisia kwamba mkewe anagawa zabibu zake kwa mwanaume mwingine.
Mleta niuzi wetu anaendelea kumwagika kuwa kutokana na kuhisi mke wake anatoka na mwanaume mwingine, alianza kufanya uchunguzi mpaka alipobaini ukweli, hivyo akaandaa mtego wa kumkamata mbogo wake.
Alisema, Hamis na Eliza wanaishi maeneo ya White Inn, Sinza Kijiweni, Dar es Salaam lakini ili kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawia, ilimlazimu mume kupanga safari feki ya kwenda mkoani Singida kwa lengo la kumhadaa mkewe na kumkamata kwa urahisi.
Mnyetishaji wetu aliendelea kusema kuwa Januari 23 mwaka huu (Jumamosi iliyopita) asubuhi, Hamis alimuaga mkewe kwamba anakwenda Singida kikazi na kuacha mahitaji yote muhimu ambapo Eliza alimtakia safari njema.
Ilipofika jioni Hamis alimpigia simu Eliza na kumueleza kuwa amefika Singida, Eliza akampa pole kwa safari, alisema mleta niuz wetu na kuongeza:
Kumbe Hamis alikuwa amejificha mtaa wa pili kutoka nyumbani kwake na alikuwa ameweka mitego kufuatilia nyenndo za mkewe. Aliweka mashushushu ambao muda wote walicheza na safari za Eliza kisha wakawa wanampa taarifa jamaa.
Mleta niuz wetu anaendelea kupayuka; Ilipofika majira ya saa 12:30, mtego ulianza kuonesha matumaini baada ya mashushushu kubaini kwamba Eliza alikuwa anaupara bila kujua anakoelekea.
Alipomaliza kuupara, taratibu kwa mwendo wa kinyonga huku akiikanyaga ardhi kwa kudonyoa kama siyo kunyata, alivuka daraja na kuingia Makanya Guest ambayo ipo jirani kabisa na nyumba anayoishi na mumewe.
Alipofika hapo, Eliza alikutana na njemba aliyenaswa naye, wakatulizana sehemu moja iliyokuwa na mwanga hafifu, hapo wakaanza kunywa mvinyo. Walipokolea kilevi, walikodi chumba namba 26 kwa ajili ya kuichinja amri ya sita.
Wakati hayo yote yanafanyika, kila hatua ilikuwa inafuatiliwa na wapambe wa Hamis na ilipofika hatua ya kuingia chumbani, timu nzima akiwemo Hamis mwenyewe waliizingira Makanya Guest na kuingia chumba husika.
Waliingia chumbani bila kumuuliza mtu, walisukuma mlango kwa nguvu, ukaitika, wakawakuta wote wakiwa wamevaa nguo za ndani, hapo ikawa inaonekana wazi kabisa kuwa walikuwa wakikaribia kuifumua fumua amri ya sita.
Baada ya hapo, ikawa ni piga piga yule jamaa aliyenaswa ugoni alipigwa mno na wapambe wa Hamis ambaye naye alimpa kipigo cha aina yake mke wake na matukio yote hayo yalikuwa yanarekodiwa kwa picha.
Kutokana na kuzidiwa na kipigo, mgoni huyo alichoropoka na kutokomea akiwa na nguo ya ndani, huku nyuma Hamis alimchukua mke hadi nyumbani kwake na muda wote Eliza alikuwa anaomba msamaha kwamba harudii tena.
Risasi lilipopata habari hiyo pamoja na picha, kesho yake (Jumapili), lilituma paparazi wake kwenye gesti hiyo na kuongea na meneja aliyejitambulisha kwa jina la Said Omari, ambaye alikiri tukio hilo kutokea lakini akadai hana maelezo kwa sababu hakuwepo.
