Kesi ya wabunge kutoka CHADEMA, Mdee na Bulaya yatupiliwa mbali

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, imetupilia mbali maombi ya kupinga kusimamishwa kutohudhuria vikao vya bunge wabunge wawili wa Chadema, Halima Mdee (Kawe) na Esther Bulaya(Bunda).

Sababu kutupwa maombi yao zimetajwa ni kanuni za kudumu za Bunge kupingana na Katiba, jambo ambalo Mahakama hiyo ilisema kesi za kikatiba zina taratibu zake.

Kesi hiyo ilisikilizwa jana mahakamani hapo na Jaji Hamisa Kalombola huku kina Mdee na Bulaya wakiwakilishwa na wakili wao, Fredy Kalonga na upande wa serikali ukiwakilishwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Angaza Mwipopo.

Pamoja na kutupiliwa mbali maombi hayo, Jaji Kalombola alisema Mahakama hiyo ina uwezo wa kuhoji kinachofanyika bungeni.

Kwa upande wa Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, ambaye aliweka kusudio la kufungua kesi ya kudhalilishwa na askari wa Bunge, Mahakama hiyo haijamruhusu kufungua kesi kwa maelezo kuwa hajafuata taratibu za ndani za Bunge za kupinga maamuzi yaliyotolewa na Spika Job Ndugai.

Mahakama hiyo pia ilisema kiapo cha mwombaji kilikuwa na mapungufu kwa kuunganisha hoja za kisheria na kuongelea mwenendo wa Bunge bila kufuata taratibu za Bunge jambo ambalo ni kinyume cha Sheria ya Kinga, Maadili na Mamlaka ya Bunge kifungu namba 21.

Juni 5, mwaka huu Bunge liliazimia kuwafungia kutohudhuria mikutano mitatu ya Bunge Mdee na Bulaya kwa kudharau Mamlaka ya Spika.

Kwa upande wake, Mnyika akipewa adhabu na Spika Ndugai ya kutohudhuria kwa siku saba kwa kosa la kufanya fujo bungeni.

Tujikumbushe alichokisema Tundu Lissu kabla hajapeleka kesi mahakamani.

 
Huwezi kumuona Tundu Lissu na jopo lake la mawakili wakileta mrejesho wa kilichotokea mahakamani pamoja na kuwaaminisha baadhi ya watu kuwa wanakwenda ‘’kumshughulikia Spika’’.

Hata kwenye kesi ya Mbowe kuhusu kuwashitaki Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Kanda maalumu ya Dar es Salaam, Simon Siro hawakuleta mrejesho baada ya kugaragazwa mahakamani.

Thread ya kilichotokea mahakamani kuhusu kesi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam gonga hii link;

LINK>>Mbowe agonga mwamba kortini, hata TLS watagonga mwamba

Wengine tulijua mapema kuwa kesi wameishashindwa kabla hata ya kuzifungua na nilisema kwenye thread hii;

LINK>>Mbowe ameshindwa kesi kabla hata haijaanza

Nilipoyasikia maelezo ya Tundu Lissu nilijua anapiga ''soga la kisiasa'' ili kuwafurahisha wafuasi wake ambao wengi wao hawajui hata mantiki kisheria ya kile anachokiongea.

Hii ndio faida ya kuwa na wanasiasa ambao wanatumia ujinga wa baadhi ya wafuasi wao ili kubakia katika uwanja wa kisiasa!

Sheria hazina siasa!

Kinachoshangaza na kuchekesha zaidi, Tundu Lissu anataka mahakama ingilie maamuzi ya bunge halafu hapo hapo hataki bunge liwe dhaifu. Hajui kama mahakama kuingilia maamuzi ya bunge ni kulidhaifisha bunge.
 
Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, imetupilia mbali maombi ya kupinga kusimamishwa kutohudhuria vikao vya bunge wabunge wawili wa Chadema, Halima Mdee (Kawe) na Esther Bulaya(Bunda).

Sababu kutupwa maombi yao zimetajwa ni kanuni za kudumu za Bunge kupingana na Katiba, jambo ambalo Mahakama hiyo ilisema kesi za kikatiba zina taratibu zake.

