beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Mtoto wa kike mwenye miaka 14 mwanafunzi wa darasa la saba Shule ya Msingi Mtongani amejinyonga hadi kufa nyumbani kwao Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani baada ya mama yake mzazi kumtuhumu kuiba Sh5,000.
Akizungumza leo Jumatano Mei 26, 2021 Kamanda wa polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa amesema tukio hilo limetokea juzi Jumatatu Mei 24, 2021 na uchunguzi ulipofanyika ilibainika chanzo cha kifo kutuhumiwa kuiba kiasi hicho cha fedha.
"Ni kweli tukio hili limetokea lakini sisi Jeshi la polisi tulipofanya uchunguzi wetu tukabaini huyu mtoto aliamua kujitoa roho kwa sababu mama yake mzazi, Ashura Selemani alimtuhumu kumuibia pesa ambayo ilikuwa ya mama huyo.”
“Tunamshikilia mama huyo pamoja na baba mlezi (jina linahifadhiwa) kwa mahojiano zaidi,” amesema.
Chanzo: Mwananchi
Akizungumza leo Jumatano Mei 26, 2021 Kamanda wa polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa amesema tukio hilo limetokea juzi Jumatatu Mei 24, 2021 na uchunguzi ulipofanyika ilibainika chanzo cha kifo kutuhumiwa kuiba kiasi hicho cha fedha.
"Ni kweli tukio hili limetokea lakini sisi Jeshi la polisi tulipofanya uchunguzi wetu tukabaini huyu mtoto aliamua kujitoa roho kwa sababu mama yake mzazi, Ashura Selemani alimtuhumu kumuibia pesa ambayo ilikuwa ya mama huyo.”
“Tunamshikilia mama huyo pamoja na baba mlezi (jina linahifadhiwa) kwa mahojiano zaidi,” amesema.
Chanzo: Mwananchi