"Kesi ya Manara inafundisha kuwa,yeyote awe na haki asiwe na haki atafungiwa tu na wenye mamlaka"!!

Song of Solomon

JF-Expert Member
Aug 5, 2021
2,733
5,489
Ujumbe Kutoka Kwa Kolo Anaeajielewa


Toka sakata la kinidhamu na labda la kijinai lifanyike pale uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha, bado hakuna taswira sahihi ya nini hasa kilichosababisha hali ile na ukweli halisi wa maneno yaliyozungumzwa kwenye eneo husika.

Nani alisema nini na chanzo kilikuwa nini, vyote hivyo havisemwi bali tunasikia maneno ya Upande mmoja zaidi, kuwa Haji Manara alisema hivi na vile, wakati video inaonesha majibizano, je, upande wa pili ulikuwa unasema nini ??, Hatuambiwi !!!

Kesi hii itufungue akili juu ya Sheria na kanuni za makosa zinavyotekelezwa na Kamati ya Maadili dhidi ya mtu yeyote na si kuchagua upande kwa sababu za kishabiki au kutafuta afadhali au kuona kwa kuwa fulani limemfika basi wacha limfike kwa kuwa si mimi lililonifika.

Tunaweza kuanza kwa kusema siku zote mlikuwa wapi wakati fulani au fulani anakumbwa na adhabu kupitia sheria hizo hizo na kudhani hatuna sababu ya kuziongelea sasa kwa upofu ule tuliokuwa nao hapo awali, lakini Shaaban Robert katika Kitabu chake cha Kusadikika aliandika.."Shujaa huwa hapatikani mpaka tukio kubwa litokee."

Itoshe kuona kuwa hili ni tukio kubwa kwa kuwa linahusisha mamlaka kuu ya soka na lilifanyika katika moja ya matukio makubwa na hata waliokuwepo kwenye eneo husika wanatosha kuitwa wakubwa, hivyo wanaosema kwa nini iwe sasa, tunawashauri wanyamaze tu kwa kuwa uwezo wao wa kujua sababu za mambo makubwa kutokea na kuleta mabadiliko ni mdogo na hatuwezi kupoteza muda kuupa nafasi.

Hukumu dhidi ya Manara ituamshe kwenye mambo kadhaa ambayo kesho na Keshokutwa utajikuta mtuhumiwa ni wewe na lazima utiwe hatiani kwa kuwa wanaokushtaki tayari walishajiandaa kukuadhibu.

Ni wazi kuwa Manara alishakuwa na ameshakuwa na Maneno makali ambayo wakati mwingine huleta taharuki na kuamsha hisia hasi dhidi yake au dhidi ya eneo analowajibikia, hilo halina ubishi na ndilo linaloweza kumfanya akawa ameshahukumiwa hata kama ataitwa kujitetea.

Maswali ni mengi kuhusu hukumu dhidi yake lakini ambayo pengine yangeweza kuwa majibu ya leo na kesho kwenye eneo hilo hilo la Kamati ya Maadili ni;

Nani alikuwa mshtaki wa Manara ?

Swali hili limekuwa muhimu sana kwani imekuwa kawaida kusikia mtu ameitwa Kamati ya Maadili bila kujua mshtaki wake hasa ni nani?

Kwenye misingi ya haki lazima awepo mshtaki kwani ndiye atakayetakiwa kutoa au kuleta ushahidi ambao utaondoa shaka ya wenye mamlaka za kuhukumu ili watende haki.

Lakini kwa asili ya kinachoonekana kwa wengi ni wazi kuwa mshtaki wa Manara ndio huyo huyo aliyekuwa mtoa hukumu.

Nani aliyepeleka ushahidi dhidi ya Manara??

Kimsingi lazima mshtaki ambaye hapa ni wazi anahesabika kuwa Rais wa TFF ndiye ambaye alipaswa kupeleka kesi na ushahidi au mashahidi dhidi ya kile kilichoonekana kuwa ni utovu wa nidhamu au kosa lililostahili adhabu, lakini hakuna sehemu yoyote tunayoambiwa kuwa mshtaki au shahidi alitoa ushahidi kadha wa kadha unaomtia hatiani mtuhumiwa.

Kosa dhidi ya Manara ni lipi na nani alitoa ushahidi usioacha shaka??

