Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,343
- 217,371
Taarifa kutoka Mahakama ya Kisutu inaeleza kwamba Ile kesi ya unyang'anyi wa Gari la kisasa la Range Rover , mali ya Pedeshee Patrick Christopher Kamwelwe , inayowakabili Paulo Makonda na William Malecela ama Le Mutuz Nation , Imetajwa Mahakamani leo tarehe 13/10/2022 .
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imetoa siku 14 kwa upande wa mdaiwa Paul Makonda, ambaye amewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuwasilisha utetezi wake katika shauri la tuhuma za uporaji wa gari mali ya mlalamikaji Patrick Christopher Kamwelwe anadai kuporwa gari hilo aina ya Range Rover.
Leo Alhamisi Oktoba 13, 2022, Hakimu wa mahakama hiyo Richard Kabate ametoa siku 14 kwa upande wa mdaiwa kuwasilisha utetezi wake. Hata hivyo, Makonda hakuwepo mahakamani hapo na aliwakilishwa na wakili wake, Chima Andrew
Chanzo : Mwananchi .
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imetoa siku 14 kwa upande wa mdaiwa Paul Makonda, ambaye amewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuwasilisha utetezi wake katika shauri la tuhuma za uporaji wa gari mali ya mlalamikaji Patrick Christopher Kamwelwe anadai kuporwa gari hilo aina ya Range Rover.
Leo Alhamisi Oktoba 13, 2022, Hakimu wa mahakama hiyo Richard Kabate ametoa siku 14 kwa upande wa mdaiwa kuwasilisha utetezi wake. Hata hivyo, Makonda hakuwepo mahakamani hapo na aliwakilishwa na wakili wake, Chima Andrew
Chanzo : Mwananchi .