Kesi ya mke wa karamagi

Ochu

JF-Expert Member
May 13, 2008
975
47
Kesi ya wizi wa mkufu na simu ya mkononi iliyokuwa ikimkabili mke wa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Naziri Karamagi, Nadia imeyeyuka baada ya Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam kuifutilia mbali.
Akitangaza kufutwa kwa kesi hiyo, hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo John Msafiri alisema, Mahakama yake imefikia hatua hiyo baada ya mlalamikaji Bi. Maselina Rweymamu kuiomba mahakama ifute shitaka hilo...“Mlalamikaji aliwasilisha hati ya kuiomba mahakama kukufutia kesi, kwa hiyo tunakueleza kuwa kesi yako imefutwa subiri taratibu zingine za kimahakama utakazotakiwa kufuata,” Msafiri alimweleza Nadia .

Awali, mwendesha mashtaka wa Polisi Nassoro Sisiwayaa alidai mahakamani hapo kuwa, Bi. Rweymamu aliiomba mahakama hiyo kumfutia kesi Bi. Nadia ili wamalizane nje ya mahakama.

Mke wa Karamagi ambaye ni mzungu mwenye asili ya kirusi aliburuzwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Juni 26, mwaka huu akikabiliwa na tuhuma za wizi.

Katika kesi hiyo ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa Polisi Nassoro Sisiwayaa kuwa, Juni 17 mwaka huu saa 5 asubuhi maeneo ya Oysterbay Jijini Dar es Salaam Nadia aliiba mkufu wa dhahabu wenye thamani ya Sh.90,000 na simu ya mkononi yenye thamani ya Sh.155,000 mali ya Maselina.

Hata hivyo, Nadia ambaye ni meneja wa mgahawa Colossian uliopo Jijini Dar es Salaam alikana mashitaka hayo na kuachiwa kwa dhamana hadi jana kesi yake ilipofutwa.
 
Last edited:
Kesi ya wizi wa mkufu na simu ya mkononi iliyokuwa ikimkabili mke wa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Naziri Karamagi, Nadia imeyeyuka baada ya Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam kuifutilia mbali.
Akitangaza kufutwa kwa kesi hiyo, hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo John Msafiri alisema, Mahakama yake imefikia hatua hiyo baada ya mlalamikaji Bi. Maselina Rweymamu kuiomba mahakama ifute shitaka hilo...“Mlalamikaji aliwasilisha hati ya kuiomba mahakama kukufutia kesi, kwa hiyo tunakueleza kuwa kesi yako imefutwa subiri taratibu zingine za kimahakama utakazotakiwa kufuata,” Msafiri alimweleza Nadia .

Awali, mwendesha mashtaka wa Polisi Nassoro Sisiwayaa alidai mahakamani hapo kuwa, Bi. Rweymamu aliiomba mahakama hiyo kumfutia kesi Bi. Nadia ili wamalizane nje ya mahakama.

Mke wa Karamagi ambaye ni mzungu mwenye asili ya kirusi aliburuzwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Juni 26, mwaka huu akikabiliwa na tuhuma za wizi.

Katika kesi hiyo ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa Polisi Nassoro Sisiwayaa kuwa, Juni 17 mwaka huu saa 5 asubuhi maeneo ya Oysterbay Jijini Dar es Salaam Nadia aliiba mkufu wa dhahabu wenye thamani ya Sh.90,000 na simu ya mkononi yenye thamani ya Sh.155,000 mali ya Maselina.

Hata hivyo, Nadia ambaye ni meneja wa mgahawa Colossian uliopo Jijini Dar es Salaam alikana mashitaka hayo na kuachiwa kwa dhamana hadi jana kesi yake ilipofutwa.

kwa kawaida mlalamikaji ni shahidi namba moja na hana nguvu ya kufuta kesi.
hii inakuwaje wanaJF? je toka lini kesi ya jinai ikafanyiwa usuluhishi nje ya mahakama? je DPP ana taarifa na hili?
 
Sasa huyo mlalamikaji kafuta kesi kwa sababu gani> Au alimsingizia mama wa watu!
 
Sasa huyo mlalamikaji kafuta kesi kwa sababu gani> Au alimsingizia mama wa watu!

kisheria mlalamikaji hawezi kufuta kesi ya jinai hata siku moja ni DPP tu ndo mwenye mamlaka. mlalamikaji ni shahidi tu. toka lini shahidi akafuta kesi?
 
Back
Top Bottom