Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Tumeshuhudia tokea Mwangosi auawe kinyama na polisi, septemba 2, mwaka huu, na jinsi, jeshi hilo la polisi, lilivyojitahidi kwa juhudi zote, kujifanya kuwa wao hawakuhusika, badala yake wakadai, kuna kitu kizito kimerushwa toka kwa wafuasi na viongozi wa Chadema, lakini kwa jinsi Mungu alivyo mkuu, aliwapa ujasiri wapiga picha, wakapata picha zenye ushahidi wa wazi, kuwa polisi ndiyo wamehusika na mauaji hayo. Sasa wasiwasi wa wananchi wengi ni kuwa huyo polisi waliyemfikisha mahakamani, wamelazimika tu kumfikisha mahakamani, kutokana na shinikizo kubwa sana la vyombo vya habari na wananchi, pamoja na wanaharakati. Sasa kutokana na mlolongo wa matukio, kama vile kumfikisha mtuhumiwa mahakamani na gari la kifahari, la Land Cruiser, polisi kuzuia kabisa, mtuhumiwa huyo, asipigwe picha na paparazi. Vile vile, kitendo cha Kamuhanda kutoshtakiwa na kuendelea na kazi, wakati inafahamika wazi kuwa yeye, ndiye aliyesimamia hiyo operesheni ya mauaji ya Mwangosi. Kwa mazingira hayo nadhani ipo haja kwa wanaharakati na wanasheria wazalendo, kutoa taarifa ya kuwa hatuna imani na mahakama hiyo, kama mashahidi wa kesi hiyo, ndiyo hao hao mapolisi, wanaozuia hata mtuhumiwa asipigwe picha! Kwa hiyo nadhani ingekuwa vyema, wanasheria wazalendo wakaangalia vifungu vya sheria, vinavyoweza kuruhusu kesi hiyo, ihamishiwe mahakama ya kimataifa,ya the Hague, ambako tunaamini haki itaweza kutendeka