Mh. Rais kauli yako kuhusu majambazi tumeisikia, lakini Mh. Ningependa kukumbusha kuhusu wafanyabiashara wa mahenge waliosemekana majambazi wakapigwa risasi na kuuwawa.
Naamini kipindi hicho ulikuwa waziri wa ujenzi na hawa wafanyabiashara walikuwa wamekuja Dar es Salaam wakiwa na madini yao, waliishia kupigwa risasi na askari wakisemekana ni majambazi. Hili suala lilienda mahakamani na nashukuru Mh. Kikwete hakuta kufunika kombe mpaka mahakama ilipomtia hatiani Bageni (OCD) kinondoni kunyongwa.
Mh. Majambazi ni watu hatari na kama jamii tungependa kusiwepo na watu wa aina hii lakini ni muhimu kujihakikishia kila jambazi anayeuwawa ni jambazi kweli? Isiwe tiketi ya kuuwa raia wasiokuwa na makosa na kuporwa mali zao kisha wakasemwa ni majambazi.
IGP naomba katika utendaji wenu mzingatie ukweli na sio kutokea matukio ya kudhurumu raia na kuwabambikizia kesi za ujambazi, mwisho wa siku tutajibu kwa mola.
Natanguliza shukrani.
Naamini kipindi hicho ulikuwa waziri wa ujenzi na hawa wafanyabiashara walikuwa wamekuja Dar es Salaam wakiwa na madini yao, waliishia kupigwa risasi na askari wakisemekana ni majambazi. Hili suala lilienda mahakamani na nashukuru Mh. Kikwete hakuta kufunika kombe mpaka mahakama ilipomtia hatiani Bageni (OCD) kinondoni kunyongwa.
Mh. Majambazi ni watu hatari na kama jamii tungependa kusiwepo na watu wa aina hii lakini ni muhimu kujihakikishia kila jambazi anayeuwawa ni jambazi kweli? Isiwe tiketi ya kuuwa raia wasiokuwa na makosa na kuporwa mali zao kisha wakasemwa ni majambazi.
IGP naomba katika utendaji wenu mzingatie ukweli na sio kutokea matukio ya kudhurumu raia na kuwabambikizia kesi za ujambazi, mwisho wa siku tutajibu kwa mola.
Natanguliza shukrani.