KESI YA TUNDU LISSU CCM WAZIDI KUJICHANGANYA.
SHAHIDI:23.
SHAHIDI Stephen Jude, 37, Anaishi Dar, Tabata.
Mtaalamu wa ICT, and information and communication technology. Elimu yake ni ICT-Higher national Diploma 1999, London. Cyberom Certified network-Masuala ya usalama ya kimtandao.
Kwa miaka kadhaa nilikuwa katika technical support, and customer service. ( Head of Department.). katika kampuni ya Certcom Africa Limited, na sasa ni business development and public relations katika kampuni hiyo.
Wakili: Upo mahakamani, ni nini hasa kimekufanya uje hapa kuja kutoa ushahidi.
PW: Nilipata mawasiliano kama wiki mbili hivi, nilitumiwa documents ili niweze kujua kama zimeandaliwa katika Chanzo kimoja., Nilifanya physical identification, na baadaye technological identification
JAJI; Samahani wakili, niambie kama shahidi wako anafanya kazi, na anatambuliwa na serikali au NGO?.
Wakili:Kwa kuwa yupo hapa, naomba aseme mwenyewe.
PW: Mimi niliwahi kusaidia kuandaa website ya Taifa, iliyozinduliwa na Mkapa,
JAJI: Mimi sihitaji mambo ya Mkapa, je uliwahi kutangazwa kwenye gazeti la serikali?
JAJI: Basi huna sifa
Umesema kuwa ulipewa Nyaraka, je tukikuonyesha unaweza kuzikumbuka?
WAKILI:Tusaidie umeona nini?
PW: Nimgeundua kuwa zote zimeandikwa kwa Times New Roman., Jingine ni ‘font size' zote zimefanana katika barua zote.
JAJI: Tumbie nini unaona, acha kutueleza mambo ya font size, utuambie yanayoonekana kwa macho kila mtu aweze kuona. Kwanza haupo qualified, na hujawahi kutangazwa na gazeti la serikali, hivyo tunasikiliza tu ushahidi wako.
MASWALI:
T/L: Umewahi kuniona mahali?
PW: Ukweli sikufahamu kabisa.
T/L: Umewahi kuniona nikiandika chochote kwa mkono?
PW: Kwa kuwa sikufahamu sijawahi kukuona pia.
T/L; Vile vile hujawahi kuniona nina type barua popote
PW: NDIYO.
T/L: Hizo barua kwa kuzingalia tu unaweza kumwambia jaji zimeandikwa na nani?
PW: haiwezekani hata kwa kutumia vifaa
T/L: Mimi nimeshtakiwa kwenye kesi hii kwa sababu inadaiwa kuwa hizo barua nimeandika mimi, kwa muda uliokaa nazo unaweza kusema kuwa barua hizo nimeandika mimi?
PW: katika barua hizi sijaona jina lako
T/L: Kwa hiyo huwezi kusema kuwa zimeandikwa na Lissu?
PW: Hilo haliwezekani.
T/L Katika kuzifananisha fananisha kuna kitu hujakisahau?
PW: Kipo
T/L. Unaweza kumweleza Jaji?
PW: Jaji naomba niangalie karatasi nilipoandika majibu.
JAJI: Sikuruhusu
T/L. Angalia barua zote, uniambie kama hazina muhuri wa ‘received' zinazofanana. Mwambie jaji kama mhuri unafanana au haufanani?
PW; Zinafanana
T/L. Mbona hiyo hukutaja hiyo wakati unajieleza?
PW: Nilipoletewa niliambiwa niangalie kama zinatoka katika chanzo kimoja au la?
T/L. Uliagizwa na nani?
PW: Wakili Wasonga
T/L. Ulilipwa?
PW: SIKULIPWA.
T/L. Hiyo kampuni unayofanyia kazi ni kampuni au ni kituo cha misaada?
PW. Ni kampuni ya biashara.
T/L. Na wewe ni mfanykazi wa kampuni hiyo na unalipwa mshahara na kuifanyia kazi kampuni?
PW: Ni kweli
T/L. Mweleze jaji kwanini katika hili hukulipwa wakati ulitumia muda wa kampuni?
PW; Huwa hatulipwi kabla.
T/L. Kwa hiyo utalipwa ukitoka hapa kizimbani kwa ushahidi unaoutoa?
Pw: NDIYO.
T/L. Mwambie Jaji kama maandishi uliyosema ni Times New roman, yapo katika computer zote zinazotumia Microsoft word? Iwe Kenya, iwe Uganda, au hata mbinguni?
PW: Ndiyo.
T/L. Je kuna tatizo kutumia ‘Times New Roman kuandika barua?
PW: Hakuna
T/L; Kwa kuangalia hayo tu unaweza kusema barua imeandikwa na nani?
PW: Huwezi kabisa kujua.
T/L, Unajua ku copy na kupaste? Pamoja na kusave?
NDIYO.
Unafahamu Flash DISK?
KESI Inaendelea, tutaendelea kuwapa yanayojiri