Kesi ya Mbowe na wanasheria wa Tigo na Airtel ikumbushe wenye mamlaka kutunza siri za wateja ni muhimu kujenga sekta imara ya benki na mawasiliano

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,308
45,618
Shahidi ambaye ni wakili katika kesi ya Mbowe kwa jina la Frank Kapara ameeleza kwa mlolongo mrefu uzoefu na utendaji wa kazi yake katika kampuni ya Tigo. Pia ameeleza jinsi gani anavyotoa taarifa za wateja kwa vyombo vingine pale anapohitajika kufanya hivyo. Maelezo yake anaonyesha ni rahisi sana kwa taarifa za wateja kutoka kampuni za simh kutolewa kwa vyombo kama polisi zinapotakiwa jambo ambalo si afya ksa faragha ya mawasiliano kwa wateja. Hali hiyo inaweza kuwa hivyo pia kwa mabenki.

Tatizo la upatikanaji kwa urahisi taarifa za wateja iwe kwenye mawasiliano, benki, hospitali au sehemu nyingine ni taarifa hizo kuweza kutumiwa vibaya na watu wenye nia ovu. Lakini pia kila binadamu anapenda na kuhusudu faragha. Hii ndio sababu imezifanya nchi nyingi zilizoendelea na kustaarabika kuweka sheria kali za kulinda siri za wateja hata za kawaida tu.

Pia duniani kuna ncho zinazotambulia kama nchi nzuri zaidi za watu kuhifadhi fedha zao na zimevutia watu wengi kutoka kila kona ya dunia kuhifadhi fedha zao. Nchi hizo ni pamoja na Panama, Cayman, Switzerland, Luxembourg, Seychelles,Singapore, Belize Ujerumani n.k. Sifa kuu katika nchi hizi ni utunzaji wa siri za wateja wao. Sifa hii imefanya nchi hizi kuwa na ukwasi mkubwa wa kifedha kwa njia ya mitaji inayotumika kuziendeleza. Ili upate taarifa za mteja katika nchi hizi ni lazima usote sana mahakamani na majaji wajiridhishe kwamba kweli kuna ulazima huo jambo ambalo huwa nadra sana majaji kukubali.

Kesi ya Mbowe inayoendelea iliamshe bunge kama mhimili na chombo cha kutunga sheria, kuweka sheria madhubuti za upatikanji taarifa za wateja katika simu, mabenki, hospitali na huduma nyingine. Hii itasaidia sana pia kuvutuia uwekezaji kutoka nje.
 
Hiyo yote ilikuwa ni master mind ya utawala wa Magufuli. Chini ya utawala wake haki ya kikatiba ya faragha Ni moja ya Sheria zilizovunjwa sana. Wahanga Ni wengi, Kama Membe, Makambas, Nape, Kinana, Mawaziri wote, wakuu wa mikoa, Wilaya nakadhalika.

Ninachojua faragha ya mtu inaweza kuingiliwa kwa Amri ya Mahakama. Kilichofanyika Chini ya Magufuli Ni uharamia na ubakaji wa Hali ya juu wa matakwa ya katiba.

Na Kuna uwezekano hata hacking ilifanyika Sana kwenye anuani za watu. Hii kesi itatupa mengi, Tuendelee kufuatilia. Lakini at least tumeshaona jinsi MITANDAO hii ya simu, Voda(kipindi Cha kina Membe) na Tigo ilivyo fragile and weak kutunza faragha za wateja wao.

Ni JAMIIFORUMS pekee, so far, ndio walioonesha ukomavu, uelewa na ufahamu katika kutetea faragha ya wateja wao. Heko Maxi Mello.
 
Haki ambayo hailindwi kwa sheria madhubuti ni vigumu kuzingatiwa. Lazima ziwepo sheria kwanza ambazo zinazuia haki hiyo kuvunjwa.
Hiyo yote ilikuwa ni master mind ya utawala wa Magufuli. Chini ya utawala wake haki ya kikatiba ya faragha Ni moja ya Sheria zilizovunjwa sana. Wahanga Ni wengi, Kama Membe, Makambas, Nape, Kinana, Mawaziri wote, wakuu wa mikoa, Wilaya nakadhalika...
 
