Kesi ya mwanafunzi wa Law School of Tanzania aliyeomba iendeshwe LIVE yapangiwa Majaji

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,355
8,043
Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na mwanafunzi wa Shule ya Sheria kwa Vitendo (Law School of Tanzania – LST), Alexander Barunguza, ambayo ameiomba mahakama iruhusu mwenendo wake utangazwe mubasahara kwenye vyombo vya habari, imepangiwa jopo la majaji watakaoisikiliza.

Akizungumza na Mwananchi, leo jana, Septemba 14,2022, Barunguza amesema amepata hati ya wito kwa wadaiwa na kwamba imepangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu litakaloongozwa na Jaji Deo Nangela. Majaji wengine katika jopo hilo ni Ephery Sedekia Kisanya na Dk. Theodora Mwenegoha.

“Pia kesi imepangwa kutajwa Septemba 16, saa 8 mchana. Tayari nimeshapokea summons (hati ya wito wa mahakama), kwa ajili ya kuwapelekewa (wadaiwa) respondentsm,” amesema Baranguza.

Barunguza mwenye usajili namba SLT/2019/30/104 chuoni hapo, amefungua shauri la kikatiba Mahakama Kuu Masjala Kuu dhidi ya Shule hiyo ya Sheria, Jaji Dk. Benhajj Masoud (mkuu wa shule hiyo ya sheria) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Katika Shauri hilo la kikatiba namba 11 la mwaka 2022, Barunguza anapinga matokeo ya mitihiani yake ya muhula wa kwanza na wa pili mwaka 2019/2020 ambayo yanaonesha kwamba ameshindwa kufikisha alama za ushindi katika kozi mbili.

Anapinga kanuni na taratibu za rufaa baada ya rufaa yake ya kupinga matokeo ya mitihani hiyo, kuwa ni kinyume cha Katiba na kwamba katika mchakato wa rufaa yake hiyo ilyotupiliwa mbali hakupewa haki ya kusiklilizwa.

Vilevile anadai kuwa haki zake ya kuishi na usalama zimekiukwa au zinaelekea kukiukwa kutokana na kutishiwa maisha na mmoja wa walimu chuoni hapo wakati akiwa katika mchakato wa rufaa ya kupinga matokeo hayo, huku akidai kutengwa, kubaguliwa na kutokutambuliwa kama mwanafunzi.

Kufuatia kesi hiyo, Barunguza amemwandikia barua Jaji Kiongozi akiomba aridhie wakati wa usikilizaji wa shauri hilo tangu liendeshwe mubashara kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Barua hiyo ya juzi Jumanne, Septemba 13, 2022, anaeleza anaomba kesi hiyo iendeshwe mubashara ili kutoa fursa kwa ndugu na marafiki zake walioko nje ya nchi kufuatilia.

“Ninaomba mahakama yako Tukufu, kuruhusu na kuridhia kurushwa kwa matangazo ya moja kwa moja au mubashara (live) ya mwenendo wa shauri hili tangu siku ya kwanza ya shauri hili litakapotajwa na kuanza kusikilizwa,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Hata hivyo, anabainisha lengo la kuomba kesi hiyo iendeshwe mubasahara kuwa ni ili kutoa fursa kwa ndugu, marafiki na jamaa zake waishio nje ya nchi washriki kwa nji ya mtandao na vyombo vya habari kushuhudia yanayojiri katika shauri hilo.

Amezitaja baadhi ya nchi hizo waliko ndugu marafiki na jamaa zake hao kuwa ni pamoja na ngu waishio Marekani, Sweden, Lebanon na Afrika Kusini.

“Aidha ili kuhakikisha zoezi hili linafanyika kwa ufanisi mkubwa na kwa wakati, nimeandaa timu yangu ya wataalamu wa IT (Teknolojia ya Habari), ambao wako tayari kuanza kazi yao mara moja katika kurusha matangazo ya shauri hili.”anasema Barunguza na kuongeza:

“Pia niko tayari kutoa ushirikiano wote na wa kutosha pale ambapo mahakama itapendekeza njia tofauti ili kuhakikisha ndugu, rafiki na jamaa zangu waishio ughaibuni kuweza kupata matangazo ya moja kwa moja ya shauri hili kutokea mahakamani.”

