Kibali cha Polisi Kuandamana.

Diana-DaboDiff

JF-Expert Member
Jul 13, 2009
376
19
Kwenye miaka ya tisini baada ya tume ya Nyalali kurekebisha sheria kipengele cha kuomba kibali polisi kilifutwa na tukaambiwa mkitaka kuandamana munawajulisha polisi watoe ulinzi. Kuna nyimbo ya Bob Mapesa wa Kenya anauliza kila mara 'tuko mbele au tuko nyuma' mpenzi wake anajibu tuko mbele,sio nia yangu kuongelea wimbo huu lakini nauliza pia 'tunaenda mbele au nyuma' ?
Miaka ya hivi karibuni naona kile kipengele cha kuomba kibali polisi kimerudi kinyemela utasikia polisi wamezuia kundi flani kuandamana.Naomba wanasheria humu ndani watujulishe ni vipi tunaomba kibali au tunawajulisha polisi tukitaka kuandamana ?
 
polisi wa hii nchi ndugu yangu wapo kimaslahi zaidi,ukiwa na mkwanja utaandamana mpaka uchoke ila kama ni chaka chinu we utakuwa ni mtu wa kulalamika daima,wanazijuwa sheria ila ni makaidi sana,hakuna kilichobadilika kila kitu kipo wazi,hata wanapoongelea kuwa nchi haipo ktk mstabari wa mzuri wa amani wana juwa kuwa Raisi ndiye mwenye mamlaka ya kutangaza hali ya hatari,ila wao wanatumia kigezo hicho pasipo hata Raisi kutangaza

Ila ndio polisi wetu walivyo(walitowa kibali kwa makongoro mahanga kuhutubia wapiga kura-wakamnyima mpendazoe) sasa haki ipo wapi?


mapinduziiii daimaaaaa
 
haaaa, hawa polisi jamani

Hivi tanzania tunao polisi kweli( in the real sense of the word), Au watu wanaovaa uniform za polisi?

Kuna kamjamaa kalishikwa live na mabox yenye kura nje ya kituo cha kuhesabia kura, akapelekwa polisi mpaka leo polisi hawajazungumzia ni vipi jamani, angalia kifungu 91 (1)(h) cha sheria ya uchaguzi sura 343 kama ilivyorekebishwa Juni 2010. Wala hawajamfikisha mahakamani.

Waandishi mbona hawafuatilii hii kitu?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom