Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,087
- 6,568
Sheria za Tanzania zipo wazi kabisa kuwa mtuhumiwa anatakiwa kukiri kwa hiari ili hiyo kiri iweze kutumika mahakamani. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 27 cha sheria ya ushahidi ya Tanzania.
Lakini kifungu cha 29 kinawapa kiburi polisi kupiga na kutesa watu maana kinasema kama mtu ataubaki ukweli kutokana na mateso au kipigo, maneno aliyokiri yatatumika kama ushahidi. Hii ina maana kama ukituhumiwa wizi alafu ukapigwa na kuteswa alafu ukapatikana na mali ya wizi basi maelezo yako yatakubalika mahakamani.
Ndio maana polisi wanachofanya ni kupiga na kutesa mtu yoyote, awe ametenda kosa au hajatenda ili mradi tu wabahatishe kumkuta na anahusika au hauhusiki.
Tunaona wazi kuwa unaweza kuteswa na kupigwa na polisi ukakubali, lakini wakaja kukuta ulikubali kwa kipigo au mateso ikiwa kama wakikosa kukukuta na kidhibiti au ushahidi wa kutosha na kujikuta wanakuachia au mahakama ikakuachaia.
Andha Kanoon
Lakini kifungu cha 29 kinawapa kiburi polisi kupiga na kutesa watu maana kinasema kama mtu ataubaki ukweli kutokana na mateso au kipigo, maneno aliyokiri yatatumika kama ushahidi. Hii ina maana kama ukituhumiwa wizi alafu ukapigwa na kuteswa alafu ukapatikana na mali ya wizi basi maelezo yako yatakubalika mahakamani.
Ndio maana polisi wanachofanya ni kupiga na kutesa mtu yoyote, awe ametenda kosa au hajatenda ili mradi tu wabahatishe kumkuta na anahusika au hauhusiki.
Tunaona wazi kuwa unaweza kuteswa na kupigwa na polisi ukakubali, lakini wakaja kukuta ulikubali kwa kipigo au mateso ikiwa kama wakikosa kukukuta na kidhibiti au ushahidi wa kutosha na kujikuta wanakuachia au mahakama ikakuachaia.
Andha Kanoon