Hapa ndipo palipojaa mkanganyiko kwa kuwa haionekani popote aliyetakiwa kuwa Mshtaki na Shahidi wa muhimu kujitokeza popote au kuitwa kwenye Kamati husika ili kueleza au kuhojiwa na kuthibitisha makosa dhidi ya Manara, tunachoona ni nukuu tu za maneno kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati kuwa Manara alisikika akisema na sio shahidi au mashahidi walimsikia akisema, na pia watuambie aliposema alijibiwa nini ??

Anyway.

Ni wazi hata kwa muonekano wa video ile isiyokuwa na maneno yanayosikika ilikuwa wazi kuwa kulikuwa na tukio lisilo la kawaida na hivyo haikupaswa kwa mtu yeyote na si Manara pekee, kufanya au kuhusika na tukio lolote linaloleta taharuki au kuvunja sheria kwa sababu yoyote ile.

Suala zima kwa jinsi linavyoonekana kuendeshwa ni wazi linaondoa sifa za kuhukumiana na hata linachafua nafasi ya Urais wa TFF kwa kuwa itaonekana na mpaka sasa inaonekana kama ni hukumu inayotokana na maelekezo au iliyokusudia kulinda tu nafasi ya Urais bila watoa hukumu kujali kuwa hata yeye Rais alipaswa kuitwa na kuhojiwa ukweli wa kile kilichotokea hata kama yeye hakupeleka mashtaka moja kwa moja ili kila mmoja ajue alikuwa na maoni gani, vp kama kesho atajitokeza kwenye Press na kusema walikuwa wanataniana ??.

Wakati wa mzozo ule, Rais alikuwa anajibu nini ??

Video inaonesha kuna majibizano, je Rais alikuwa anajibu nini au alikuwa anamnasihi Haji Manara aende Msikitini kuswali ?? Majibu yake hasa dhidi ya maneno yanayosemwa kuwa makali ya Haji yalikuwa yapi??

Najua ipo furaha kumuona Haji Manara amefungiwa lakini waliomfungia wanatuachia ujumbe gani kuhusu misingi ya kesi na haki zake katika uendeshaji, tunacheka leo kwa Manara, kesho nasi tunangojewa kufanywa mfano kwa Wengine..!!!

Kwa msingi wa hoja zote hapo juu, Sisemi kuwa Manara kaonewa au hajaonewa, bali nasema kuwa haki dhidi ya shauri la Manara ni wazi kuwa haikuonekana kutendeka !!!

Imenyesha sana, panapovuja panabomoka !!!
 
Ujumbe Kutoka Kwa Kolo Anaeajielewa


Toka sakata la kinidhamu na labda la kijinai lifanyike pale uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha, bado hakuna taswira sahihi ya nini hasa kilichosababisha hali ile na ukweli halisi wa maneno yaliyozungumzwa kwenye eneo husika.

Nani alisema nini na chanzo kilikuwa nini, vyote hivyo havisemwi bali tunasikia maneno ya Upande mmoja zaidi, kuwa Haji Manara alisema hivi na vile, wakati video inaonesha majibizano, je, upande wa pili ulikuwa unasema nini ??, Hatuambiwi !!!

Kesi hii itufungue akili juu ya Sheria na kanuni za makosa zinavyotekelezwa na Kamati ya Maadili dhidi ya mtu yeyote na si kuchagua upande kwa sababu za kishabiki au kutafuta afadhali au kuona kwa kuwa fulani limemfika basi wacha limfike kwa kuwa si mimi lililonifika.

Tunaweza kuanza kwa kusema siku zote mlikuwa wapi wakati fulani au fulani anakumbwa na adhabu kupitia sheria hizo hizo na kudhani hatuna sababu ya kuziongelea sasa kwa upofu ule tuliokuwa nao hapo awali, lakini Shaaban Robert katika Kitabu chake cha Kusadikika aliandika.."Shujaa huwa hapatikani mpaka tukio kubwa litokee."

Itoshe kuona kuwa hili ni tukio kubwa kwa kuwa linahusisha mamlaka kuu ya soka na lilifanyika katika moja ya matukio makubwa na hata waliokuwepo kwenye eneo husika wanatosha kuitwa wakubwa, hivyo wanaosema kwa nini iwe sasa, tunawashauri wanyamaze tu kwa kuwa uwezo wao wa kujua sababu za mambo makubwa kutokea na kuleta mabadiliko ni mdogo na hatuwezi kupoteza muda kuupa nafasi.