“Aidha shauri hili ni la kikatiba na linahusisha kuvunjwa (zinazoelekea kuvunjwa) kwa haki zangu za binadamu ikiwemo haki ya kuishi au kuwa hai pamoja na usalama wangu (right of life and safety.”, anasisitiza Barunguza kwenye barua hiyo.

Hata hivyo uongozi wa mahakama bado haujatoa majibu ya maombi yake katika barua hiyo kuhusu kesi hiyo kuendeshwa kupitia vyombo vya habari mubashara iwapo utamkubalia au la.

MWANANCHI
 
Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na mwanafunzi wa Shule ya Sheria kwa Vitendo (Law School of Tanzania – LST), Alexander Barunguza, ambayo ameiomba mahakama iruhusu mwenendo wake utangazwe mubasahara kwenye vyombo vya habari, imepangiwa jopo la majaji watakaoisikiliza...
Nina wasiwasi Hawezi kushinda kesi kama hiyo labda isikilizwe Kenya. Moreover mahakama ina tendency ya kutoingilia mambo ya academics ie ina inclination ya kutoingilia maamuzi ya senate and the like in Higher learning institutions.

KWA TULIO WAVIVU KUSOMA MAKARATASI MENGI SOME EXCERPT KUTOKA KESI HIYO

courts have been reluctant to interfere in matters of academics in colleges and universities

However, there is also a considerable body of case laws to show that courts have been reluctant to interfere in matters of academics in colleges and universities especially through judicial review. See, for instance, R v. University of London ex parte Vijayatunga (1987) 3 All ER 222, Clerk v University of Lincolnshire and Humberside (2000) 3 All ER 763 and David Joseph Jumbe & Others v. The Council Dar es Salaam Institute of Technology & Others, Miscellaneous Civil Cause No. 112 of 2004 (unreported).

The reason is not far-fetched, whereas disciplinary proceedings in higher learning institutions deals with college or university students general conduct, academic affairs of colleges and universities lies at the heart of academic excellence for which examination of any kind be it written or oral, thesis or dissertation is a reliable measurement tool of knowledge and skill of the candidates and therefore, are meant to be honestly and honorably conducted by both colleges and universities as well as students such that courts are not the appropriate machinery to compel academic institutions to confer an academic award which is the exclusive monopoly of internal academic mechanisms within the respective colleges and universities and the aim being to maintain the integrity and quality of academic awards.

It is convenient to point out here that courts cannot compel colleges or universities to confer or grant an academic award, the minimum that courts can do is to direct colleges and universities to comply with existing academic machinery. The very purpose of which is to allow academic freedom and advance the course of academic excellence and the integrity of the examination process.

In view of the aforesaid, we find no merit in the appeal. Consequently, we dismiss it in its entirety with costs.

Soma kesi hii ingawa ni tofauti kidogo na hiyo
 

Attachments

  • PRAGIALISM_UNIVERSITY DAR ES SALAAM.pdf
    367 KB · Views: 10
Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na mwanafunzi wa Shule ya Sheria kwa Vitendo (Law School of Tanzania – LST), Alexander Barunguza...
Hao walimu wanamtishia kwa sababu ipi hasa ya msingi?

Mwanasheria mkuu wa serikali hapo anaingiaje kwenye ishu za chuo?
 
Barunguza mwenye usajili namba SLT/2019/30/104 chuoni hapo, amefungua shauri la kikatiba Mahakama Kuu Masjala Kuu dhidi ya Shule hiyo ya Sheria, Jaji Dk. Benhajj Masoud (mkuu wa shule hiyo ya sheria) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Mnyamma anamla mwenye mnyama, mambo haya mpaka raha
 
Nimeona mada za kuchambua taarifa ya kufeli kwa wanafunzi Law School of Tanzania.

Binafsi na mimi nimepitia Law School, na haya ndiyo ninayoyafahamu kuhusiana na hiki chuo.

