Kibiti, Pwani: Ujumbe wa kuua polisi zaidi wazidisha hofu

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Siku mbili tangu kuuawa kwa polisi wawili wa Kikosi cha Usalama Barabarani ambao walikuwa kazini katika kijiji cha Bungu B, hali ya wasiwasi imezidi baada ya wauaji hao kusambaza ujumbe unaoeleza kuwa wanaendelea kusaka askari kwa kuwa ni wadhulumaji.

Watu hao wametuma ujumbe mfupi ulioandika kwenye karatasi na kisha kuutuma katika mitandao ya kijamii, ukidai kuwa waliouawa (japo hawajatajwa majina yao) wanadhulumu watu kwa kutumia kazi yao.

"Tunawatangazia wananchi tumewaua hawa kwa sababu wanadhulumu watu kwa kutumia kazi zao na yeyote atakayefanya kazi hapa au nje ya hapa tutamtafuta hadi nyumbani kwake.

Sisi tumejitolea kufa kuliko kuishi, kwa hiyo dereva au raia popote uwaonapo toa taarifa iwe nyumbani au kazini", unasema ujumbe huo.

"Hakuna njia ya kumaliza dhuluma isipokuwa chuma tu, hapa chuma tuuu!"

Ujumbe huo ambao umeandikwa kwa mkono kwa kutumia kalamu ya rangi ya bluu unadaiwa kuwa unazungumzia vifo vya askari polisi wawili wa kituo cha polisi Kibiti, Sajent Salum na PC Masola waliouawa kwa kupigwa risasi wakiwa kazini.

Mmoja wa madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Kibiti) jina tunalo) alisema ujumbe huo unawalenga askari wa kawaida na wa kikosi cha usalama barabarani.

Diwani huyo alisema kundi hilo linalofanya mauaji katika wilaya za Kibiti na Rufiji bado lina nguvu.

"Linaonyesha bado lina uwezo mkubwa wa kufanya mauaji na kutokomea kusikojulikana", alisema

Alisema kwa sasa Serikali inapaswa kuongeza nguvu zaidi ya wapelelezi ili kukomesha kikundi hicho ambacho hakijulikani kinafanya hivyo kwa sababu zipi na wala kinakojificha.

Akizungumza ujumbe huo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga alisema jeshi la polisi litaendelea kuwasaka. "Tutapambana nao tu", alisema Kamanda Lyanga na kukata simu.

Chanzo: Mwananchi
 
Siku mbili tangu kuuawa kwa polisi wawili wa Kikosi cha Usalama Barabarani ambao walikuwa kazini katika kijiji cha Bungu B, hali ya wasiwasi imezidi baada ya wauaji hao kusambaza ujumbe unaoeleza kuwa wanaendelea kusaka askari kwa kuwa ni wadhulumaji.

Watu hao wametuma ujumbe mfupi ulioandika kwenye karatasi na kisha kuutuma katika mitandao ya kijamii, ukidai kuwa waliouawa (japo hawajatajwa majina yao) wanadhulumu watu kwa kutumia kazi yao.

"Tunawatangazia wananchi tumewaua hawa kwa sababu wanadhulumu watu kwa kutumia kazi zao na yeyote atakayefanya kazi hapa au nje ya hapa tutamtafuta hadi nyumbani kwake.

Sisi tumejitolea kufa kuliko kuishi, kwa hiyo dereva au raia popote uwaonapo toa taarifa iwe nyumbani au kazini", unasema ujumbe huo.

"Hakuna njia ya kumaliza dhuluma isipokuwa chuma tu, hapa chuma tuuu!"

Ujumbe huo ambao umeandikwa kwa mkono kwa kutumia kalamu ya rangi ya bluu unadaiwa kuwa unazungumzia vifo vya askari polisi wawili wa kituo cha polisi Kibiti, Sajent Salum na PC Masola waliouawa kwa kupigwa risasi wakiwa kazini.

Mmoja wa madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Kibiti) jina tunalo) alisema ujumbe huo unawalenga askari wa kawaida na wa kikosi cha usalama barabarani.

Diwani huyo alisema kundi hilo linalofanya mauaji katika wilaya za Kibiti na Rufiji bado lina nguvu.

"Linaonyesha bado lina uwezo mkubwa wa kufanya mauaji na kutokomea kusikojulikana", alisema

Alisema kwa sasa Serikali inapaswa kuongeza nguvu zaidi ya wapelelezi ili kukomesha kikundi hicho ambacho hakijulikani kinafanya hivyo kwa sababu zipi na wala kinakojificha.

Akizungumza ujumbe huo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga alisema jeshi la polisi litaendelea kuwasaka. "Tutapambana nao tu", alisema Kamanda Lyanga na kukata simu.