Hukumu dhidi ya Manara ituamshe kwenye mambo kadhaa ambayo kesho na Keshokutwa utajikuta mtuhumiwa ni wewe na lazima utiwe hatiani kwa kuwa wanaokushtaki tayari walishajiandaa kukuadhibu.

Ni wazi kuwa Manara alishakuwa na ameshakuwa na Maneno makali ambayo wakati mwingine huleta taharuki na kuamsha hisia hasi dhidi yake au dhidi ya eneo analowajibikia, hilo halina ubishi na ndilo linaloweza kumfanya akawa ameshahukumiwa hata kama ataitwa kujitetea.

Maswali ni mengi kuhusu hukumu dhidi yake lakini ambayo pengine yangeweza kuwa majibu ya leo na kesho kwenye eneo hilo hilo la Kamati ya Maadili ni;

Nani alikuwa mshtaki wa Manara ?

Swali hili limekuwa muhimu sana kwani imekuwa kawaida kusikia mtu ameitwa Kamati ya Maadili bila kujua mshtaki wake hasa ni nani?

Kwenye misingi ya haki lazima awepo mshtaki kwani ndiye atakayetakiwa kutoa au kuleta ushahidi ambao utaondoa shaka ya wenye mamlaka za kuhukumu ili watende haki.

Lakini kwa asili ya kinachoonekana kwa wengi ni wazi kuwa mshtaki wa Manara ndio huyo huyo aliyekuwa mtoa hukumu.

Nani aliyepeleka ushahidi dhidi ya Manara??

Kimsingi lazima mshtaki ambaye hapa ni wazi anahesabika kuwa Rais wa TFF ndiye ambaye alipaswa kupeleka kesi na ushahidi au mashahidi dhidi ya kile kilichoonekana kuwa ni utovu wa nidhamu au kosa lililostahili adhabu, lakini hakuna sehemu yoyote tunayoambiwa kuwa mshtaki au shahidi alitoa ushahidi kadha wa kadha unaomtia hatiani mtuhumiwa.

Kosa dhidi ya Manara ni lipi na nani alitoa ushahidi usioacha shaka??

Hapa ndipo palipojaa mkanganyiko kwa kuwa haionekani popote aliyetakiwa kuwa Mshtaki na Shahidi wa muhimu kujitokeza popote au kuitwa kwenye Kamati husika ili kueleza au kuhojiwa na kuthibitisha makosa dhidi ya Manara, tunachoona ni nukuu tu za maneno kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati kuwa Manara alisikika akisema na sio shahidi au mashahidi walimsikia akisema, na pia watuambie aliposema alijibiwa nini ??

Anyway.

Ni wazi hata kwa muonekano wa video ile isiyokuwa na maneno yanayosikika ilikuwa wazi kuwa kulikuwa na tukio lisilo la kawaida na hivyo haikupaswa kwa mtu yeyote na si Manara pekee, kufanya au kuhusika na tukio lolote linaloleta taharuki au kuvunja sheria kwa sababu yoyote ile.

Suala zima kwa jinsi linavyoonekana kuendeshwa ni wazi linaondoa sifa za kuhukumiana na hata linachafua nafasi ya Urais wa TFF kwa kuwa itaonekana na mpaka sasa inaonekana kama ni hukumu inayotokana na maelekezo au iliyokusudia kulinda tu nafasi ya Urais bila watoa hukumu kujali kuwa hata yeye Rais alipaswa kuitwa na kuhojiwa ukweli wa kile kilichotokea hata kama yeye hakupeleka mashtaka moja kwa moja ili kila mmoja ajue alikuwa na maoni gani, vp kama kesho atajitokeza kwenye Press na kusema walikuwa wanataniana ??.

Wakati wa mzozo ule, Rais alikuwa anajibu nini ??

Video inaonesha kuna majibizano, je Rais alikuwa anajibu nini au alikuwa anamnasihi Haji Manara aende Msikitini kuswali ?? Majibu yake hasa dhidi ya maneno yanayosemwa kuwa makali ya Haji yalikuwa yapi??

Najua ipo furaha kumuona Haji Manara amefungiwa lakini waliomfungia wanatuachia ujumbe gani kuhusu misingi ya kesi na haki zake katika uendeshaji, tunacheka leo kwa Manara, kesho nasi tunangojewa kufanywa mfano kwa Wengine..!!!

Kwa msingi wa hoja zote hapo juu, Sisemi kuwa Manara kaonewa au hajaonewa, bali nasema kuwa haki dhidi ya shauri la Manara ni wazi kuwa haikuonekana kutendeka !!!

Imenyesha sana, panapovuja panabomoka !!!
Wenye akili kubwa tu watakuelewa.
Umechambua kwa uwezo uliotukuka.
Wachambuzi wetu wameacha kuchambua mpira wanachambua sheria zinazohukumu makosa ya mtu. Sijui wamesomea wapi
 
Siku ya tukio jemedari alipost kuelezea sintofahamu iliyotokea uwanjani lakini Manara alikuja kukanusha.

Tena alikanusha kwa kauli mbovu akidai Jemedari anamuandama kama aliwahi kutembea na mke wake basi aseme.

Kwani yeye alivyofundwa hawezi kabisa kubishana na mkubwa wake. Na kwa kusingiziwa huko na Jemedari anafikiria kufungua shauri mahakamani dhidi yake.

Sio siri mimi nilimuamini Manara na nilimuona Jemedari kama mtu fulani mwenye chuki binafsi.

Lakini suddenly tukasikia tamko kutoka TFF likielezea kile kile alicho post Jemedari masaa machache kupita.

Lakini pia bado nilibaki njia panda mpaka pale alipoonekana kwa Karia akisema alienda kuomba radhi.

Hapa Manara alitudanganya wengi tuliingia kingi kuwa anasingiziwa.

Na baada ya hapo aliitisha press akiomba radhi kwa umma kuwajulisha watu kuwa ni kweli alikosea.

Na moja ya kauli zake kwenye hiyo press kama mtakumbuka alisema yeye haombi msamaha eti kwasababu asihukumiwe.

Kama kamati ya maadili itakaa na kuona kuna haja ya mimi kuhukumiwa haina shida.

Yale yalikuwa ni maneno ya kiungwana sana kwenye ile interview

Lakini kwa bahati mbaya hapa tena mchizi alikuwa anatudanganya kwa mara ya pili.

Hukumu imetoka akapost kuonesha kukubaliana na matokeo na kusema yote heri inshallah.

Hapa alitudangaya tena kuwa kile alichokisema mwanzo kwenye interview kuwa hata akihukumiwa ni fresh basi post hii ilikuwa inathibitisha maneno yake.

Huu ulikuwa ni uwongo wa tatu.

Press ya juzi hapo ndio kaja kuharibu, kaongea vitu ambavyo alipaswa kuviongea mahakamani

Kazungumza maneno ambayo alijaribu kutoa picha ya upande wa pili

Lakini huu yaweza kuwa ni uwongo wa nne.

Hupaswi kumuamini muongo hata kama akiongea ukweli

Kwa wote ambao mnaona hoja zake zina sound good ebu jaribu kufikiria angezitoa kwenye mahakama zisingekuwa na msaada kwake?

Au kwakua hili swala linahusu sheria na wengi wetu sheria hatuzijui na ndio maana inakuwa rahisi kumuona manara kaonewa?
 
Siku ya tukio jemedari alipost kuelezea sintofahamu iliyotokea uwanjani lakini Manara alikuja kukanusha.

Tena alikanusha kwa kauli mbovu akidai jrmedari anamuandama kama aliwahi kutembea na mke wake basi aseme.

Kwani yeye alivyofundwa hawezi kabisa kubishana na mkubwa wake. Na kwa kusingiziwa huko na jemedari anafikiria kufungua shauri mahakamanindhidi yake.

Sio siri mimi nilimuamini Manara na nilimuona Jemedari kama mtu fulani mwenye chuki binafsi.

Lakini suddenly tukasikia tamko kutoka TFF likielezea kile kile alicho lost Jemedari masaa machache kupita.

Lakini pia bado nilibaki njia panda mpaka pale alipoonekana kwa Karia akisema alienda kuomba radhi.

Hapa Manara alitudanganya wengi tuliingia kingi kuwa anasingiziwa

Na baada ya hapo aliitisha press akiomba radhi kwa umma kuwajulisha watu kuwa ni kweli alikosea.

Na moja ya kauli zake kwenye hiyo press kama mtakumbuka alisema yeye haombi msamaha eti kwasababu asihukumiwe.

Kama kamati ya maadili itakaa na kuona kuna haja ya mimi kuhukumiwa haina shida.