Kesi hiyo ilisikilizwa jana mahakamani hapo na Jaji Hamisa Kalombola huku kina Mdee na Bulaya wakiwakilishwa na wakili wao, Fredy Kalonga na upande wa serikali ukiwakilishwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Angaza Mwipopo.

Pamoja na kutupiliwa mbali maombi hayo, Jaji Kalombola alisema Mahakama hiyo ina uwezo wa kuhoji kinachofanyika bungeni.

Kwa upande wa Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, ambaye aliweka kusudio la kufungua kesi ya kudhalilishwa na askari wa Bunge, Mahakama hiyo haijamruhusu kufungua kesi kwa maelezo kuwa hajafuata taratibu za ndani za Bunge za kupinga maamuzi yaliyotolewa na Spika Job Ndugai.

Mahakama hiyo pia ilisema kiapo cha mwombaji kilikuwa na mapungufu kwa kuunganisha hoja za kisheria na kuongelea mwenendo wa Bunge bila kufuata taratibu za Bunge jambo ambalo ni kinyume cha Sheria ya Kinga, Maadili na Mamlaka ya Bunge kifungu namba 21.

Juni 5, mwaka huu Bunge liliazimia kuwafungia kutohudhuria mikutano mitatu ya Bunge Mdee na Bulaya kwa kudharau Mamlaka ya Spika.

Kwa upande wake, Mnyika akipewa adhabu na Spika Ndugai ya kutohudhuria kwa siku saba kwa kosa la kufanya fujo bungeni.

Tujikumbushe alichokisema Tundu Lissu kabla hajapeleka kesi mahakamani.


Ngoja waje wale nyumbu utasikia leo mahakama haijawahi tenda haki.
 
Kumbe ina uwezo wa kuhoji kinachoendelea Bungeni!!
Hoja sio mahakama kuhoji bali ni nini kinachohojiwa na mahakama.

Mahakama haina uwezo wa kuhoji maamuzi ya bunge kama ambavyo serikali haina uwezo wa kuhoji maamuzi ya mahakama.
 
mahakama hii hii yenye kaimu jaji mkuu ndo iliyomuachia huru lijua likali..

mahakama hii hii ndo ilimuachia kwa dhamana mh lema baada ya figisu za wakili wa serikali kugonga mwamba.
Una uhakika? ujue kabla ya hapo tamko la mwenye nyumba la kuwashughulikia lilikuwa halijatoka.
 
Nilisema hapa habari za Bunge kuzipeleka Mahakamani zina mlolongo mrefu wa kuhakikisha kinga za kibunge hazivunjwi.

Inaelekea kuna watu wamo Bungeni ama hawajui hili, ama wanalidharau wakifikiri Mahakama itaparamia mambo kwa pupa za kisiasa.

Mahakama za Tanzania zimeonyesha ukomavu kwa kutotaka kujiingiza kwenye kesi za Bunge kiholela.

Hilo lingeleta precedent mbaya ya kuvunja katiba na utawala wa sheria unaoheshimu kutoingiliana kwa mihimili mitatu ya nchi.
 
MsemajiUkweli tunashukuru kwa mrejesho. Maelezo ya Mahakama uliyoyaleta hayaoneshi kwamba Ester Bulaya na Mwenzake Halima Mdee wameshindwa kesi bali walikosea mahali pa kufungulia kesi yao na pia kiufundi (Technicalities) hawakufuata kanuni za ufunguaji wa kesi yenyewe.

Ushindi mkubwa hapo ni pale mahakama inaposema inayo mamlaka ya kisheria kuhoji kinachofanyika bungeni ikiwa ni kinyume na mtizamo wa Job Ndugai Spika wa Bunge kuwa bunge haliwezi kuhojika kwa maamuzi yake kwingine kokote kule.

Halafu si Lissu aliyefungua kesi bali ni Halima Mdee na Ester Bulaya. Lissu si muathirika bali hao wawili.
 
Back
Top Bottom