Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
POSHO za vikao ambazo mjadala wake umechukua takriban mwaka mmoja sasa, huenda zikafikia ukomo mwaka huu kutokana na kuwapo kwa taarifa kwamba wabunge wamepania kuzifuta katika Bajeti ya mwaka ujao wa fedha.
Habari ambazo zimelifikia gazeti hili kutoka bungeni na serikalini zinasema Tume ya Huduma za Bunge tayari imeanza kujadili suala hilo na kwamba uamuzi ni kuanza kufuta posho za vikao kwa wabunge ambazo ni Sh70,000 kwa siku.
Taarifa za kuwapo kwa mpango huo zimekuja siku chache tangu Rais Jakaya Kikwete alipokataa kuidhinisha mapendekezo mapya ya posho za vikao kwa wabunge kutoka kiasi hicho cha Sh70,000 hadi Sh200,000 kwa siku.
Ikiwa uamuzi huo utatekelezwa, utakuwa ni ushindi kwa wabunge ambao waliasisi vita dhidi ya posho za vikao kiasi cha kusababisha tofauti za wazi na wabunge wenzao ambao wamekuwa wakiwatuhumu kwamba wanatafuta umaarufu wa kisiasa.
Miongoni mwa wabunge hao ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, January Makamba na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe.
Mwingine ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ambaye aliwahi kuziita posho za vikao kuwa ni wizi wa kitaasisi ulioasisiwa hali ukiwa hauna tija kwa Taifa na badala yake kupoteza fedha nyingi za Serikali.
Mmoja wa viongozi waandamizi wa Bunge ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alisema suala la wabunge kufuta posho za vikao tayari limeanza kujadiliwa na Tume ya Huduma za Bunge ambayo Mwenyekiti wake ni Spika Anne Makinda. Kuanzia mwaka ujao wa fedha tunataka kuacha kabisa kulipwa posho za vikao (sitting allowance), kwa hiyo hata hiyo Sh70,000 hatutachukua itakuwa ni ziro kabisa maana tumechoka kuandamwa, alisema kiongozi huyo na kuongeza: Lakini wakati tukifanya uamuzi huo, serikalini, mahakamani na katika mashirika mengine ya umma nako wajiandae, hakuna bajeti yoyote ya posho za vikao itakayopitishwa na hili tutaanza kuwapa maelekezo rasmi wakati wa vikao vya mipango ya bajeti mwezi Aprili mwaka huu.
Spika wa Bunge, Makinda alipotafutwa juzi na jana kuzungumzia taarifa za taasisi yake kuweka mkakati wa kufuta posho hizo, simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita kwa muda mrefu bila majibu.
Kwa upande wake Naibu Spika, Job Ndugai alipoulizwa iwapo kuna mpango wa wabunge kusimamia kufutwa kwa posho zote za vikao ndani ya Bunge, serikalini na katika Idara ya Mahakama hakukanusha wala kuthibitisha suala hilo, badala yake akashauri kwamba: usubiriwe wakati mwafaka.
Alipoulizwa wakati mwafaka ni upi alisema: Mimi nadhani suala la posho linachosha, hakuna jambo jingine la kuzungumza ina maana ni posho tu? Tumesema sana kama ni kuhusu kufutwa basi mimi nadhani tusubiri wakati mwafaka, wakati wa bajeti maana mchakato wake unaanza Aprili, tusubiri tutapata majibu mwafaka, alisema Ndugai ambaye amekuwa msemaji wa suala hilo kwa muda mrefu sasa.
Habari ambazo zimelifikia gazeti hili kutoka bungeni na serikalini zinasema Tume ya Huduma za Bunge tayari imeanza kujadili suala hilo na kwamba uamuzi ni kuanza kufuta posho za vikao kwa wabunge ambazo ni Sh70,000 kwa siku.
Taarifa za kuwapo kwa mpango huo zimekuja siku chache tangu Rais Jakaya Kikwete alipokataa kuidhinisha mapendekezo mapya ya posho za vikao kwa wabunge kutoka kiasi hicho cha Sh70,000 hadi Sh200,000 kwa siku.
Ikiwa uamuzi huo utatekelezwa, utakuwa ni ushindi kwa wabunge ambao waliasisi vita dhidi ya posho za vikao kiasi cha kusababisha tofauti za wazi na wabunge wenzao ambao wamekuwa wakiwatuhumu kwamba wanatafuta umaarufu wa kisiasa.
Miongoni mwa wabunge hao ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, January Makamba na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe.
Mwingine ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe ambaye aliwahi kuziita posho za vikao kuwa ni wizi wa kitaasisi ulioasisiwa hali ukiwa hauna tija kwa Taifa na badala yake kupoteza fedha nyingi za Serikali.
Mmoja wa viongozi waandamizi wa Bunge ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alisema suala la wabunge kufuta posho za vikao tayari limeanza kujadiliwa na Tume ya Huduma za Bunge ambayo Mwenyekiti wake ni Spika Anne Makinda. Kuanzia mwaka ujao wa fedha tunataka kuacha kabisa kulipwa posho za vikao (sitting allowance), kwa hiyo hata hiyo Sh70,000 hatutachukua itakuwa ni ziro kabisa maana tumechoka kuandamwa, alisema kiongozi huyo na kuongeza: Lakini wakati tukifanya uamuzi huo, serikalini, mahakamani na katika mashirika mengine ya umma nako wajiandae, hakuna bajeti yoyote ya posho za vikao itakayopitishwa na hili tutaanza kuwapa maelekezo rasmi wakati wa vikao vya mipango ya bajeti mwezi Aprili mwaka huu.
Spika wa Bunge, Makinda alipotafutwa juzi na jana kuzungumzia taarifa za taasisi yake kuweka mkakati wa kufuta posho hizo, simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita kwa muda mrefu bila majibu.
Kwa upande wake Naibu Spika, Job Ndugai alipoulizwa iwapo kuna mpango wa wabunge kusimamia kufutwa kwa posho zote za vikao ndani ya Bunge, serikalini na katika Idara ya Mahakama hakukanusha wala kuthibitisha suala hilo, badala yake akashauri kwamba: usubiriwe wakati mwafaka.
Alipoulizwa wakati mwafaka ni upi alisema: Mimi nadhani suala la posho linachosha, hakuna jambo jingine la kuzungumza ina maana ni posho tu? Tumesema sana kama ni kuhusu kufutwa basi mimi nadhani tusubiri wakati mwafaka, wakati wa bajeti maana mchakato wake unaanza Aprili, tusubiri tutapata majibu mwafaka, alisema Ndugai ambaye amekuwa msemaji wa suala hilo kwa muda mrefu sasa.