Kesi ya Mbowe na wenzake imetufumbua macho, haki za Watanzania zipo mikononi mwa Jeshi la polisi

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,087
6,568
Sheria za Tanzania zipo wazi kabisa kuwa mtuhumiwa anatakiwa kukiri kwa hiari ili hiyo kiri iweze kutumika mahakamani. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 27 cha sheria ya ushahidi ya Tanzania.

Lakini kifungu cha 29 kinawapa kiburi polisi kupiga na kutesa watu maana kinasema kama mtu ataubaki ukweli kutokana na mateso au kipigo, maneno aliyokiri yatatumika kama ushahidi. Hii ina maana kama ukituhumiwa wizi alafu ukapigwa na kuteswa alafu ukapatikana na mali ya wizi basi maelezo yako yatakubalika mahakamani.

Ndio maana polisi wanachofanya ni kupiga na kutesa mtu yoyote, awe ametenda kosa au hajatenda ili mradi tu wabahatishe kumkuta na anahusika au hauhusiki.

Tunaona wazi kuwa unaweza kuteswa na kupigwa na polisi ukakubali, lakini wakaja kukuta ulikubali kwa kipigo au mateso ikiwa kama wakikosa kukukuta na kidhibiti au ushahidi wa kutosha na kujikuta wanakuachia au mahakama ikakuachaia.

Andha Kanoon
 
Sheria za Tanzania zipo wazi kabisa kuwa mtuhumiwa anakiwa kukiri kwa hiari ili hiyo kiri iweze kutumika mahakamani. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 27 cha sheria ya ushahidi ya Tanzania.
Ziko mikononi mwa Watu wasiojulikani wametutegulia kitendawili, tulikuwa tunawatafuta wasiojulikana
 
Sheria za Tanzania zipo wazi kabisa kuwa mtuhumiwa anakiwa kukiri kwa hiari ili hiyo kiri iweze kutumika mahakamani. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 27 cha sheria ya ushahidi ya Tanzania...
Ipo siku hao wanaofanya unyama watalipa hizo dhambi.
 
Kwanza kama ww sio mhalifu huwezi kufika mikononi mwa polisi. Ndio maana mahakama ipo pale kuamua, kama kweli adamoo aliteswa ama hakuteswa, ushahidi ndio utakao amua.

Usidhani kila alilolisema Adamoo ni la kweli mengi ameongea ili kujinasua kwenye majanga lkn mahakama ndio muamuzi wa mwisho.
 
😁😁😁
AIgmal.jpg
 
Back
Top Bottom