Kibali cha Kimataifa cha Kuendesha Gari, Tanzania

wehoodie

JF-Expert Member
Nov 20, 2011
1,021
992
Wakuu

Naomba msaada wa kimaelekezo namna ya kupata International Driving Permit (IDP) kutoka hawajamaa wa AAT ambao naamini ndio issuing authority Tanzania. Zaidi ningependa kupata mtu aliepata anipe uzoefu wake, je yawezekana kuipata bila muhitaji kufika physically kwa hawajamaa naaminisha kwa kutumia mtu n.k.

Hivi kwa nini Taasisi kama hizi hawana hata website?

Note. Muhitaji wa IDP anayo leseni yakwaida (zile mpya) inayotolewa na TRA.

Shukrani!
Leseni ya kimataifa
UTARATIBU WA KUPATA &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; INTERNATIONAL DRIVING PERMIT


HAPA NCHINI.

  • Mwombaji anatakiwa kuwa na leseni ya Udereva ya daraja lolote lile iliyo hai ya hapa Nchini.
  • Anatakiwa kuipeleka leseni yake ofisi ya Mamlaka ya Leseni (T) TRA kwa ajili ya ukaguzi,
  • Baada ya Ukaguzi, Mamlaka ya Leseni (T) TRA itatoa barua rasmi kwenda kwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani(T) kuthibitisha uhalali wa leseni hiyo.
  • Ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) itakagua leseni hiyo pamoja na cheti cha Umahiri (Certificate of Competence) kuthibitisha uhalali wa leseni na cheti hicho cha umahiri.
  • Baada ya kuthibitisha uhalali wa leseni hiyo, Ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) itatoa barua rasmi kwenda Oisi ya Automobile Association Tanzania ambayo ndiyo asasi pekee hapa nchini yenye Mamlaka ya kutoa leseni za Kimataifa.
 
Leseni ya kimataifa
UTARATIBU WA KUPATA – INTERNATIONAL DRIVING PERMIT
HAPA NCHINI.
  • Mwombaji anatakiwa kuwa na leseni ya Udereva ya daraja lolote lile iliyo hai ya hapa Nchini.
  • Anatakiwa kuipeleka leseni yake ofisi ya Mamlaka ya Leseni (T) TRA kwa ajili ya ukaguzi,
  • Baada ya Ukaguzi, Mamlaka ya Leseni (T) TRA itatoa barua rasmi kwenda kwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani(T) kuthibitisha uhalali wa leseni hiyo.
  • Ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) itakagua leseni hiyo pamoja na cheti cha Umahiri (Certificate of Competence) kuthibitisha uhalali wa leseni na cheti hicho cha umahiri.
  • Baada ya kuthibitisha uhalali wa leseni hiyo, Ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (T) itatoa barua rasmi kwenda Oisi ya Automobile Association Tanzania ambayo ndiyo asasi pekee hapa nchini yenye Mamlaka ya kutoa leseni za Kimataifa.
 
Na kama mimi ni mtanzania ambae nilichukua leseni tokea muda ambao certificate of compatence hazijaanza kutumika kama ni kielelezo cha uhalali wa udereva nitawezaje kupata hiyo international driving permit?
Naombeni msaada wa kuelewa hilo wadau wezangu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom