Kesi ya Mbowe: Hadi sasa sijaona ushahidi wowote unaoonesha kulikuwa na ugaidi

Takribani mashahidi wanne hadi sasa wameshatoa ushahidi wao lakini kati ya hao wote sijaona ushahidi wenye nguvu ya kuwatia hatiani watuhumiwa wa ugaidi.

Shahidi badala ya kuthibitisha uhusiano wa silaha iliyokamatwa na mtuhumiwa anakuja kutuambia silaha zilizokamatwa ni nzima kwani silaha kuwa nzima ni uthibitisho kuwa hiyo silaha ni ya mtuhumiwa.

Shahidi anasema alikutana na Mbowe January 2020 akiwa na gari la KUB wakati Mbowe alinyang’anywa gari tangu 2019 na January 2020 alikuwa mahabusu.

Shahidi anasema saini zinatofautiana kwasababu zingine alisaini akiwa amesimama zingine akiwa amekaa.

Mwingine anasema hakumbuki rangi ya shati maana hakuvaa miwani lkn aliweza kuona rangi ya bastola na kusoma namba zake.

Shahidi mwingine anasema watuhumiwa walipanga kulipua vituo vya mafuta, kukata miti, kupulizia viongozi sumu na kuua viongozi, walipoulizwa mliwakuta na vilipuzi hakuna, mapanga au shoka za kukatia miti hakuna, kuna vituo vya mafuta vilivyolipuliwa hakuna, kuna kiongozi kauawa hakuna.

Labda kama wamepanga kumfunga Mbowe wamfunge tu tujue moja lkn kwa ushahidi huu wa kuhisi kwa kesi kubwa kama hii ni kumuonea bure.
Very brief summary nimekupenda bure kutoa mwenendo wa kesi ulivyo
 
Vyeti vya kudesa. Polisi wana tatizo la vyeti wanavyo tumia sio vyao. Yaani form four leaver hajui maan aya terrorism na tourism?? Bado anaitwa ofisa wa serikali...
Mie nilitaraji kungekuwa na network ya ndani na nje ya nchi watu mpango mzima wa ungizwaji silaha unaomuhisisha mshtakiwa wa nne na wengine moja kwa moja
Lakini kinachofanyika km ni ku build evidence basi tutarajie mashahid elf mbili
 
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Morogoro Vituo gani kwamba vinatakiwa Kulipuliwa

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Maandamano yalitakiwa kufanyika Wapi Mkoa wa Morogoro

Shahidi: Si kumwambia
 
Mpaka sasa upande wa mashtaka wana mashahidi 12, katika wote waliotoa ushahidi mahakamani hasa ikizingatiwa shahidi huyu aliyepita Lut Denis Urio ndiye alikuwa Kiungo muhimu kuliko wote kubeba maamuzi ya kesi naye kaharibu na kuvurunda kabisa. Mpaka sasa kwakweli siioni "Angle" ya yeyoteya kisheria kumfunga Mbowe kwa Ugaidi kupitia ushahidi huu. Hiki kitu hakionekani kabisa.

Labda wamfunge kwa kulazimisha, kwa uongo, kwa maagizo ya kisiasa, lakini kwa angle ya kisheria hakuna kitu kama hicho. Kumfunga kisiasa ni kawaida sana na imewatokea wanasiasa wengi, na ikiwa itatokea akafungwa kisiasa kwa Pressure ya Kikundi flani cha watu wenye kuona raha yeye akiwa anateseka, I swear to God CCM ina muda mfupi mno, tutabisha lakini laana ya hii kitu itaimaliza CCM. 2025 CCM wasifikiri ndio Mbowe akifungwa itakuwa Raha yao kuingia madarakani tena. Time will tell, ngoja wamfunge tuone.
 
Back
Top Bottom