Yale yalikuwa ni maneno ya kiungwana sana kwenye ile interview

Lakini kwa bahati mbaya hapa tena mchizi alikuwa anatudanganya kwa mara ya pili

Hukumu imetoka akapost kuonesha kukubaliana na matokeo na kusema yote heri inshallah

Hapa alitudangaya tena kuwa kile alichokisema mwanzo kwenye interview kuwa hata akihukumiwa ni fresh basi post hii ilikuwa inathibitisha maneno yake.

Huu ulikuwa ni uwongo wa tatu

Press ya juzi hapo ndio kaja kuharibu, kaongea vitu ambavyo alipaswa kuviongea mahakamani

Kazungumza maneno ambayo alijaribu kutoa picha ya uoamde wa pili

Lakini huu utakuwa ni uwongo wa nne

Hupaswi kumuamini muongo hata kama akiongea ukweli

Kwa wote ambao mnaona hoja zake zina sound good ebu jaribu kufikiria angezitoa kwenye mahakama zisingekuwa na msaada kwake?

Au kwakua hili swala linahusu sheria na wengi wetu sheria hatuzijui na ndio maana inakuwa rahisi kumuona manara kaonewa?
Mkuu watu kama wewe ndio mnapaswa kujadili hii issue. Hii ndio jamii forum haswa
Hoja kwa hoja sio hoja kwa kejeli .
Kongole
 
Mpira wetu bado unatawaliwa na wahuni wengi. Kuanzia wachezaji, wafanyakazi kwenye timu na hata hao tiefuefu wote bado wanafikiri mpira wa Tanzania ni yanga na simba. Kimsingi kinachoendelea ni matokeo ya kutotambua mpira kuwa ni sekta ya ajira kama utalii,kilimo,uvuvi na biashara nyingine. Tuna mazuzu wengi wamo humo na hawataki kuelimishwa.
 
Siku ya tukio jemedari alipost kuelezea sintofahamu iliyotokea uwanjani lakini Manara alikuja kukanusha.

Tena alikanusha kwa kauli mbovu akidai Jemedari anamuandama kama aliwahi kutembea na mke wake basi aseme.

Kwani yeye alivyofundwa hawezi kabisa kubishana na mkubwa wake. Na kwa kusingiziwa huko na Jemedari anafikiria kufungua shauri mahakamani dhidi yake.

Sio siri mimi nilimuamini Manara na nilimuona Jemedari kama mtu fulani mwenye chuki binafsi.

Lakini suddenly tukasikia tamko kutoka TFF likielezea kile kile alicho post Jemedari masaa machache kupita.

Lakini pia bado nilibaki njia panda mpaka pale alipoonekana kwa Karia akisema alienda kuomba radhi.

Hapa Manara alitudanganya wengi tuliingia kingi kuwa anasingiziwa.

Na baada ya hapo aliitisha press akiomba radhi kwa umma kuwajulisha watu kuwa ni kweli alikosea.

Na moja ya kauli zake kwenye hiyo press kama mtakumbuka alisema yeye haombi msamaha eti kwasababu asihukumiwe.

Kama kamati ya maadili itakaa na kuona kuna haja ya mimi kuhukumiwa haina shida.

Yale yalikuwa ni maneno ya kiungwana sana kwenye ile interview

Lakini kwa bahati mbaya hapa tena mchizi alikuwa anatudanganya kwa mara ya pili.

Hukumu imetoka akapost kuonesha kukubaliana na matokeo na kusema yote heri inshallah.

Hapa alitudangaya tena kuwa kile alichokisema mwanzo kwenye interview kuwa hata akihukumiwa ni fresh basi post hii ilikuwa inathibitisha maneno yake.

Huu ulikuwa ni uwongo wa tatu.

Press ya juzi hapo ndio kaja kuharibu, kaongea vitu ambavyo alipaswa kuviongea mahakamani

Kazungumza maneno ambayo alijaribu kutoa picha ya upande wa pili

Lakini huu yaweza kuwa ni uwongo wa nne.

Hupaswi kumuamini muongo hata kama akiongea ukweli

Kwa wote ambao mnaona hoja zake zina sound good ebu jaribu kufikiria angezitoa kwenye mahakama zisingekuwa na msaada kwake?

Au kwakua hili swala linahusu sheria na wengi wetu sheria hatuzijui na ndio maana inakuwa rahisi kumuona manara kaonewa?
Wanasema ukiwa mwongo uwe na kumbukumbu
 
Back
Top Bottom