Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,192
- 25,493
Nimesoma humu JF kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James ameomba radhi kwa mambo yaliyofanywa na kuomba 'maridhiano' ya kitaifa ili tusonge mbele pamoja chini ya Rais wetu mpendwa Mama Samia Suluhu Hassan.
Nikasoma tena humuhumu kuwa Kheri James huyohuyo amesema kuwa msamaha aliouomba ni wake binafsi na si wa UVCCM kama taasisi.
Kuomba radhi ni jambo la kiungwana na kuungwa mkono. Kuomba radhi hufuatiwa na kukubaliwa au kukataliwa kwa radhi husika. Lakini, radhi lazima ianike mambo mahsusi yahusuyo radhi hiyo.
Kwa waliomsikia Kheri James akizungumza au kusoma andiko lake halisi, ameainisha mambo gani hasa aliyoyaombea radhi? Mabaya/makosa/maovu gani ambayo ameyaombea radhi?
Nikasoma tena humuhumu kuwa Kheri James huyohuyo amesema kuwa msamaha aliouomba ni wake binafsi na si wa UVCCM kama taasisi.
Kuomba radhi ni jambo la kiungwana na kuungwa mkono. Kuomba radhi hufuatiwa na kukubaliwa au kukataliwa kwa radhi husika. Lakini, radhi lazima ianike mambo mahsusi yahusuyo radhi hiyo.
Kwa waliomsikia Kheri James akizungumza au kusoma andiko lake halisi, ameainisha mambo gani hasa aliyoyaombea radhi? Mabaya/makosa/maovu gani ambayo ameyaombea radhi?