SAKATA LINAENDELEA
Mtoa habari wetu alieleza kuwa fumanizi lilifanyika baada ya mume wa Eliza, Hamis Bashaija kuanza kunusa harufu mbaya ya usaliti ndani ya nyumba yake ambapo alisoma dalili na kupata hisia kwamba mkewe anagawa zabibu zake kwa mwanaume mwingine.
Mleta niuzi wetu anaendelea kumwagika kuwa kutokana na kuhisi mke wake anatoka na mwanaume mwingine, alianza kufanya uchunguzi mpaka alipobaini ukweli, hivyo akaandaa mtego wa kumkamata mbogo wake.
Alisema, Hamis na Eliza wanaishi maeneo ya White Inn, Sinza Kijiweni, Dar es Salaam lakini ili kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawia, ilimlazimu mume kupanga safari feki ya kwenda mkoani Singida kwa lengo la kumhadaa mkewe na kumkamata kwa urahisi.
Mnyetishaji wetu aliendelea kusema kuwa Januari 23 mwaka huu (Jumamosi iliyopita) asubuhi, Hamis alimuaga mkewe kwamba anakwenda Singida kikazi na kuacha mahitaji yote muhimu ambapo Eliza alimtakia safari njema.
Ilipofika jioni Hamis alimpigia simu Eliza na kumueleza kuwa amefika Singida, Eliza akampa pole kwa safari, alisema mleta niuz wetu na kuongeza:
Kumbe Hamis alikuwa amejificha mtaa wa pili kutoka nyumbani kwake na alikuwa ameweka mitego kufuatilia nyenndo za mkewe. Aliweka mashushushu ambao muda wote walicheza na safari za Eliza kisha wakawa wanampa taarifa jamaa.
Mleta niuz wetu anaendelea kupayuka; Ilipofika majira ya saa 12:30, mtego ulianza kuonesha matumaini baada ya mashushushu kubaini kwamba Eliza alikuwa anaupara bila kujua anakoelekea.
Alipomaliza kuupara, taratibu kwa mwendo wa kinyonga huku akiikanyaga ardhi kwa kudonyoa kama siyo kunyata, alivuka daraja na kuingia Makanya Guest ambayo ipo jirani kabisa na nyumba anayoishi na mumewe.
Alipofika hapo, Eliza alikutana na njemba aliyenaswa naye, wakatulizana sehemu moja iliyokuwa na mwanga hafifu, hapo wakaanza kunywa mvinyo. Walipokolea kilevi, walikodi chumba namba 26 kwa ajili ya kuichinja amri ya sita.
Wakati hayo yote yanafanyika, kila hatua ilikuwa inafuatiliwa na wapambe wa Hamis na ilipofika hatua ya kuingia chumbani, timu nzima akiwemo Hamis mwenyewe waliizingira Makanya Guest na kuingia chumba husika.
Waliingia chumbani bila kumuuliza mtu, walisukuma mlango kwa nguvu, ukaitika, wakawakuta wote wakiwa wamevaa nguo za ndani, hapo ikawa inaonekana wazi kabisa kuwa walikuwa wakikaribia kuifumua fumua amri ya sita.
Baada ya hapo, ikawa ni piga piga yule jamaa aliyenaswa ugoni alipigwa mno na wapambe wa Hamis ambaye naye alimpa kipigo cha aina yake mke wake na matukio yote hayo yalikuwa yanarekodiwa kwa picha.
Kutokana na kuzidiwa na kipigo, mgoni huyo alichoropoka na kutokomea akiwa na nguo ya ndani, huku nyuma Hamis alimchukua mke hadi nyumbani kwake na muda wote Eliza alikuwa anaomba msamaha kwamba harudii tena.
Risasi lilipopata habari hiyo pamoja na picha, kesho yake (Jumapili), lilituma paparazi wake kwenye gesti hiyo na kuongea na meneja aliyejitambulisha kwa jina la Said Omari, ambaye alikiri tukio hilo kutokea lakini akadai hana maelezo kwa sababu hakuwepo.
SAKATA LINAENDELEA