Kesi ya uhujumu uchumi: Kitilya na wenzake wapokea awamu ya kwanza ya vielelezo kutoka Uingereza

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,252
SINARE.jpg

Upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Kamishna Mkuu Mstaafu wa TRA, Harry Kitilya na wenzake umeieleza mahakama kuwa wamepokea awamu ya kwanza ya vielelezo kutoka nchini Uingereza.

Hayo yameelezwa Leo na wakili wa Serikali, Christopher Msigwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa.

Msigwa ameiambia mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa wanatarajia awamu ya pili ya vielelezo kuwasili nchini Tanzania wakati wowote kuanzia sasa.

Hata hivyo wakili wa utetezi, Mwanahamisi Adam ameuomba upande wa mashtaka kueleza muda muafaka ambao utatumika kwa vielelezo hivyo kufika nchini.

Aidha Hakimu Mkeha amewaambia upande wa mashtaka huo muda wowote wanaoutaja wahakikishe unaangukia ndani ya siku 14 na ikishindikana basi Juni 30 mwaka huu waeleze vielelezo hivyo vitafika ndani ya siku ngapi.

Miezi miwili iliyopita upande wa mashtaka uliieleza mahakama kuwa upalelezi dhidi ya kesi hiyo uliokuwa unafanywa ndani ya nchi umekamilika na kuwa bado wanasubiri upepelelezi unaofanywa nje ya nchi.

Mbali na Kitilya washtakiwa wengine ni Miss Tanzania, 1996, Shose Sinare na Sioi Graham Solomon.Wanadaiwa kutenda makosa nane likiwemo la utakatishaji wa fedha wa kiasi cha USD milioni sita.

Mbali na shtaka la utakatishaji wa fedha, watuhumiwa hao wanakabiliwa na tuhuma za kula njama, kutoa nyaraka za uongo na kughushi.

Wanadaiwa kutenda makosa hayo katika tarehe tofauti kati ya Machi2013 na Septemba 2015 wakati wa mchakato wa Mkopo wa USD 550 wa Serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard ya Uingereza
 
Wanakomolewa sababu ya uhusiano wao na babu wa ukawa!!!! Hili deal lingekuwa kule nalo lingepelekwa kuwa ni mali ya jeshi hivyo lisingehojiwa
Na huyo babu wa ukawa ndo alitumia pesa ya hiyo deal kumkatia Mwenyekiti ili amteme mzee wa mihogo
 
To be honest Mnyonge mnyongeni ila Magufuli means business akisema anapambana na ufisadi aisee.

Mpaka kuwa na courage ya kupambana na haya mawe......JK alikuwa anawachekea au na yeye wanampa chake!

Off all people..Kitilya? The most powerful man in the country. Leo yuko gerezani?

Shikamoo Magu!
 
Back
Top Bottom