1. Law School kiuhalisia, siyo sehemu ya mafunzo kwa vitendo kama mnavyosikia redioni.

2. Somo la field lipo, ila marks zake hazihusiki kwenye kubaini ufaulu. Yaani alama za somo la field hazina maana kwenye GPA calculation maana hazitambuliki.

3. Wanafunzi wa Law School hufundishwa kwa nadharia darasani, na kuingia semina kama ilivyo vyuo vikuu.

4. Mwalimu mmoja hutoa mhadhara kwa wanafunzi wote 600+ na akimaliza anaingia mwingine hadi siku inaisha.

5. Mada zinazofundishwa Law School ni zilezile mwanafunzi alifundishwa vyuoni ngazi ya degree na hakuna tofauti.

6. Muda wa mitihani haupo fair. Kwenye mtihani mmoja, kunakuwa na maswali ya kuandaa hati za mashtaka na madai nyingi mno kiasi kwamba muda wa kuandaa hati hizo hautoshi. Kwa wasijua, hati za kisheria uandaaji wake unahitaji kurejea vifungu vya sheria mbalimbali ambazo unakuwa unazo mezani(Acts).

7. Wahadhiri wa Law School huamini kwamba wanafunzi wao watafeli na mtu akifaulu wanashangaa sana. Yaani wapo kama miungu watu. Pale Law School hata secretary anamdharau mwanafunzi na anataka umuinamie kumsujudu.

8. Mahakimu, na waajiriwa wengine wenye uzoefu kwenye sheria wakienda kujiendeleza Law School nao hufeli pia.

9. Kuna wakati mahakimu walishauriwa wasijiendeleze Law School maana ni fedhea hakimu mzoefu unafeli Law School. Badala yake waliaambiwa watapewa utambulisho maalum kwamba wamefuzu vigezo vya sheria kwa vitendo.

10. Suplementary yaani mitihani ya kurudia haina kikomo Law School. Unaweza hata ukakaa na sup. hata miaka 40.

11. Law School ukikata rufaa ya matokeo haipatiwi majibu na unaweza ukaanza apya kusoma na kumaliza bila kupata majibu ya rufaa.

12. Law School unasoma masomo yote uliyofundishwa kwenye shahada ya sheria kwa miaka minne, lakini ukifika Law School unafundishwa kwa miezi 6 na unapewa mitihani. Halafu miezi mingine 6 unaenda field.
 
Nimeona mada za kuchambua taarifa ya kufeli kwa wanafunzi Law School of Tanzania.

Binafsi na mimi nimepitia Law School, na haya ndiyo ninayoyafahamu kuhusiana na hiki chuo.

1. Law School kiuhalisia, siyo sehemu ya mafunzo kwa vitendo kama mnavyosikia redioni.

2. Somo la field lipo, ila marks zake hazihusiki kwenye kubaini ufaulu. Yaani alama za somo la field hazina maana kwenye GPA calculation maana hazitambuliki.

3. Wanafunzi wa Law School hufundishwa kwa nadharia darasani, na kuingia semina kama ilivyo vyuo vikuu.

4. Mwalimu mmoja hutoa mhadhara kwa wanafunzi wote 600+ na akimaliza anaingia mwingine hadi siku inaisha.

5. Mada zinazofundishwa Law School ni zilezile mwanafunzi alifundishwa vyuoni ngazi ya degree na hakuna tofauti.

6. Muda wa mitihani haupo fair. Kwenye mtihani mmoja, kunakuwa na maswali ya kuandaa hati za mashtaka na madai nyingi mno kiasi kwamba muda wa kuandaa hati hizo hautoshi. Kwa wasijua, hati za kisheria uandaaji wake unahitaji kurejea vifungu vya sheria mbalimbali ambazo unakuwa unazo mezani(Acts).

7. Wahadhiri wa Law School huamini kwamba wanafunzi wao watafeli na mtu akifaulu wanashangaa sana. Yaani wapo kama miungu watu. Pale Law School hata secretary anamdharau mwanafunzi na anataka umuinamie kumsujudu.