Nini kilitokea kwenye kesi ya Sabaya?
 
Kama ilifanyika hivyo bila idhini ya mahakama ni kosa. Bahati mbaya sana hakuna watu wengi makini waliofuatilia au wanaofuatilia kesi za Sabaya kwa sababu ya udhalimu wake mwingi aliotuhumiwa nao kuwafanyia binadamu wenzake hata kabla ya kufikishwa mahakamani.
 
Wakuu, habari ndiyo hiyo, tumefumbuliwa macho na mwanasheria wa kampuni husika, Hakuna usiri wowote wa mteja unaolindwa.

Wala Hakuna taratibu zozote za kuwashirikisha wateja au mahakama pale taarifa zinapohitajika kitu kilicho kinyume na sheria.

Kuweni makini Sana wateja wa Tigo
 
Duniani kuwa safe inabidi uwe malaika au shetani hata shetani bado hayuko safe, anapigwa sana kwa jina la Yesu. Ndugu hata msaada wa kisheria ukihitaji bado uliowashtaki, watamnunua Mwendsha mashtaka au mwanasheria wako.
 
Duniani kuwa safe inabidi uwe malaika au shetani hata shetani bado hayuko safe,anapigwa sana kwa jina la Yesu.
ndugu hata msaada wa kisheria ukihitaji bado uliowashtaki ,watamnunua Mwendsha mashtaka au mwanasheria wako.
Yaani ilimradi uteseke tu
 
Naona kila mtu anazungumzia usiri kuhusu kutoa taarifa za wateja. Hili jambo sijaelewa, mfano ikitokea kuna jambo lolote baya linafanywa na mteja, kisheria imekaaje? Tigo inapaswa kumlinda mteja mmoja hata kama jambo lolote hatarishi linalenga wateja wengi?

Mmmh
 
Kumekucha wateja wa tigo_tz

Screenshot_20211102-152326_Twitter.jpg
 
Shahidi wa leo, kwenye kesi dhidi ya Mh. Mbowe na wenzake, bwana Fredy ametudhihirishia wateja wa mitandao ya simu kuwa polisi wanaweza kwenda kwenye hii mitandao na kuwaambia wenye mitandao wawape taarifa zako zote, kama mawasiliano, ulipo, miamala yako, wao hata hawaulizi ni kwaajili ya nini, wanawapa.

Watanzania hatupo salama kiusalama wala kifaragha, kila unapotumia mtandao wa simu. Polisi mwenye nia mbaya nawe, anaweza kwenda kwenye mitandao, na kuomba location yako, atapewa; akitaka kujua una mahusiano na mtu gani, atapewa; akitaka kujua simu yako ilituma hela kwa nani na ina balance kiasi gani, anapewa; atapewa chochote anachotaka alimradi tu ni polisi.

Hii ni wakeup call, kuwa usitumie mitandao ya simu kama siyo lazima sana. Labda utumie zaidi data ili mawasiliano yawe kwa whatsap, skype au telegram, huduma ambazo savers hazipo nchini, lakini siyo sms wala calls, au kutuma hela.
 
Naona kila mtu anazungumzia usiri kuhusu kutoa taarifa za wateja. Hili jambo sijaelewa, mfano ikitokea kuna jambo lolote baya linafanywa na mteja, kisheria imekaaje? Tigo inapaswa kumlinda mteja mmoja hata kama jambo lolote hatarishi linalenga wateja wengi?

Mmmh
Kama mteja mwenye namba ya kampuni husika anafanya vitendo vya uharifu na Polisi wakagundua, Taratibu ziko wazi kabisa mkuu kwa mujibu wa sheria

1) Mteja imempasa afahamishwe
2) Akikataa , kampuni husika wanatakiwa wapeleke maombi Mahakamani

Huyu jamaa kakataa kabisa kuwa wao sio kazi yao kuwalinda wateja kuhusiana na usili wao, na kwamba Polisi wakitaka details za wateja wao iwe kwa uchnguzi wa jinai au Laah wao wanatoa TU, kinyume na sheria 34
 
Wakili wa kampuni katuthibitishia kabisa kwamba kwao usiri wa wateja sio kipaumbele, kwao utii kwa mamlaka ndiyo kipaumbele

 
Back
Top Bottom