Kesi za barabarani; Trafiki bongo wamepewa mamlaka makubwa mno wakiamua wanaweza hata kukutandika makofi na usiwafanye kitu kama huna ushahidi

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,276
21,395
Kuna watu mtaniuliza ni sheria gani inaruhusu hilo?

Na Mimi nawajibu kwa maswali;
  • Polisi Traffic akishachukua leseni yako anaamua kukugandisha makusudi pembeni ya barabara saa nzima huwa anatumia sheria gani?
  • Polisi Trafiki anapochomoa funguo wa Gari yako wakati wa mazungumzo na kuizuia hadi umlambe miguu ndipo akupe huwa anatumia sheria gani?
UKAMATAJI WA MAKOSA

Katika ofisi za Umma kuna msemo uko hivi; Mteja (customer) hadanganyi,

Ikiwa na maana kwamba mteja akikushitaki kwa bosi wako ni rahisi sana wewe kutumbuliwa kwasababu Mteja husikilizwa!

Upande wa Traffic case hilo lipo kinyume, Huku Polisi traffic ndiyo husikilizwa kwanza na hakosei,
  1. Mkipelekana kwa in charge wake anaesikilizwa kwanza ni yeye siyo wewe uliyekamatwa.
  2. Akikupeleka kituoni unawezwa lazwa ndani halafu ukasiilizwa kesho yake na hakuna wa kuhoji!
Uhalali wa Makosa ya kuviziana;

Kuna makosa ya wazi hayo Yanaeleweka!

Shida ipo kwenye Makosa haya ya kuviziana!
Mfano;
  • Dreva anaefika kwenye taa ambapo concentration yake iko kwenye taa (ikitokea bahati mbaya kukawa na trafiki anaongoza Gari mathalani alifunikwa na Gari ukashindwa kumuona), Vile taa ya kijani ikaruhusu ukapita halafu mbele wakudake! Hawatakuwa na simile na wewe utahesabika umezarau Alama za barabarani (KOSA) n.k
  • Ukisimamishwa halafu ukaenda simama mita 50m mbele mathalani ulikuwa speed au kwa kutazama sehemu nzuri ya kusimama, Hapo wakiamua kukushikilia kwa kosa la kuwakimbia traffic bado hakuna ataekusikiliza wakiamua hata ndani rupango unalala! na huwafanyi lolote;
Kwa mazingira kama hayo; Polisi trafiki bongo wanao uwezo hata wa kukuchapa makofi na wakasikilizwa wao kwanza kama hakuna ushahidi, tena na rupango waweza lala kusubili kupelekwa mahakaman!

Hivi kwa mazingira kama hayo Mimi mwanachi Naachaje Kutoa Rushwa ili Nisipotezewe Mda wangu Bure?
 
Du..
3946A007-6CAA-41BC-AD87-3399B3BAD5BC.jpeg
 
Juzi wiki iliyopita nilikuwa naendesha kufika Manzese gari lazima ghafla wakati inatembea nitajitahidi mwa mwendo nilivyokuwa nayo nikaoegesha upande wa kushoto wa Barbara, akashuka jamaa aliyekuwa upande wa kushoto kuweka terminal vizuri ili niwashe nitembee, cha rajabu alitoka askari wa kike ambaye alichukua leni yangu akaingangania kwa dakika kama 20 hivi akidai nilikuwa nashusha abiria mbele yake, hakika nilishuhudia uonevu wa traffic live siku hiyo.
 
Juzi wiki iliyopita nilikuwa naendesha kufika Manzese gari lazima ghafla wakati inatembea nitajitahidi mwa mwendo nilivyokuwa nayo nikaoegesha upande wa kushoto wa Barbara, akashuka jamaa aliyekuwa upande wa kushoto kuweka terminal vizuri ili niwashe nitembee, cha rajabu alitoka askari wa kike ambaye alichukua leni yangu akaingangania kwa dakika kama 20 hivi akidai nilikuwa nashusha abiria mbele yake, hakika nilishuhudia uonevu wa traffic live siku hiyo.
pole sana ! vipi lakini huyo askari arikurudishia Leni yako?
 
Back
Top Bottom