8. Mahakimu, na waajiriwa wengine wenye uzoefu kwenye sheria wakienda kujiendeleza Law School nao hufeli pia.

9. Kuna wakati mahakimu walishauriwa wasijiendeleze Law School maana ni fedhea hakimu mzoefu unafeli Law School. Badala yake waliaambiwa watapewa utambulisho maalum kwamba wamefuzu vigezo vya sheria kwa vitendo.

10. Suplementary yaani mitihani ya kurudia haina kikomo Law School. Unaweza hata ukakaa na sup. hata miaka 40.

11. Law School ukikata rufaa ya matokeo haipatiwi majibu na unaweza ukaanza apya kusoma na kumaliza bila kupata majibu ya rufaa.

12. Law School unasoma masomo yote uliyofundishwa kwenye shahada ya sheria kwa miaka minne, lakini ukifika Law School unafundishwa kwa miezi 6 na unapewa mitihani. Halafu miezi mingine 6 unaenda field.
Duh...!.
P
 
Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na mwanafunzi wa Shule ya Sheria kwa Vitendo (Law School of Tanzania – LST), Alexander Barunguza, ambayo ameiomba mahakama iruhusu mwenendo wake utangazwe mubasahara kwenye vyombo vya habari, imepangiwa jopo la majaji watakaoisikiliza.

Akizungumza na Mwananchi, leo jana, Septemba 14,2022, Barunguza amesema amepata hati ya wito kwa wadaiwa na kwamba imepangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu litakaloongozwa na Jaji Deo Nangela. Majaji wengine katika jopo hilo ni Ephery Sedekia Kisanya na Dk. Theodora Mwenegoha.

“Pia kesi imepangwa kutajwa Septemba 16, saa 8 mchana. Tayari nimeshapokea summons (hati ya wito wa mahakama), kwa ajili ya kuwapelekewa (wadaiwa) respondentsm,” amesema Baranguza.

Barunguza mwenye usajili namba SLT/2019/30/104 chuoni hapo, amefungua shauri la kikatiba Mahakama Kuu Masjala Kuu dhidi ya Shule hiyo ya Sheria, Jaji Dk. Benhajj Masoud (mkuu wa shule hiyo ya sheria) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Katika Shauri hilo la kikatiba namba 11 la mwaka 2022, Barunguza anapinga matokeo ya mitihiani yake ya muhula wa kwanza na wa pili mwaka 2019/2020 ambayo yanaonesha kwamba ameshindwa kufikisha alama za ushindi katika kozi mbili.

Anapinga kanuni na taratibu za rufaa baada ya rufaa yake ya kupinga matokeo ya mitihani hiyo, kuwa ni kinyume cha Katiba na kwamba katika mchakato wa rufaa yake hiyo ilyotupiliwa mbali hakupewa haki ya kusiklilizwa.

Vilevile anadai kuwa haki zake ya kuishi na usalama zimekiukwa au zinaelekea kukiukwa kutokana na kutishiwa maisha na mmoja wa walimu chuoni hapo wakati akiwa katika mchakato wa rufaa ya kupinga matokeo hayo, huku akidai kutengwa, kubaguliwa na kutokutambuliwa kama mwanafunzi.

Kufuatia kesi hiyo, Barunguza amemwandikia barua Jaji Kiongozi akiomba aridhie wakati wa usikilizaji wa shauri hilo tangu liendeshwe mubashara kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Barua hiyo ya juzi Jumanne, Septemba 13, 2022, anaeleza anaomba kesi hiyo iendeshwe mubashara ili kutoa fursa kwa ndugu na marafiki zake walioko nje ya nchi kufuatilia.

“Ninaomba mahakama yako Tukufu, kuruhusu na kuridhia kurushwa kwa matangazo ya moja kwa moja au mubashara (live) ya mwenendo wa shauri hili tangu siku ya kwanza ya shauri hili litakapotajwa na kuanza kusikilizwa,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Hata hivyo, anabainisha lengo la kuomba kesi hiyo iendeshwe mubasahara kuwa ni ili kutoa fursa kwa ndugu, marafiki na jamaa zake waishio nje ya nchi washriki kwa nji ya mtandao na vyombo vya habari kushuhudia yanayojiri katika shauri hilo.

