Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,396
Wazee wa baraza katika kesi ya mauaji ya mwafrika mmarekani George Floyd wanatarajiwa kurejea mchana huu na majibu ya hatia kwa mashtaka yote matatu.
Derek Chauvin ambae alikuwa askari polisi alimwekea goti shingoni George Floyd kwa dakika tisa na sekunde 29 alipokuwa akimkamata na kusababisha ukosefu wa hewa kwake hali ilompelekea kufariki.
Matarajio ya hukumu ya kukutwa na hatia kwa Wazee hao kunatokana na kutochukua muda mrefu wa kutafakari kila kosa kati ya matatu yanomkabili Derek Chauvin.
Kesi hiyo ya mauaji inafanyikia katika jiji la Minneapolis katika jimbo la Minnesota.
Chauvin anakabiliwa na mashtaka matatu ambayo ni mauaji ya bila kukusudia katika daraja la pili kosa linalobeba miaka 40 ya kifungo. Kosa la pili ni mauaji kwa kudharau taratibu na kanuni za kazi miaka 25 na kosa la tatu ni linabeba miaka 10 ambalo ni kusababisha kifo kwa kuweka goti kwenye shingo ya George Floyd bila kuzingatia hali ya muathirika.
Chanzo:
Vyanzo mbalimbali vya habari.
Update:
Derek Chauvin akielekezwa kwenda nje ya mahakama akiwa amefungwa pingu mara baada ya kusomewa uamuzi wa kukutwa na hatia ya mauaji ya George Floyd: Picha na Reuters
Derek Chauvin amekutwa na hatia ya mashtaka yote matatu na hukumu itatolewa baada ya wiki nane.
Wazee wa baraza walikaa karibu masaa kumi na nusu kufikiri na kupima uzito wa mashtaka yalowasilishwa na upande wa mashtaka kwenye mahakama na hakimu mkazi ya Hennepin jijini Minneapolis katika kesi hiyo ilochukua wiki tatu.
Chauvin alikuwa akikabiliwa na mashtaka matatu ta kumuua George Floys baada ya kumwekea goti katika shingo yake tarehe 25 mwezi March mwaka 2020, tukio lilozua maandamano nchini Marekani na kuungwa mkono duniani kote.
Chauvin mwenye umri wa miaka 45, anatazama miaka 75 jela ikiwa atatumikia miaka yote iliomo kwenye kila shtaka kwa pamoja.
Ikiwa kila shtaka litatumikiwa kivyake , Chauvin atatumikia kifungo cha miaka 25 jela kwa kila shtaka.
Derek Chauvin ambae alikuwa askari polisi alimwekea goti shingoni George Floyd kwa dakika tisa na sekunde 29 alipokuwa akimkamata na kusababisha ukosefu wa hewa kwake hali ilompelekea kufariki.
Matarajio ya hukumu ya kukutwa na hatia kwa Wazee hao kunatokana na kutochukua muda mrefu wa kutafakari kila kosa kati ya matatu yanomkabili Derek Chauvin.
Kesi hiyo ya mauaji inafanyikia katika jiji la Minneapolis katika jimbo la Minnesota.
Chauvin anakabiliwa na mashtaka matatu ambayo ni mauaji ya bila kukusudia katika daraja la pili kosa linalobeba miaka 40 ya kifungo. Kosa la pili ni mauaji kwa kudharau taratibu na kanuni za kazi miaka 25 na kosa la tatu ni linabeba miaka 10 ambalo ni kusababisha kifo kwa kuweka goti kwenye shingo ya George Floyd bila kuzingatia hali ya muathirika.
Chanzo:
Vyanzo mbalimbali vya habari.
Update:
Derek Chauvin akielekezwa kwenda nje ya mahakama akiwa amefungwa pingu mara baada ya kusomewa uamuzi wa kukutwa na hatia ya mauaji ya George Floyd: Picha na Reuters
Derek Chauvin amekutwa na hatia ya mashtaka yote matatu na hukumu itatolewa baada ya wiki nane.
Wazee wa baraza walikaa karibu masaa kumi na nusu kufikiri na kupima uzito wa mashtaka yalowasilishwa na upande wa mashtaka kwenye mahakama na hakimu mkazi ya Hennepin jijini Minneapolis katika kesi hiyo ilochukua wiki tatu.
Chauvin alikuwa akikabiliwa na mashtaka matatu ta kumuua George Floys baada ya kumwekea goti katika shingo yake tarehe 25 mwezi March mwaka 2020, tukio lilozua maandamano nchini Marekani na kuungwa mkono duniani kote.
Chauvin mwenye umri wa miaka 45, anatazama miaka 75 jela ikiwa atatumikia miaka yote iliomo kwenye kila shtaka kwa pamoja.
Ikiwa kila shtaka litatumikiwa kivyake , Chauvin atatumikia kifungo cha miaka 25 jela kwa kila shtaka.