Chanzo: Mwananchi
Nilizungumzia hili kwenye mada yangu hivyo pamoja na kuwasaka wauaji lakini jeshi nalo lijitafakari na kusafisha uozo wote ndani ya jeshi
 
Siku mbili tangu kuuawa kwa polisi wawili wa Kikosi cha Usalama Barabarani ambao walikuwa kazini katika kijiji cha Bungu B, hali ya wasiwasi imezidi baada ya wauaji hao kusambaza ujumbe unaoeleza kuwa wanaendelea kusaka askari kwa kuwa ni wadhulumaji.

Watu hao wametuma ujumbe mfupi ulioandika kwenye karatasi na kisha kuutuma katika mitandao ya kijamii, ukidai kuwa waliouawa (japo hawajatajwa majina yao) wanadhulumu watu kwa kutumia kazi yao.

"Tunawatangazia wananchi tumewaua hawa kwa sababu wanadhulumu watu kwa kutumia kazi zao na yeyote atakayefanya kazi hapa au nje ya hapa tutamtafuta hadi nyumbani kwake.

Sisi tumejitolea kufa kuliko kuishi, kwa hiyo dereva au raia popote uwaonapo toa taarifa iwe nyumbani au kazini", unasema ujumbe huo.

"Hakuna njia ya kumaliza dhuluma isipokuwa chuma tu, hapa chuma tuuu!"

Ujumbe huo ambao umeandikwa kwa mkono kwa kutumia kalamu ya rangi ya bluu unadaiwa kuwa unazungumzia vifo vya askari polisi wawili wa kituo cha polisi Kibiti, Sajent Salum na PC Masola waliouawa kwa kupigwa risasi wakiwa kazini.

Mmoja wa madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Kibiti) jina tunalo) alisema ujumbe huo unawalenga askari wa kawaida na wa kikosi cha usalama barabarani.

Diwani huyo alisema kundi hilo linalofanya mauaji katika wilaya za Kibiti na Rufiji bado lina nguvu.

"Linaonyesha bado lina uwezo mkubwa wa kufanya mauaji na kutokomea kusikojulikana", alisema

Alisema kwa sasa Serikali inapaswa kuongeza nguvu zaidi ya wapelelezi ili kukomesha kikundi hicho ambacho hakijulikani kinafanya hivyo kwa sababu zipi na wala kinakojificha.

Akizungumza ujumbe huo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga alisema jeshi la polisi litaendelea kuwasaka. "Tutapambana nao tu", alisema Kamanda Lyanga na kukata simu.

Chanzo: Mwananchi
Na wasiwasi tunaanza kuona matokeo na matunda ya kuajiri kwa upendeleo wa undugu, ukabila na urafiki. Jeshi la NYERERE halikuwa hivi, Serikali ifanye upya udahili wa viongozi wa jeshi tupate watu wanaoweza kupambana na ujambazi na ugaidi wa karne 21.
 
wanakurupuka na makomando wakati hawajui hata rangi za maadui!
seheme yakufanya angalau upelelezi kwanza kusaidia wataanzia wapi, sasa hao makomando wana mimina risasi hewani sijui
vikundi kama hivi vinaanza vidogo badae wakiwa wengi wataleta shida kubwa sana, mwanzo wa vita vya wenyewe kwa wenyewe..
 
Nilizungumzia hili kwenye mada yangu hivyo pamoja na kuwasaka wauaji lakini jeshi nalo lijitafakari na kusafisha uozo wote ndani ya jeshi
Aanze Siiro!!
Kuna makauli yake flani hivi huwa yanaeleweka kwenye parade peke yake.
 
Aisee!
Hao wauaji wakishamalizana na viongozi,askari na eagambo watarudi kwa raia. Wananchi wa huko toeni ushirikiano kwa jeshi wakamatwe.
 
Nauliza kwa sauti tu,, Na wenyeviti wa vijiji na vitongoji nao wanadhulumu nn!!? Tunatakiwa kuwa makin, wanachofanya wauaji ni kutuaminisha kwamba serikali ni mbaya kwa wananchi ili tu wananchi wasiseme au kutoa taarifa kuwataja popote walipo. Mwisho wa siku wataanza na kundi jingine la kuwalenga hatimae tutabaki kwenye taharuki kubwa jamii nzima hakuna utengamano tena, bali vita ya wenyewe kwa wenyewe na uhasama mkubwa. Ni mwanzo mbaya Sana kwa nchi yetu kwa hayo yanayoendelea kibiti. Kila mwenye akili timamu hawezi kushabikia
 
Back
Top Bottom