Amezitaja baadhi ya nchi hizo waliko ndugu marafiki na jamaa zake hao kuwa ni pamoja na ngu waishio Marekani, Sweden, Lebanon na Afrika Kusini.

“Aidha ili kuhakikisha zoezi hili linafanyika kwa ufanisi mkubwa na kwa wakati, nimeandaa timu yangu ya wataalamu wa IT (Teknolojia ya Habari), ambao wako tayari kuanza kazi yao mara moja katika kurusha matangazo ya shauri hili.”anasema Barunguza na kuongeza:

“Pia niko tayari kutoa ushirikiano wote na wa kutosha pale ambapo mahakama itapendekeza njia tofauti ili kuhakikisha ndugu, rafiki na jamaa zangu waishio ughaibuni kuweza kupata matangazo ya moja kwa moja ya shauri hili kutokea mahakamani.”

“Aidha shauri hili ni la kikatiba na linahusisha kuvunjwa (zinazoelekea kuvunjwa) kwa haki zangu za binadamu ikiwemo haki ya kuishi au kuwa hai pamoja na usalama wangu (right of life and safety.”, anasisitiza Barunguza kwenye barua hiyo.

Hata hivyo uongozi wa mahakama bado haujatoa majibu ya maombi yake katika barua hiyo kuhusu kesi hiyo kuendeshwa kupitia vyombo vya habari mubashara iwapo utamkubalia au la.

MWANANCHI

He is destroying his life and carrier
 
Nimeona mada za kuchambua taarifa ya kufeli kwa wanafunzi Law School of Tanzania.


Binafsi na mimi nimepitia Law School, na haya ndiyo ninayoyafahamu kuhusiana na hiki chuo.

1. Law School kiuhalisia, siyo sehemu ya mafunzo kwa vitendo kama mnavyosikia redioni.

2. Somo la field lipo, ila marks zake hazihusiki kwenye kubaini ufaulu. Yaani alama za somo la field hazina maana kwenye GPA calculation maana hazitambuliki.

3. Wanafunzi wa Law School hufundishwa kwa nadharia darasani, na kuingia semina kama ilivyo vyuo vikuu.

4. Mwalimu mmoja hutoa mhadhara kwa wanafunzi wote 600+ na akimaliza anaingia mwingine hadi siku inaisha.

5. Mada zinazofundishwa Law School ni zilezile mwanafunzi alifundishwa vyuoni ngazi ya degree na hakuna tofauti.

6. Muda wa mitihani haupo fair. Kwenye mtihani mmoja, kunakuwa na maswali ya kuandaa hati za mashtaka na madai nyingi mno kiasi kwamba muda wa kuandaa hati hizo hautoshi. Kwa wasijua, hati za kisheria uandaaji wake unahitaji kurejea vifungu vya sheria mbalimbali ambazo unakuwa unazo mezani(Acts).

7. Wahadhiri wa Law School huamini kwamba wanafunzi wao watafeli na mtu akifaulu wanashangaa sana. Yaani wapo kama miungu watu. Pale Law School hata secretary anamdharau mwanafunzi na anataka umuinamie kumsujudu.

8. Mahakimu, na waajiriwa wengine wenye uzoefu kwenye sheria wakienda kujiendeleza Law School nao hufeli pia.

9. Kuna wakati mahakimu walishauriwa wasijiendeleze Law School maana ni fedhea hakimu mzoefu unafeli Law School. Badala yake waliaambiwa watapewa utambulisho maalum kwamba wamefuzu vigezo vya sheria kwa vitendo.

10. Suplementary yaani mitihani ya kurudia haina kikomo Law School. Unaweza hata ukakaa na sup. hata miaka 40.

11. Law School ukikata rufaa ya matokeo haipatiwi majibu na unaweza ukaanza apya kusoma na kumaliza bila kupata majibu ya rufaa.

12. Law School unasoma masomo yote uliyofundishwa kwenye shahada ya sheria kwa miaka minne, lakini ukifika Law School unafundishwa kwa miezi 6 na unapewa mitihani. Halafu miezi mingine 6 unaenda field.
Engineers hatuna mambo haya ya Kijinga. Kaeni na Ungwini wenu huko.
 
Back
Top Bottom