2mbaku
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 316
- 67
Kwanza inua mkono wako wa kulia ulishwe kiapo kwamba unakubali kwa yakini:
1.Kwamba sikuzote utafanya kazi ya udaktari kwa ujuzi na uwezo wako wote kwa ajili ya mema, afya na usalama wa watu wote watakaofika mbele yako kwa nia ya matibabu.
2.Kwamba hutafanya kwa makusudi wala kwa nia kitu chochote au kuwapa kitu chochote cha kuwadhuru au cha kuwaondolea heshima.
3.kwamba hutatoa siri yoyote imhusuyo mgonjwa uliyosikia au kuigundua katika uwezo wako wa udaktari kazini bila sababu rasmi.
4.Kwamba hutatumia njia za siri za matibabu wala kuwaficha madaktari wenzio namna yoyote ya matibabu utakayogundua kuwa ni matibabu safi.
5.Kwamba hutajitangaza wala hutakubali utangazwe kwa nia ya kujivutia wagonjwa.
6.Kwamba katika uhusiano wako na madaktari wenzio siku zote utajiweka katika mwenendo safi wa heshima kama inavyotakiwa na umoja wa kazi muhimu ya udaktari.
Basi ukitimiza hivyo, Mungu pamoja na Umma watakutukuza.
Hebu tujadili kiapo hiki bila ushabiki, hasa kifungu cha 1,2 na 6. Je katika vifungu hivyo, kuna chochote kinamzuia daktari kugoma directly au indirectly?
Vipi kuhusu umoja wa madaktari, je kifungu cha 6 hakiwahukumu wale wote ambao waliwasaliti wenzao na kuendelea na kazi?
Nawasilisha>>>>
1.Kwamba sikuzote utafanya kazi ya udaktari kwa ujuzi na uwezo wako wote kwa ajili ya mema, afya na usalama wa watu wote watakaofika mbele yako kwa nia ya matibabu.
2.Kwamba hutafanya kwa makusudi wala kwa nia kitu chochote au kuwapa kitu chochote cha kuwadhuru au cha kuwaondolea heshima.
3.kwamba hutatoa siri yoyote imhusuyo mgonjwa uliyosikia au kuigundua katika uwezo wako wa udaktari kazini bila sababu rasmi.
4.Kwamba hutatumia njia za siri za matibabu wala kuwaficha madaktari wenzio namna yoyote ya matibabu utakayogundua kuwa ni matibabu safi.
5.Kwamba hutajitangaza wala hutakubali utangazwe kwa nia ya kujivutia wagonjwa.
6.Kwamba katika uhusiano wako na madaktari wenzio siku zote utajiweka katika mwenendo safi wa heshima kama inavyotakiwa na umoja wa kazi muhimu ya udaktari.
Basi ukitimiza hivyo, Mungu pamoja na Umma watakutukuza.
Hebu tujadili kiapo hiki bila ushabiki, hasa kifungu cha 1,2 na 6. Je katika vifungu hivyo, kuna chochote kinamzuia daktari kugoma directly au indirectly?
Vipi kuhusu umoja wa madaktari, je kifungu cha 6 hakiwahukumu wale wote ambao waliwasaliti wenzao na kuendelea na kazi?
Nawasilisha>>>>