Kibano cha Rais Magufuli kwa Tanzanite chang'ata hadi Nje ya Nchi: India yasalimu Amri. Balozi wake atembelea Tume ya Madini.

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
IMG_8800.JPG


Wiki iliyopita Balozi wa India nchini, Sandeep Arya alimtembelea Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Prof. Idris Kikula, jijini Dodoma kwa lengo la kujitambulisha pamoja na kufahamu majukumu ya Tume hiyo.
Hata hivyo, wajuvi wa mambo wanadai kuwa, Ziara hiyo ya Balozi ni matokeo ya kibano cha Tanzania cha kuzuia utoroshwaji wa Tanzanite kupitia magendo kupitia uzio uliojengwa kuzunguka Migodi ya Tanzanite iliyopo Mirerani, Simanjiro Manyara.

Ingawa Tanzania ndiye mzalishaji pekee wa Tanzanite lakini India imekuwa ikiuza sana Tanzanite kutokana na biashara ya magendo. Kufuatia Zuio la Serikali, Ziara ya Balozi ni mkakati sahihi kwao kutazama namna ya kuendelea kufanya biashara katika mazingira mapya ya uwepo wa Tume na udhibiti ulioimarishwa.

IMG_8798.JPG

Masonara wakiwa kazini huko Jaipur, Rajasthan India.

IMG_8793.JPG
 
Noah zetu ziko wapi hasa ya kwangu ile ya pink naitaka huyo nani aliyekwenda chooni mi simjui. Kama mwanaume John Thornton alikuja kwa kichaa wetu kwenye ile jumba jeupe tena akajiffananisha nae kumbe yeye kichaa yaani jiwe likajifananisha na binadamu akasema watatuachia kishika uchumba cha dola mil 300 alafu wakasepa.

Mererani wale wana-apolo walipasua ukuta kwa baruti wakatoroka na tanzanite na hawakuwahi kamatwa mpaka mkapeleka vifaru vya jeshi. Mamaee zenu nyie algae wa kijani msituzuzue twatak noah zetu na balimu zetu huyo aliekwenda kutalii sisi hatuhusu sisi twataka noah na hela zetu
 
Hatuwezi kusubiri Noa bila kuonyesha dunia Kuwa hii mali ni yetu.Hata tukikosa kabisaaa lakini wezi wamejua Kuwa wanaowaibia wamezinduka usingizini.
 
Mzigo wa deni umeifanya ianze kutafuta msaada, kuna uwezekano ikachangia 'share'na kampuni ya Rand-gold Resources Limited kwa uwiano wa 66.6 kwa 33.4. ACACIA wameanza kutapatapa (source: Daily News-25/09/2018 page 19)
 
Mzigo wa deni umeifanya ianze kutafuta msaada, kuna uwezekano ikachangia 'share'na kampuni ya Rand-gold Resources Limited kwa uwiano wa 66.6 kwa 33.4. ACACIA wameanza kutapatapa (source: Daily News-25/09/2018 page 19)

Hiki ulichoongea kinawezekana kina ukweli, lakini uliposema source ya hiyo taarifa yako ni Daily News ndio nimepuuza chochote ulichoandika. Huwezi kuaamini taarifa yoyote inayotoka serekalini kwa sasa inapokuja kwenye mambo haya kwani serekali na vyombo vyake vimeacha weledi na kujikita kwenye propaganda na kupika data.
 
View attachment 877251

Wiki iliyopita Balozi wa India nchini, Sandeep Arya alimtembelea Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Prof. Idris Kikula, jijini Dodoma kwa lengo la kujitambulisha pamoja na kufahamu majukumu ya Tume hiyo.
Hata hivyo, wajuvi wa mambo wanadai kuwa, Ziara hiyo ya Balozi ni matokeo ya kibano cha Tanzania cha kuzuia utoroshwaji wa Tanzanite kupitia magendo kupitia uzio uliojengwa kuzunguka Migodi ya Tanzanite iliyopo Mirerani, Simanjiro Manyara.

Ingawa Tanzania ndiye mzalishaji pekee wa Tanzanite lakini India imekuwa ikiuza sana Tanzanite kutokana na biashara ya magendo. Kufuatia Zuio la Serikali, Ziara ya Balozi ni mkakati sahihi kwao kutazama namna ya kuendelea kufanya biashara katika mazingira mapya ya uwepo wa Tume na udhibiti ulioimarishwa.

View attachment 877250
Masonara wakiwa kazini huko Jaipur, Rajasthan India.

View attachment 877239
Aibu sana hii.Yaani Tanzanite tuzalishe sisi halafu wa export India.Hapa inabidi niwe bold na straight.
Wanaozitetea awamu za tatu na nne kwamba zilifanya vizuri na wanaomsakama Dr Joseph Pombe Magufuli, ni LUNATICS.I am sorry.
 
Mererani wale wana-apolo walipasua ukuta kwa baruti wakatoroka na tanzanite na hawakuwahi kamatwa mpaka mkapeleka vifaru vya jeshi. Mamaee zenu nyie algae wa kijani msituzuzue twatak noah zetu na balimu zetu huyo aliekwenda kutalii sisi hatuhusu sisi twataka noah na hela zetu

Mkuu hili tukio ni la lini??
 
Tungejenga mji wa vito. kama ni Dodoma au Arusha. Hapo tuuze Ruby, Almasi, dhahabu, Tanzanite, saphire etc. Nchi nyingi unakuta kuna miji na mitaa ambayo iko special kwa kuuza na kukata madini ya vito.
 
Back
Top Bottom